Alhamisi, 18 Ramadan 1445 | 2024/03/28
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

Afisi ya Habari
Kitengo cha Wanawake

H.  23 Safar 1439 Na: 1439/004
M.  Jumapili, 12 Novemba 2017

Taarifa kwa Vyombo vya Habari


Watoto wa Rohingya Wanadhalilishwa Mikononi mwa Mabudha! Je, Wanaye Mtetezi?

Shirika la misaada la Médecins Frontiéres, limeripoti kuwa zaidi ya nusu ya wasichana katika kambi ya wakimbizi wa Rohingya eneo la Cox's Bazar, Bangladesh ambao limewatibu baada ya kudhulimiwa kimapenzi na kubakwa nchini Myanmar wako chini ya umri wa miaka 18, na wengine wako chini ya miaka 10. Limeeleza kuwa mamia ya wasichana wa Rohingya wamepewa usaidizi wa kimatibabu na wa kisaikolojia katika kliniki yake mjini Kutupalong inayotibu wahanga wa dhulma za kijinsia lakini likasisitiza kuwa hao ni sehemu tu ya wale wanao amanika kudhulumiwa kimapenzi na kubakwa na majeshi katili ya kibudha tangu kutokea kwa kampeni ya mauaji ya halaiki dhidi ya Waislamu wa Rohingya mnamo Agosti. Wengi wa wasichana hawa wadogo na watoto walio shambuliwa na wahalifu hawa wa kinyama walifunga safari ya usaliti kuelekea nchini Bangladesh kukimbia mauaji huku wakivuja damu na kulia kwa uchungu kutokana na shambulizi hili la kinyama. Mtaalamu mmoja wa kimatibabu katika masuala ya dhulma za kijinsia katika kambi ya wakimbizi wa Rohingya nchini Bangladesh alikiambia chombo cha habari cha Uingereza, gazeti la 'The Guardian', kwamba amemtibu mtoto chini ya miaka 10 akiwa na uvujaji mkubwa wa damu kutokana na kubakwa na majeshi ya Myanmar. Yote haya ikiwa ni pamoja na mashambulizi ya kinyama ambayo wanawake wa Rohingya wamekuwa wakiyapitia kutoka kwa majeshi haya ya kibudha, ikiwemo kuvuliwa nguo na kudhalilishwa, maziwa yao yakivyofolewa kwa visu, huku wakibakwa mbele ya watoto wao, waume zao na baba zao, wakibakwa kwa zamu na wanajeshi kadhaa mpaka kufikia hatua ya kufariki, na huku wakishindiliwa vijiti au silaha ndani ya sehemu zao za siri, yote ikiwa ni jaribio la kuwaogofya na kuitakasa Myanmar kutokana na jamii ya Waislamu ya Rohingya. Taarifa nyengine ni kuwa wanawake na wasichana wa Rohingya wamebakwa na kisha kufungiwa ndani ya nyumba na kuchomwa. La hawla wala quwata illah billah!       

Enyi watoto wa majeshi ya Kiislamu! Vipi munashuhudia dada zenu, mama zenu, binti zenu wakidhalilishwa, kukosewa heshima na kukatwa katwa katika hali ya kuogofya na makatili hawa wa kibudha na kisha musende kuwahami? Je, vilio vyao vya hofu, machozi yao ya aibu, hali yao ya kutapa tapa na kukata tamaa haiwatii hasira na kuwapa jinamizi akilini mwenu? Je munasubiri jamii ya kimataifa kuja kuwaokoa… jamii ya kimataifa hiyo hiyo iliyo wafungia macho na kuwapa mgongo dada zenu nchini Syria, Kashmir, Bosnia, Afrika ya Kati na kwengineko wakidhalilishwa na kuchinjwa na maadui wa Uislamu? Enyi mulio pewa jukumu na Allah (swt) la kuhami Waumini! Je, damu yenu haichemki kutokana na fikra ya kuhudumia chini ya tawala hizi khawafi katika biladi za Waislamu ambazo zimeukhini na kuutelekeza Ummah huu katika mikono ya madhalimu; watawala ambao hawaoni tofauti katika vilio vya dada zenu na ambao wamefeli hata kuwapa Waislamu hawa wanao tapatapa mahitaji na haki zao msingi, badala yake wame watelekeza katika kambi duni za kinyama ambazo hazistahili hata wanyama kukaa ndani yake? Je, hamuoni aibu kuhudumia tawala hizi ambazo zimewatumia kupigana katika vita kwa niaba ya dola za kigeni kuuwa kaka zenu na dada zenu Waislamu badala ya kulinda hadhi yao na damu yao kutokana na maadui wa dini yenu?

Enyi Majenerali na Wajeshi ya Kiislamu! Watoto wa Kiislamu wa Myanmar, Palestina, Syria, Afghanistan, Kashmir, Afrika ya Kati na biladi nyenginezo ulimwenguni wanawasubiri nyinyi kuwakomboa kutokana na hofu ya janga hili! Ni jibu gani mutakalompa Mola wenu (swt) siku ya Qiyama kwa kupuuza vilio vyao na kuwatelekeza kwa wabakaji na wauwaji wao… Siku ambayo hamutaweza kujificha kutokana na hisabu yenu?!! Tunawalingania kuvunja utiifu wenu kwa serikali hizi fedhehefu ambazo haziku waletea chochote isipo kuwa fedheha na kwa Ummah huu hofu, umwagikaji wa damu, na mateso. Na tunawalingania kuipatia Nusrah Hizb ut Tahrir kusimamisha Khilafah Rashidah ya pili itakayo watuma mara moja kuhami na kukomboa Ummah wenu ili mupate kurithi utukufu wa mashujaa wa Uislamu mfano wa Khalid bin Walid (ra), Salahuddin Ayubi, na Muhammad ibn Qasim, mupate hadhi katika maisha haya na malipo makubwa kesho Akhera!

Allah (swt) asema,  

وَمَا لَكُمْ لاَ تُقَاتِلُونَ فِي سَبِيلِ اللّهِ وَالْمُسْتَضْعَفِينَ مِنَ الرِّجَالِ وَالنِّسَاء وَالْوِلْدَانِ الَّذِينَ يَقُولُونَ رَبَّنَا أَخْرِجْنَا مِنْ هَـذِهِ الْقَرْيَةِ الظَّالِمِ أَهْلُهَا وَاجْعَل لَّنَا مِن لَّدُنكَ وَلِيًّا وَاجْعَل لَّنَا مِن لَّدُنكَ نَصِيرًا

"Na muna nini musipigane katika njia ya Allah na ya wale wanao onewa, miongoni mwa wanaume na wanawake na watoto, ambao husema: Mola wetu! Tutoe katika kijiji hiki ambacho watu wake ni madhalimu, na tujaalie tuwe na mlinzi anaye toka kwako, na tujaalie tuwe na wakutunusuru anaye toka kwako"  [An-Nisa: 75]

Dkt. Nazreen Nawaz
Mkurugenzi wa Kitengo cha Wanawake Katika Afisi Kuu ya Habari ya Hizb ut Tahrir

Hizb-ut Tahrir: Afisi ya Habari
Kitengo cha Wanawake
Address & Website
Al-Mazraa Sanduku la Posta. 14-5010 Beirut- Lebanon
Tel: 00961 1 30 75 94 Mobile: 00961 71 72 40 43
www.hizb-ut-tahrir.info
Fax: Telefax
E-Mail: ws-cmo@hizb-ut-tahrir.info

Andika maoni

Hakikisha umejaza (*) habari zinazohitajika palipoashiriwa. Kodi za HTML haziruhusiwi.

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu