Jumamosi, 09 Jumada al-thani 1447 | 2025/11/29
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

Kuanguka kwa Khilafah Kunaashiria Wito wa Kuhuishwa Kwake

Mnamo tarehe 3 Machi 1924, sawia na 28 Rajab 1342 H, kikundi kidogo cha wasaliti wa Kituruki, wakiongozwa na Mustafa Kemal, walivunja urithi wa zaidi ya karne 13 za umoja wa Waislamu. Kuanzia wakati huo na kuendelea, Waislamu walipoteza paa lao juu ya vichwa vyao na wakawa mayatima. Leo, miaka 104 ya hijria imepita tangu tukio hili la kusikitisha. Baada ya kuanguka kwa Khilafah, makafiri waligawanya ulimwengu wa Kiislamu katika maeneo madogo yaliyojitenga. Waliweka vikwazo vya usafiri kati ya maeneo haya, yakihitaji pasipoti na visa, na kuharibu majeshi yetu, silaha, rasilimali, ardhi, uwezo wa binadamu, na teknolojia-kila kitu.

Soma zaidi...

Trump Aitishia Gaza kwa Uvamizi wa Moja kwa Moja na Kuwafukuza Watu Wake

Jioni ya Jumanne, 4 Februari 2025, Rais wa Marekani Donald Trump alitangaza katika mkutano wake na Waziri Mkuu wa Kiyahudi kwamba "Wapalestina hawana chaguo zaidi ya kuondoka Ukanda wa Gaza. Nataka kuona Jordan na Misri zikipokea Wapalestina kutoka Gaza. Hakuna badali kwa wakaazi wa Gaza isipokuwa kuondoka." Aliongeza, "Jordan na Misri tayari zimekataa kuwapokea wakaazi kutoka Gaza, lakini baadhi ya watu wanakataa mambo isipokuwa hatimaye kukubaliana nayo."

Soma zaidi...

Enyi Majeshi ya Waislamu: Nani Atawakomesha Wapumbavu Hawa Wawili?!

Jana usiku, chaneli za satelaiti zilitangaza sherehe za mapokezi ya Rais wa Marekani Donald Trump kwa Waziri Mkuu wa umbile la Kiyahudi, pamoja na mkutano wa waandishi wa habari uliotangulia mazungumzo yao. Trump alionekana kama mcheshi akilenga kufurahisha watazamaji wanaomtazama, kwa kauli zake za kizembe kuhusu Ukanda wa Gaza, na nia yake ya kuwaondoa watu wake na kuweka udhibiti wa Amerika juu yake.

Soma zaidi...

Al-Burhan Anatafuta Kuiga Mfumo Ule Ule wa Kisekula Uliopita

Katika hotuba iliyotolewa leo na Jenerali Al-Burhan, Mwenyekiti wa Baraza la Utawala na Amiri Jeshi Mkuu, alisema: "Kipindi kijacho kitashuhudia kuundwa kwa serikali ili kukamilisha kazi za mpito. Inaweza kuitwa serikali ya muda. Baada ya kuidhinishwa kwa waraka wa katiba, serikali itaundwa, na waziri mkuu atachaguliwa kutekeleza majukumu yake katika kusimamia baraza la mawaziri la serikali bila kuingiliwa."

Soma zaidi...

Enyi Watu wa Sudan, Komesheni Mambo Matatu ya Marekani ambayo Yanahusisha Uhalifu Mkali: Vita, Kuitenga Darfur, na Uhalalishaji Mahusiano na Umbile la Kiyahudi

Kila mtu anashangaa juu ya siri iliyoko nyuma ya kuongezeka kwa kasi hii katika operesheni za kijeshi za jeshi hivi karibuni, kama vile vita vilivyokuwa hapo awali, na kwa zaidi ya mwaka mmoja, vimekuwa vikifanyika ndani ya duara lililofungwa, huku kukiwa na kusonga mbele na kurudi nyuma, bila ya kuwepo na uamuzi wa kijeshi kutoka upande wowote.

Soma zaidi...

Je, Ugaidi ni Quran na Vitabu, Enyi Mliofilisika

Tovuti ya Russia Today ilichapisha ripoti ya habari mnamo tarehe 5/2/2025 ikisema kwamba "Huduma ya Usalama ya Shirikisho la Urusi ilisambaratisha seli ya magaidi yenye mafungamano na Hizb ut Tahrir katika Rasi ya Crimea na kuwakamata watu watano waliokuwa wakisajili wafuasi wa Hizb, ambayo imepigwa marufuku nchini Urusi." Ripoti hiyo ilijumuisha video inayoonyesha operesheni ya ukamataji na uvamizi wa nyumba, ambapo ilionekana wazi kwamba kile ambacho idara ya usalama ya Urusi ilichukua kutoka kwa nyumba za Mashababu ni nakala za Al-Quran Al-Kareem, vitabu, na vijitabu vya kisiasa na kifikra vya Kiislamu - machapisho maarufu ya Hizb ut Tahrir kwa jina pamoja na maalumati yaliyomo.

Soma zaidi...
Jiunge kwa hii RSS feed

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu