Jumanne, 18 Dhu al-Qi'dah 1447 | 2026/05/05
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

Jibu la Swali: Matukio nchini Syria na Kuanguka kwa Utawala wa Assad

Asharq Al-Awsat ilichapishwa mnamo tarehe 8 Disemba 2024: (Utawala wa Assad umeanguka: Upinzani wa Syria umetangaza leo, Jumapili, kwamba umeikomboa Damascus na kuupindua utawala wa miaka 24 wa Rais Bashar al-Assad. Taarifa ya upinzani kwenye televisheni ya taifa ilisomeka: “Sifa zote ni za Mwenyezi Mungu, mji wa Damascus umekombolewa na dhalimu Bashar al-Assad amepinduliwa.” Upinzani uliongeza kuwa wafungwa wote wameachiliwa huru.)

Soma zaidi...

Watawala wa Bara Arabu Wanashindana katika Ufisadi na Utiifu kwa Maadui wa Ummah!

Siku chache zilizopita, watawala wa Imarati walijigamba juu ya uhamasishaji wao mkubwa wa kuwafikia wauaji wa Rabbi wa Kiyahudi, Zvi Kogan, kwenye ardhi zao, na kupongeza umakini wa vyombo vya usalama na kasi ya taratibu zao zilizochangia kufichua tukio hilo, baada ya huduma hizi zote kufanya kwa muda wote, kulingana na yale yaliyoelezwa katika taarifa ya Wizara ya Mambo ya Ndani. Wakati huo huo, Imarati na Wizara yake ya Ulinzi haikujitolea kuwanusuru zaidi ya mashahidi elfu 44 na elfu 104 waliojeruhiwa huko Gaza, ingawa muuaji wao anajulikana na haihitaji uchunguzi au umakini wa vyombo vya usalama kumfikia.

Soma zaidi...

Miaka Miwili ya Utawala bila Uislamu: Kupuuza Amana ya Mwenyezi Mungu

Katika hafla ya kuadhimisha mwaka wake wa pili afisini, Waziri Mkuu wa Malaysia, Datuk Seri Anwar Ibrahim, aliandaa Mpango wa Miaka Miwili wa Serikali ya Madani (2TM) na Kongamano la Kitaifa la 2024 la Marekebisho ya Utumishi wa Umma mnamo Novemba 23-24, 2024 katika Jumba la Mikutano la Kuala Lumpur (KLCC). Hafla hilo ilionyesha huduma mbalimbali za serikali chini ya paa moja, na zaidi ya vibanda 30 vinavyotoa huduma na bidhaa kwa umma. Ripoti zilisifu hafla hiyo kuwa ya mafanikio, ikiwa na zaidi ya wageni 200,000. Zaidi ya hayo, Anwar aliendesha kikao cha ukumbi wa jiji kuangazia mafanikio na mipango yake chini ya serikali ya Madani huku akishughulikia ukosoaji, haswa kuhusu mahojiano yake ya CNN yenye utata kuhusu uwepo wa umbile la Kiyahudi na ufadhili wa makampuni ya kibinafsi wa safari zake na ujumbe wake nje ya nchi.

Soma zaidi...

Hizb ut Tahrir / Wilayah Uturuki: Makala ya Filamu “Mustakabali wenye Bishara Njema kutoka Karne Iliyopotea!"

Kwa mnasaba wa miaka 103 H ya mkoloni kafiri, kwa msaada wa wasaliti wa Kiarabu na Kituruki, kuivunja dola ya Uislamu (Khilafah Uthmani) na kukomeshwa kwa mfumo wa utawala katika Uislamu (Khilafah) kutoka katika maisha ya Umma wa Kiislamu, Afisi ya Habari ya Hizb ut Tahrir katika Wilaya ya Uturuki ilitoa filamu ya makala yenye kichwa: “Mustakabali wenye Matumaini kutoka Karne Iliyopotea!”

Soma zaidi...

Maamuzi ya Mkutano wa GCC ni Ushirikiano katika Dhambi na Udanganyifu

Mnamo Jumapili, tarehe 1 Disemba 2024, katika taarifa ya mwisho iliyotolewa na kikao cha 45 cha Baraza Kuu la Baraza la Ushirikiano wa Ghuba iliyoandaliwa na Serikali ya Kuwait, viongozi wa nchi za Baraza la Ushirikiano wa Ghuba (GCC) na wawakilishi wao walitoa wito wa kumalizwa kwa uhalifu wa mauaji na adhabu ya pamoja huko Gaza, uhamishaji wa wakaazi, uharibifu wa vifaa na miundombinu ya raia. Walitoa wito wa kuingilia kati kulinda raia, kusitisha vita, na kufadhili mazungumzo mazito ili kufikia suluhu endelevu, wakisisitiza misimamo yao madhubuti kuhusu kadhia ya Palestina, kukomesha uvamizi huo, na uungaji mkono wao kwa uhuru wa watu wa Palestina juu ya ardhi zote za Palestina zinazokaliwa kwa mabavu tangu Juni 1967, na kuanzishwa kwa dola huru ya Palestina na Jerusalem Mashariki kama mji mkuu wake, na kuhakikisha haki za wakimbizi, kwa mujibu wa Mpango wa Amani wa Kiarabu na maazimio ya uhalali wa kimataifa. Kuhusiana na Lebanon, viongozi hao walithibitisha mshikamano kamili na Lebanon.

Soma zaidi...
Jiunge kwa hii RSS feed

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu