Jumatano, 19 Dhu al-Qi'dah 1447 | 2026/05/06
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

Sura Mpya ya Walaji Njama katika Astana 22 Imetanguliwa na Mkutano huko Tarnaba na Majadiliano kuhusu Kufungua Barabara na Vivuko vya Kimataifa

Enyi Wana Mapinduzi: Tusikilizeni, sisi ndugu zenu katika Hizb ut Tahrir Al-Nadheer Al-Aryan (mwonyaji wa wazi), ndugu zenu ambao mumeyaona maneno yao kuwa ya kweli na ambao kuona kwao ni kukubwa. Sisi hatuhitaji fadhila katika jambo hili juu yenu, kwani huu ni wajibu wetu na tutakutana nao kwa Mwenyezi Mungu Siku ya Kiyama. Tunakuombeni nyinyi, watu wetu, mufanyeni haraka kuregesha uamuzi wenu kutoka kwa waliouiba, kwani nchi na zana zao ni mikono yenye nia mbaya inayotaka kukuangamizeni.

Soma zaidi...

Uundaji wa Wanamgambo na Vikundi vyenye Silaha: Hatari Kubwa na Chombo cha Amerika cha Kugawanya Sudan

Mnamo Jumamosi, Novemba 16, 2024, kundi lenye silaha linalojiita Harakati ya Ukombozi ya Al-Jazirah lilitangaza nia yake ya “kulikomboa Jimbo la Al-Jazirah.” Pia lilionyesha uungaji mkono wake kwa vikosi vya jeshi. Katika video iliyosambazwa na vyombo vya habari na baadhi ya wanahabari wanaounga mkono jeshi, kundi hilo liliwataka watu wa Al-Jazirah kukusanyika karibu nalo na kukumbatia malengo yake.

Soma zaidi...

Amani ya Kudumu Inaweza Tu Kupatikana huko Balochistan kupitia Kuung'oa Mfumo wa Wakoloni na Kusimamisha Khilafah Rashida

Machafuko katika jimbo la Balochistan si jambo geni. Yamedumu tangu uhuru wa Pakistan kutoka kwa Raj wa Uingereza. Watu wa Balochistan wana malalamiko ya kina, yaliyoachwa bila kutatuliwa na utawala wa kikoloni wa Uingereza na watawala ambao ni vibaraka wa wakoloni wa Magharibi. Mfumo wa wakoloni ulipangwa kuwatiisha Waislamu, badala ya kuangalia mambo yao. Unawanyima haki na unadumisha udhibiti kupitia nguvu za kijeshi.

Soma zaidi...

Msimamo Unaokinzana wa Indonesia juu ya umbile la Kiyahudi: Maneno Makali Lakini Ingali Inadumisha Mahusiano Mazuri

Indonesia imeyataka mataifa ya Kiislamu na Kiarabu kukata uhusiano wa kibiashara na kiuchumi na ‘Israel’ ili kukomesha ghasia mjini Gaza. Katika kikao cha Riyadh cha Jumuiya ya Nchi za Kiarabu na OIC, Makamu wa Waziri wa Mambo ya Nje Anis Matta alisisitiza ulazima wa kukata vitega uchumi vinavyohusiana na taasisi za Kizayuni na kuimarisha biashara ndani ya uchumi wa nchi za Kiislamu. Licha ya wito huu, biashara ya Indonesia na ‘Israel’ ilifikia dolari milioni 173 kuanzia Januari hadi Septemba 2024, ongezeko la 24.6% kutoka mwaka uliopita.

Soma zaidi...

Mtazamo kwa Ghasia za Baada ya Uchaguzi wa Msumbiji

Kwa mujibu wa Kituo cha Demokrasia na Haki za Binadamu cha Msumbiji na shirika la Reuters, kufikia tarehe 8/11/2024, jumla ya vifo 34 viliripotiwa huku vyanzo vyengine vikisema kuwa waliouawa ni zaidi ya 50, kutokana na ghasia za baada ya uchaguzi. kutangazwa kwa mgombea wa chama tawala cha Front for Liberation of Msumbiji (Frelimo), Daniel Chapo kuwa mshindi wa uchaguzi wa rais uliofanyika mnamo Oktoba 24 mwaka huu ambapo wapinzani walidai kuwa matokeo ya kura yaliibwa.

Soma zaidi...

Vitendo vya Baraza la Uongozi wa Rais na Serikali yake ni Mithili ya Sarabi Jangwani, na Kuporomoka kwa Sarafu ni Shahidi wa hilo

Sarafu ya nchi katika maeneo yanayodhibitiwa na Baraza la Uongozi wa Rais imeshuhudia mporomoko wa kihistoria dhidi ya sarafu za kigeni kwa wiki kadhaa, huku riyal ya Saudia ikivuka kizuizi cha riyal 535, na dolari ya Marekani ilivuka kizuizi cha riyal 2,000. Wakati huo huo, baadhi ya miji ilishuhudia uasi mdogo wa kiraia na kufungwa kwa maduka ya kupinga kuporomoka kwa sarafu hiyo, na maduka kadhaa ya kubadilisha fedha yalifunga milango yake kwa watu baada ya janga hili la kuporomoka na kutoweza kwa serikali kutafuta suluhisho mwafaka kwa hilo.

Soma zaidi...

Ala za Kindani kama Kikaragosi cha Makafiri wa Magharibi katika Kutekeleza Sera Zake, na Hakuna Suluhisho kwa Watu wa Yemen isipokuwa kwa Kutekeleza Shariah ya Mwenyezi Mungu

Watu wetu wa Hadhramaut na Yemen yote lazima watambue kwamba uongozi wa kisiasa nchini Yemen, kaskazini na kusini, haujali matatizo na mahitaji yao. Kinyume chake, unazidisha tu mateso yao, iwe kupitia kuzorota kwa uchumi au kukosekana kwa huduma muhimu kama vile umeme, maji, na mahitaji mengine kwa maisha yenye staha. Ni lazima tuondoe uaminifu wetu kutoka kwa wao wote, kwani pindi wanapotenda, huitumikia Magharibi kafiri, na wanaponyamaza, wanapora mali ya nchi na watu wake bila ya uwajibikaji au uangalizi!

Soma zaidi...

Ushirikiano wa Mamlaka za Uholanzi pamoja na Watu Ovyo wa Mayahudi Umesalia Kuvama ndani ya Kumbukumbu ya Umma

Vyombo vya habari vya kimataifa vimeripoti vitendo vya kundi la wachochezi wa Kiyahudi wakati na baada ya mechi ya kandanda, kujihusisha na uchokozi dhidi ya Waislamu kuhusiana na kadhia kuu ya Umma wa Kiislamu, kadhia ya Palestina. Vitendo hivi viliibua hisia za kimaumbile kutoka kwa Waislamu wa mataifa mbalimbali na kutoka kwa raia waheshimiwa wa Uholanzi wenyewe.

Soma zaidi...
Jiunge kwa hii RSS feed

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu