Ujumbe kwa Watu Wetu mjini Gaza
- Imepeperushwa katika Jarida la Al-Waie
- Kuwa wa kwanza kutoa maoni!
- |
Enyi watu wa Gaza: nyinyi leo mmesimama katika msimamo wa Mitume (as) na watu wema, mkisimama kidete kwa ajili ya haki dhidi ya dhulma. Kila dhiki, kila jeraha, kila Shahidi ni riziki katika mizani yenu ya mema, na kunyanyua daraja yenu. Ukuruba wa Mwenyezi Mungu uko pamoja nanyi, na ushindi wake uko karibu, basi subirini na muwe thabiti, na furahieni kwa yale aliyoyaahidi Mwenyezi Mungu (swt) ya bustani na daraja, na heshima ya dunia ambayo hupatikana kwa uthabiti na kujitolea mhanga.