Mfumo wa Kibepari wa Kiulimwengu Unaoongozwa na Marekani, pamoja na Maamuzi na Taasisi zake za Kimataifa, Daima Zitaiweka Pakistan Utumwani
- Imepeperushwa katika Habari na Maoni
- Kuwa wa kwanza kutoa maoni!
- |
Akisikiliza maregeleo ya rais kuhusu mradi wa mgodi wa shaba na dhahabu wa Reko Diq mnamo tarehe 2 Novemba 2022, Jaji Munib Akhtar, aliitaja faini ya Kituo cha Kimataifa cha Usuluhishi wa Mizozo ya Uwekezaji (ICSID) ya dolari bilioni 6.5 dhidi ya Pakistan kama "bomu la nyuklia," kwani linaweza kuchukuliwa popote duniani kwa ajili ya utekelezwaji.



