Alhamisi, 29 Shawwal 1447 | 2026/04/16
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu
kesho kutwa

kesho kutwa

Moyo wa Hebron na Msikiti wa Ibrahimi Wafanywa Kuwa wa Kiyahudi kwa Kufuata Hatua Zile Zile kama Ulivyofanywa kuwa wa Kiyahudi Msikiti wa Al-Aqsa

Baada ya umbile la Kiyahudi kuamua kuhamisha mamlaka ya kiidara ya Msikiti wa Ibrahimi kutoka Manispaa ya Hebron hadi “Baraza la Kidini la Kiyahudi huko Kiryat Arba,” na baada ya umbile hilo kukataa pingamizi iliyowasilishwa na Manispaa ya Hebron kuhusu uamuzi huu, pamoja na uamuzi uliofuata wa kugeuza ua wa ndani wa Msikiti wa Ibrahimi kuwa uwanja wa umma, na pamoja na vyama vya Kiyahudi vinavyofanya kazi ya kununua nyumba katika mji wa Hebron (al-Khalil) - moyo wa Mji wa Hebron, huku Msikiti wa Ibrahimi ukiwa kiini chake, unafanywa kuwa wa Kiyahudi waziwazi mbele ya ulimwengu na mbele ya Umma wa Kiislamu, kama vile eneo la Safari ya Usiku ya Mtume wake (saw) na viunga vyake linavyofanywa kuwa la Kiyahudi.

Mashirika ya Mamlaka ya Palestina na Majambazi Wao Yamkamata Mwanafunzi Saif Abu Al-Hawa

Mamlaka ya Palestina (PA), ambayo ni tiifu kwa Mayahudi, ilimkamata mwanafunzi Saif Abu al-Hawa alipokuwa akiondoka Chuo Kikuu cha Bethlehem mnamo Jumanne, 9 Disemba 2025. Kwa kutumia majambazi wasaliti na kisha kikosi kutoka kwa vyombo vya usalama vya PA, katika tukio linaloakisi mbinu za ujambazi na vitisho vya PA dhidi ya watu wa Palestina, hawazuiwi na Dini wala sheria, wala hata utakatifu wa chuo kikuu ambacho Saif alitoka. Kisha alifikishwa mbele ya mahakama mnamo Alhamisi, ambapo jaji aliongeza kifungo chake kwa siku kumi na tano, licha ya kwamba hakufanya uhalifu wowote. Kosa lake pekee lilikuwa kutaja Hukm Shari’ kwamba Waislamu hawaruhusiwi kushiriki katika sherehe za sikukuu za Kikristo!

Bajeti za Jordan Ni Nakala Zinazorudiwa katika Ufisadi Wao na Kuzishughulikia Kupitia Madeni Kuna Wiana na Dori ya Kiutendaji ya Serikali na Haijali Uchungaji wa Mambo ya Watu

Serikali ilikadiria, katika Rasimu ya Sheria ya Bajeti Kuu ya mwaka 2026, mapato ya umma yangekuwa takriban dinari bilioni 10.931, 75% kati yake yakiwa ni kutokana na kodi, na dinari milioni 735 kutoka kwa ruzuku za kigeni. Waziri wa Fedha alisema kwamba kiasi cha matumizi ya sasa ni dinari milioni 11,456, huku matumizi makuu yakifikia dinari milioni 1,600 pekee. Kuhusu nakisi inayotarajiwa kwa mwaka 2026, inakadiriwa kufikia takriban 4.6% ya Pato la Taifa.

Jiunge kwa hii RSS feed

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu