Gazeti la Al-Raya: Vichwa Vikuu vya Toleo 577
- Imepeperushwa katika Al-Rayah
- Kuwa wa kwanza kutoa maoni!
Vichwa Vikuu vya Toleo 577
Vichwa Vikuu vya Toleo 577
Shambulizi la silaha jijini Washington, D.C. wiki moja iliyopita—ambapo Rahmanullah Lakanwal, raia wa Afghanistan, anatuhumiwa kuwafyatulia risasi Walinzi wawili wa Kitaifa wa Marekani—lilitokea karibu na kituo cha Metro cha Farragut Magharibi, mita mia chache tu kutoka Ikulu ya White House, eneo ambalo kwa kawaida linalindwa na baadhi ya tabaka kali zaidi za usalama. Kutokana na ufyatuaji risasi huo, Sarah Bäckström, mlinzi wa Kitaifa wa miaka 20, aliuawa na Andrew Wolf alijeruhiwa vibaya.
Rais wa Marekani Donald Trump alituma barua iliyoandikwa kwa mkono kwa kiongozi wa Syria Ahmed Sharaa, akisisitiza uungaji mkono wake na kuahidi msaada wa Marekani. Barua hiyo iliwasilishwa Damascus kupitia Tom Barrack, mmoja wa washirika wa karibu wa Trump na mfanyibiashara wa kimataifa. Picha ya wakati Trump alipokutana na Sharaa katika Afisi ya Oval iliambatanishwa na barua hiyo. Trump aliandika barua ifuatayo kwenye picha hiyo kwa mwandiko wake mwenyewe: “Ahmed, utakuwa kiongozi mzuri, na Amerika itasaidia!” (Mashirika, 3 Disemba 2025)
Hizb ut Tahrir / Wilayah Lebanon inamuomboleza: Mwanachuoni mtukufu, khatib, sheikh, mwandishi, na mshairi, Marwan al-Khatib (Abu Muhammad)