Jumapili, 25 Shawwal 1447 | 2026/04/12
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu
kesho kutwa

kesho kutwa

Mradi wa Reli wa China–Indonesia: Mkakati wa China Kuidhibiti Indonesia

Indonesia inafikiria kujadili upya deni la mradi wa reli ya mwendo kasi wa Jakarta–Bandung, unaojulikana kama Whoosh, kutokana na mzigo mzito wa kifedha unaouweka kwa mwendeshaji wa reli ya serikali Kereta Api Indonesia (KAI). Waziri wa Biashara Zinazomilikiwa na Serikali Erick Thohir alisema mpango huo utaruhusu KAI kusimamia treni huku serikali ikisimamia miundombinu. Mradi huo wenye thamani ya dolari bilioni 7.3 ulifadhiliwa hasa kupitia mikopo kutoka Benki ya Maendeleo ya China, awali kwa riba ya asilimia 2. Hata hivyo, kukatizwa na maambukizi na masuala ya ardhi yalisukuma gharama zaidi, na kuhitaji ufadhili wa ziada kwa riba ya asilimia 3.4.

Hakuna Wokovu kwa Watu wetu nchini Sudan Wala Amani au Usalama isipokuwa chini ya Mfumo wa Uislamu

Katika yote historia, wingi wa makabila nchini Sudan kamwe haukuwa sababu ya mizozo na vita. Bali, kilichosababisha haya ni mapambano makali ya kisiasa na kijeshi baina ya dola za kikoloni na vibaraka wao, ambayo yaliharibu mazao na vizazi, hasa baada ya wao kuigawanya nchi na kupanda mbegu za fitina na mapigano ya kikabila na kimapendeleo, sawa kabisa na yale yanayotokea leo na kwa usahihi kabisa kama ilivyotokea katika siku za mwanzo za Ujahiliya.

Enyi Waislamu: Waokoeni watu wa Gaza Kabla Hawajaangamizwa Kabisa na Jihadharini Isije Akakushukieni Ghadhabu na Adhabu ya Mwenyezi Mungu

Umbile la Kiyahudi linaendelea na vita vyake vya mauaji ya halaiki katika Ukanda wa Gaza, likilenga maeneo mbalimbali ya Ukanda huo kwa mashambulizi ya anga na mizinga mikubwa, na kusababisha makumi ya vifo na majeruhi kila siku. Kwa wiki kadhaa, limezidisha mashambulizi yake katika mji wa Gaza, eneo lenye wakaazi wengi na watu waliokimbia makaazi yao kutoka sehemu ya kaskazini ya Ukanda huo, kwa ajili ya maandalizi ya kukaliwa tena kimabavu. Linalenga shule na makaazi, linatekeleza operesheni kubwa za ubomoaji inayolenga nyumba zote za makaazi, na kuvunja magorofa ya makaazi, likiambatanisha na maonyo kuhamia sehemu ya kusini ya Ukanda huo.

Hizb ut Tahrir / Wilayah Sudan Yafanya Kisimamo katika eneo la Nile Mashariki

Leo, Jumatano, tarehe 25 Rabi’ al-Awwal 1447 H sawia na 17 Septemba 2025 M, Mashababu wa Hizb ut Tahrir / Wilayah Sudan katika eneo la Nile Mashariki walifanya kisimamo baada ya Swala ya Adhuhuri katika Msikiti Mkuu wa Souq Sitta Al-Wahda. Ndani yake, mabango yaliinuliwa kuwataka Waislamu kusimama kidete kuzuia njama ya kuichana Sudan kwa kuitenganisha Darfur.

Jiunge kwa hii RSS feed

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu