Pongezi kwa Idd ul-Adha Iliyobarikiwa 1447 H
- Imepeperushwa katika Afisi Kuu ya Habari
- Kuwa wa kwanza kutoa maoni!
- |
Kutoka kwa Mtume (saw) ambaye amesema: «إِنَّ أَعْظَمَ الْأَيَّامِ عِنْدَ اللهِ يَوْمُ النَّحْرِ» “Hakika siku tukufu zaidi mbele ya Mwenyezi Mungu ni siku ya Arafah”, basi kwa mnasaba huu uliobarikiwa na kwa kutukuza alama za Mwenyezi Mungu Azza wa Jalla: ذَلِكَ وَمَن يُعَظِّمْ شَعَائِرَ اللَّهِ فَإِنَّهَا مِن تَقْوَى﴾ الْقُلُوبِ﴿ “Ndio hivyo! Na anayetukuza ibada za Mwenyezi Mungu, basi hayo ni katika unyenyekevu wa nyoyo.” [Al-Hajj: 32], na Licha ya majanga ambayo Umma wa Kiislamu unapitia chini ya watawala waliouangusha na kuusalimisha kwa adui yake, ambayo yamejaza nyoyo zetu maumivu na huzuni, bado tunapaswa kutoa pongezi na baraka zetu za dhati kwa Umma wetu wa Kiislamu, wenye subira, na wenye kutaraji mema katika Idd al-Adha iliyobarikiwa, tukimwomba Mwenyezi Mungu azifanye siku hizi za Idd kuwa za baraka, ushindi, na kuinuliwa.



