Gazeti la Al-Raya: Vichwa Vikuu vya Toleo 586
- Imepeperushwa katika Al-Rayah
- Kuwa wa kwanza kutoa maoni!
- |
Waziri Mkuu wa India Narendra Modi amepangwa kufanya ziara ya kikazi nchini Malaysia mnamo Februari 7-8, 2026, na inaripotiwa kwamba anatarajiwa kupokea mapokezi makubwa kutoka kwa serikali na jamii ya Mabaniani nchini Malaysia. Kibaraka huyu wa Amerika mara nyingi hupokea mapokezi ya heshima katika nchi nyingi kote duniani na hupewa tuzo nyingi na nchi anazotembelea, wakiwemo watawala Ruwaibidha wa Waislamu, kiasi kwamba baadhi wako tayari kukita masanamu ili tu kumfurahisha kiongozi huyu mshirikina.
Hizb ut Tahrir / Wilayah Pakistan: Gaza inawahesabu Mashahidi wake, ambao Wametolewa Kafara kwa ajili ya Trump na Netanyahu!
Matukio yanatokea kwa kasi kubwa kaskazini mashariki mwa Syria, na Vikosi vya Kidemokrasia vya Syria (SDF) vinapoteza udhibiti wa maeneo hayo kwa kasi kubwa, huku serikali ya Syria ikiyachukua. Yote haya yalitokeaje? Hili linapaswa kuelewekaje ikizingatiwa kwamba serikali na SDF ni vibaraka wa Amerika? Na licha ya idhini ya Marekani kwa serikali ya Syria kuwa wazi kama mwanga wa mchana katika kuteka maeneo hayo, utawala wa Trump unapanga nini nchini Syria au viunga vyake?
Hizb ut Tahrir Amerika ilifanikiwa kufanya kongamano lake la kila mwaka kwa mwaka huu 1447 H (2026 M), kama sehemu ya kampeni ya kimataifa iliyoandaliwa na Hizb ut Tahrir kwa mnasaba wa kumbukumbu ya kuvunjwa kwa Khilafah mnamo tarehe 28 Rajab, 1342 H. Kongamano hilo lilitumika kama wito kwa Waislamu kote duniani kutambua na kutimiza wajibu wao wa kuregesha mfumo kamili wa maisha wa Kiislamu kwa kusimamisha Khilafah kwa njia ya Mtume wetu Muhammad (saw).
Hizb ut Tahrir / Wilayah Lebanon yaandaa kongamano lake la kila mwaka kwa kichwa: “Kuhalalisha Mahusiano na Kujisalimisha au Ahadi ya Mwenyezi Mungu na Dola ya Kiislamu?!” Kwa mnasaba wa kumbukumbu uchungu ya miaka 105 ya kuvunjwa kwa dola ya Khilafah mnamo 28 Rajab 1342 H sawia na 3 Machi 1924 M
Hizb ut Tahrir / Wilayah Iraq: Rajab kati ya Jana na Leo!