Gazeti la Al-Raya: Vichwa Vikuu vya Toleo 593
- Imepeperushwa katika Al-Rayah
- Kuwa wa kwanza kutoa maoni!
- |
Kwa kuamini qadhaa ya Mwenyezi Mungu Mtukufu, Hizb ut Tahrir / Wilayah Syria inamuomboleza kwa Waislamu jumla, na kwa wabebaji dawah haswa, Ndugu Omar Abdul Rahim Khatib (Abu Abdo Khatib), mmoja wa wanachama wake, kutoka kijiji cha Arhab katika vijiji vya magharibi mwa Aleppo, na ambaye alifariki akiwa na umri wa miaka 50, ambayo aliitumia kwa utiifu kwa Mwenyezi Mungu Mtukufu.
Katika siku ya tatu ya Idd al-Fitr Iliyobarikiwa, sawia na Jumamosi, 12 Machi 2026 M, mashababu wa Hizb ut Tahrir/Wilayah Sudan walikusanyika katika afisi ya hizb katikati mwa jiji la Khartoum ili kupeana salamu za Idd. Mkutano huo ulijumuisha mashababu kutoka kote Khartoum, Omdurman, Jabal Awliya, Kalakila, Nile Mashariki, na maeneo mengine. Walitoa pongezi zao kwa Idd iliyobarikiwa na kuelezea furaha yao ya kuonana baada ya miaka mingi ya vita.
Hizb ut Tahrir / Wilayah ya Uturuki, kupitia matembezi mikubwa na taarifa kwa vyombo vya habari zilizoandaliwa kote Uturuki chini ya kauli mbiu “Iokoeni Al-Aqsa! Simameni dhidi ya Amerika!”, ililaani ukandamizaji wa umbile nyakuzi la Kizayuni, kiburi cha mkoloni Amerika, na kimya cha watawala wa nchi za Kiislamu kuhusu udhalilishaji huu.
Hizb ut Tahrir / Wilayah Uturuki iliwasilisha taarifa kwa vyombo vya habari yenye hoja kumi kwa Umma wa Kiislamu wakati wa mkutano na waandishi wa habari, yenye kichwa cha habari: “Vita dhidi ya Iran: Ukafiri ni Mila Moja, Na Waislamu ni Umma Mmoja”
Pongezi za Kitengo cha Wanawake kwa Mnasaba wa Ujio wa Idd ul-Fitr Iliyobarikiwa 1447 H
Al-Waqiyah TV: Pongezi za Kundi la Wabebaji Da’wah kwa Mnasaba wa Idd ul-Fitr Iliyobarikiwa 1447 H