Jumapili, 12 Dhu al-Hijjah 1446 | 2025/06/08
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

Hizb ut Tahrir / Wilayah Uturuki: Makala ya Filamu “Mustakabali wenye Bishara Njema kutoka Karne Iliyopotea!"

Kwa mnasaba wa miaka 103 H ya mkoloni kafiri, kwa msaada wa wasaliti wa Kiarabu na Kituruki, kuivunja dola ya Uislamu (Khilafah Uthmani) na kukomeshwa kwa mfumo wa utawala katika Uislamu (Khilafah) kutoka katika maisha ya Umma wa Kiislamu, Afisi ya Habari ya Hizb ut Tahrir katika Wilaya ya Uturuki ilitoa filamu ya makala yenye kichwa: “Mustakabali wenye Matumaini kutoka Karne Iliyopotea!”

Soma zaidi...

Maamuzi ya Mkutano wa GCC ni Ushirikiano katika Dhambi na Udanganyifu

Mnamo Jumapili, tarehe 1 Disemba 2024, katika taarifa ya mwisho iliyotolewa na kikao cha 45 cha Baraza Kuu la Baraza la Ushirikiano wa Ghuba iliyoandaliwa na Serikali ya Kuwait, viongozi wa nchi za Baraza la Ushirikiano wa Ghuba (GCC) na wawakilishi wao walitoa wito wa kumalizwa kwa uhalifu wa mauaji na adhabu ya pamoja huko Gaza, uhamishaji wa wakaazi, uharibifu wa vifaa na miundombinu ya raia. Walitoa wito wa kuingilia kati kulinda raia, kusitisha vita, na kufadhili mazungumzo mazito ili kufikia suluhu endelevu, wakisisitiza misimamo yao madhubuti kuhusu kadhia ya Palestina, kukomesha uvamizi huo, na uungaji mkono wao kwa uhuru wa watu wa Palestina juu ya ardhi zote za Palestina zinazokaliwa kwa mabavu tangu Juni 1967, na kuanzishwa kwa dola huru ya Palestina na Jerusalem Mashariki kama mji mkuu wake, na kuhakikisha haki za wakimbizi, kwa mujibu wa Mpango wa Amani wa Kiarabu na maazimio ya uhalali wa kimataifa. Kuhusiana na Lebanon, viongozi hao walithibitisha mshikamano kamili na Lebanon.

Soma zaidi...

Tanzia ya Mbebaji Ulinganizi Hajj Mustafa Abdullah Al-Issa Al-Jaber Al-Aboushi (Abu Anas)

Kwa imani katika qadhaa ya Mwenyezi Mungu (swt) na kutaka malipo Yake, Afisi ya Habari ya Hizb ut Tahrir / Wilayah Jordan inamuomboleza Mbebaji Da’wah katika safu zake: Hajj Mustafa Abdullah Al-Issa Al-Jaber Al-Aboushi (Abu Anas) Aliyefariki kwenda kwenye rehema za Mwenyezi Mungu Mtukufu asubuhi ya leo, Jumanne, 3/12/2024, akiwa na umri wa miaka 80.

Soma zaidi...

Marekani, kupitia Usitishaji vita, Inafikia Malengo Mawili Muhimu kwa Uvamizi wa Kiyahudi: Kuondolewa kwa Vikosi vya Hezbollah vinavyoungwa mkono na Iran Kaskazini mwa Mto Litani, na Kutenganishwa kwa Pande Mbili!

Mnamo tarehe 27 Novemba 2024, usitishaji vita ulitangazwa katika upande wa Lebanon kati ya umbile la Kiyahudi na Hezbollah. Moja ya masharti yake ilikuwa kwamba umbile la Kiyahudi lingeondoa jeshi lake linalovamia kutoka kusini mwa Lebanon ndani ya miezi miwili, huku Hezbollah ingerudisha nyuma majeshi yake kaskazini mwa Mto Litani. Makubaliano hayo pia yalivipa vikosi vya Kiyahudi uhuru wa kutembea kusini endapo chama hicho kitakiuka makubaliano hayo, sambamba na kuendelea na safari za ndege za adui katika anga ya Lebanon kwa ajili ya uchunguzi na ujasusi.

Soma zaidi...
Jiunge kwa hii RSS feed

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu