Jumatatu, 13 Dhu al-Hijjah 1446 | 2025/06/09
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

Baada ya Mwaka Mmoja wa Mauaji ya Halaiki (na Miaka 76 ya Ukaliaji Kimabavu), Watawala wa Ruwaibidha Wakusanyika Tena Kuendeleza Kejeli na Usaliti wao

Ni mwaka mmoja kamili baada ya watawala wa Waarabu na Waislamu kukusanyika kujadili kadhia ya Palestina kufuatia mkasa wa Oktoba 7, wanakutana tena mahali pale pale, pamoja na mtu yule yule, wakishughulikia tatizo lile lile, na hatimaye kutoa maazimio yale yale! Zaidi ya viongozi 50 wa dola za Waislamu walihudhuria Mkutano wa Waarabu na Waislamu mnamo tarehe 11/11/2024, akiwemo Waziri Mkuu wa Malaysia. Kwa kutabiriwa, mapendekezo yaliyochakaa yaliwasilishwa, na Mkutano huo ulihitimishwa kwa maazimio yaliyochakaa vilevile. Kikubwa kinachotolewa na watawala hao ni kulaani mauaji ya halaiki ya Gaza na ‘Israel’ na kuomba Umoja wa Mataifa (UN) - shirika lile lile lililohusika na kuzaliwa kwa umbile halifu la Kiyahudi.

Soma zaidi...

Hizb ut Tahrir / Wilayah Tunisia: Matembezi ya Ukombozi “Gaza Inamwachia Mwenyezi Mungu Kiwango cha Usaliti jijini Riyadh na inataka Msaada kwa Umma na Majeshi yake!”

Matembezi ya hamsini na nane ya kunusuru Palestina na mateka Al-Aqsa, ambayo yaliandaliwa na Hizb ut Tahrir / Wilayah ya Tunisia, yalifanyika katika mji mkuu, Tunis, baada ya swala ya Ijumaa, chini ya kichwa “Gaza Inamwachia Mwenyezi Mungu Kiwango cha Usaliti jijini Riyadh na inataka Msaada kwa Umma na Majeshi yake!”

Soma zaidi...

Watawala wa Iran ni Uhalisia tu wa Sauti na Maonyesho ya Fataki Hawana Uhusiano Wowote na Ushindi au Ukombozi

Kamanda wa Walinzi wa Mapinduzi ya Iran, Meja Jenerali Hossein Salami, alithibitisha katika ufunguzi wa mazoezi ya mapambano ya usalama ya “Nasrallah” kwamba “umbile la Kizayuni linakosea ikiwa linadhani kuwa Hizbullah itatoka nje ya uwanja kwa kuwauwa viongozi wake,” na kubainisha kuwa “chama hicho ni vuguvugu kubwa ambalo haliwezi kuzimwa wala kumalizwa.” Akalitisha umbile la Kiyahudi kwa kusema: “Leo tuna nyinyi machoni mwetu, na tutapigana mpaka mwisho, na hatutakuruhusuni kudhibiti hatma ya Waislamu, na tutalipiza kisasi, nanyi mtapata pigo chungu, na lazima musubiri.”

Soma zaidi...

Sura Mpya ya Walaji Njama katika Astana 22 Imetanguliwa na Mkutano huko Tarnaba na Majadiliano kuhusu Kufungua Barabara na Vivuko vya Kimataifa

Enyi Wana Mapinduzi: Tusikilizeni, sisi ndugu zenu katika Hizb ut Tahrir Al-Nadheer Al-Aryan (mwonyaji wa wazi), ndugu zenu ambao mumeyaona maneno yao kuwa ya kweli na ambao kuona kwao ni kukubwa. Sisi hatuhitaji fadhila katika jambo hili juu yenu, kwani huu ni wajibu wetu na tutakutana nao kwa Mwenyezi Mungu Siku ya Kiyama. Tunakuombeni nyinyi, watu wetu, mufanyeni haraka kuregesha uamuzi wenu kutoka kwa waliouiba, kwani nchi na zana zao ni mikono yenye nia mbaya inayotaka kukuangamizeni.

Soma zaidi...

Uundaji wa Wanamgambo na Vikundi vyenye Silaha: Hatari Kubwa na Chombo cha Amerika cha Kugawanya Sudan

Mnamo Jumamosi, Novemba 16, 2024, kundi lenye silaha linalojiita Harakati ya Ukombozi ya Al-Jazirah lilitangaza nia yake ya “kulikomboa Jimbo la Al-Jazirah.” Pia lilionyesha uungaji mkono wake kwa vikosi vya jeshi. Katika video iliyosambazwa na vyombo vya habari na baadhi ya wanahabari wanaounga mkono jeshi, kundi hilo liliwataka watu wa Al-Jazirah kukusanyika karibu nalo na kukumbatia malengo yake.

Soma zaidi...

Amani ya Kudumu Inaweza Tu Kupatikana huko Balochistan kupitia Kuung'oa Mfumo wa Wakoloni na Kusimamisha Khilafah Rashida

Machafuko katika jimbo la Balochistan si jambo geni. Yamedumu tangu uhuru wa Pakistan kutoka kwa Raj wa Uingereza. Watu wa Balochistan wana malalamiko ya kina, yaliyoachwa bila kutatuliwa na utawala wa kikoloni wa Uingereza na watawala ambao ni vibaraka wa wakoloni wa Magharibi. Mfumo wa wakoloni ulipangwa kuwatiisha Waislamu, badala ya kuangalia mambo yao. Unawanyima haki na unadumisha udhibiti kupitia nguvu za kijeshi.

Soma zaidi...

Msimamo Unaokinzana wa Indonesia juu ya umbile la Kiyahudi: Maneno Makali Lakini Ingali Inadumisha Mahusiano Mazuri

Indonesia imeyataka mataifa ya Kiislamu na Kiarabu kukata uhusiano wa kibiashara na kiuchumi na ‘Israel’ ili kukomesha ghasia mjini Gaza. Katika kikao cha Riyadh cha Jumuiya ya Nchi za Kiarabu na OIC, Makamu wa Waziri wa Mambo ya Nje Anis Matta alisisitiza ulazima wa kukata vitega uchumi vinavyohusiana na taasisi za Kizayuni na kuimarisha biashara ndani ya uchumi wa nchi za Kiislamu. Licha ya wito huu, biashara ya Indonesia na ‘Israel’ ilifikia dolari milioni 173 kuanzia Januari hadi Septemba 2024, ongezeko la 24.6% kutoka mwaka uliopita.

Soma zaidi...

Mtazamo kwa Ghasia za Baada ya Uchaguzi wa Msumbiji

Kwa mujibu wa Kituo cha Demokrasia na Haki za Binadamu cha Msumbiji na shirika la Reuters, kufikia tarehe 8/11/2024, jumla ya vifo 34 viliripotiwa huku vyanzo vyengine vikisema kuwa waliouawa ni zaidi ya 50, kutokana na ghasia za baada ya uchaguzi. kutangazwa kwa mgombea wa chama tawala cha Front for Liberation of Msumbiji (Frelimo), Daniel Chapo kuwa mshindi wa uchaguzi wa rais uliofanyika mnamo Oktoba 24 mwaka huu ambapo wapinzani walidai kuwa matokeo ya kura yaliibwa.

Soma zaidi...
Jiunge kwa hii RSS feed

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu