Ijumaa, 08 Jumada al-thani 1447 | 2025/11/28
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

Hotuba ya Amiri wa Hizb ut Tahrir, Mwanachuoni Mkubwa, Ata Bin Khalil Abu Al-Rashtah kwa Wanaozuru Ukurasa wake kwa Mnasaba wa Idd ul Fitr iliyobarikiwa ya Mwaka 1446 H sawia na 2025 M

Ndugu na Dada Wapendwa: Idd hii inakuja na dola ovu ya Kiyahudi inafanya ukatili dhidi ya watu, miti na mawe huko Gaza na Palestina yote, inafanya hivyo kwa msaada wa Marekani, ambayo inaipatia mabomu, makombora na ndege. Ingawa si ajabu kwamba umbile la Kiyahudi kwa kuungwa mkono na Marekani linatekeleza hili, kwani wao ni adui wa Uislamu na Waislamu, lakini cha ajabu ni kwamba hakuna hata mmoja wa watawala katika nchi za Kiislamu anayechukua hatua, hasa wale walioko pambizoni mwa Palestina, ili kuyakusanya majeshi yao kuinusuru Gaza, watu wake, Al-Aqsa, na viunga vyake, na kuling'oa umbile la Kiyahudi kutoka kwenye mizizi yake, na kisha kuiregesha Palestina yote kwa watu wake. Je, yule anayeikalia kwa mabavu ardhi ya Kiislamu na akawatoa watu wake humo hastahiki kupigwa vita na majeshi ya Waislamu na kufukuzwa humo kama walivyowafukuza watu wake?

Soma zaidi...

Tangazo la Matokeo ya Kuutafuta Mwezi Muandamo wa Shawwal 1446 H Pongezi kwa Idd Al-Fitr Iliyobarikiwa

Ummah umepitia mateso ya kubaki chini ya nira ya tawala za vibaraka. Umeshuhudia kwa macho yake wenyewe watawala wakifuja mali zake kwa makafiri, wakoloni wa Magharibi, kuzitelekeza kwao na sababu zake, kuzuia kwao majeshi kusonga ili kuinusuru Palestina kutoka kwenye makucha ya Mayahudi wahalifu, uingiliaji wa wazi wa Magharibi katika dini yake na uadilifu wake, na jaribio la kuulazimisha kulishuhudia  umbile la Kiyahudi, na kuuacha na chaguo kati ya uhalalalishaji mahusiano au kifo. Mandhari na matukio haya yote yameufanya utambue kwamba bila ya utawala wa Uislamu, utabakia kukoloniwa, kulengwa, na kudhalilishwa. Kukinaika kwake kwa haja ya dola ya Khilafah kumeimarishwa, na kwa hakika, Khilafah imekuwa ni kiu yake.

Soma zaidi...

Umbile la Kiyahudi Linatekeleza Mauaji ya Halaiki na Unyanyasaji wa Kijinsia mjini Gaza. Je, Kuna Njia ya Kuamsha Uzembe Huu?

Tangu kutekelezwa Operesheni ya Kimbunga cha Al-Aqsa mnamo 7 Oktoba 2023, umbile la Kiyahudi limewatenga watu walio na msimamo thabiti wa Gaza na kumwaga chuki yake juu yao. Limefanya mauaji ya mfululizo ambayo yamesababisha makumi ya maelfu kuuawa shahidi, huku Umma wa Kiislamu ukiwa bado umefungwa pingu na majeshi yake yamenyamaza kimya kama watu wa makaburini! Lilianza tena mauaji yake baada ya kukiuka usitishaji vita, kwa uungaji mkono wa wazi wa Magharibi na ushirikiano wa wazi na wa aibu wa tawala angamivu katika nchi za Waislamu.

Soma zaidi...

Leo Gaza na Yemen, na Kesho nchi zengine za Waislamu, Isipokuwa Majeshi yao Yatangaze Kusonga

Kamandi Kuu ya Ulinzi ya Marekani (CENTCOM) ilitangaza kwamba jioni ya Jumamosi, 15 Machi 2025, ilianzisha msururu wa mashambulizi ya anga dhidi ya maeneo lengwa ya Mahouthi nchini Yemen. Ilidai kuwa ilifanya mashambulizi sahihi dhidi ya maeneo lengwa ya kundi hilo kote Yemen, ikihalalisha mashambulizi hayo kama utetezi wa maslahi ya Marekani, kuzuia dhidi ya maadui, na kuregesha uhuru wa bahari, kulingana na taarifa yake. Kufikia Alhamisi jioni, Machi 20, makumi ya mashambulizi ya anga ya Marekani dhidi ya Yemen yalikuwa yameripotiwa, na kusababisha vifo vya watu 53 na wengine zaidi ya 100 kujeruhiwa, wengi wao wakiwa wanawake na watoto. Kuna matarajio kwamba operesheni zitaendelea kwa wiki kadhaa. Haya ni mashambulizi ya kwanza dhidi ya Yemen tangu makubaliano ya kusitisha mapigano kati ya umbile la Kiyahudi na Hamas mjini Gaza Januari iliyopita, kufuatia kiapo cha Trump cha "kuwamaliza kabisa."

Soma zaidi...

Hizb ut Tahrir / Wilayah Uturuki: Dua ya Kunut “Kwa ajili ya Gaza... Mikono Imeinuliwa Mbinguni?!”

Kwa kuzingatia mauaji ya kikatili ya halaiki ambayo yamekuwa yakiendelea kwa zaidi ya miezi 17, yanayofanywa na umbile halifu la Kiyahudi dhidi ya Waislamu wasio na ulinzi katika Ukanda wa Gaza, ambayo yamesababisha kuuawa shahidi na kujeruhiwa kwa Waislamu zaidi ya 170,000, wanaume na wanawake hadi sasa, Hizb ut Tahrir / Wilayah ya Uturuki iliandaa amali “Dua ya Kunut” kufuatia umbile halifu la Kiyahudi kukiuka makubaliano dhaifu ya kusitisha mapigano alfajiri ya Jumanne, 18 Machi 2025, na kuanza tena mauaji yake ya kimpangilio ya Waislamu wasio na ulinzi, ambao wengi wao wakiwa ni wanawake, watoto na wazee, chini ya kichwa: Dua ya Kunut “Kwa ajili ya Gaza... Mikono Imeinuliwa Mbinguni?!”

Soma zaidi...
Jiunge kwa hii RSS feed

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu