Ijumaa, 08 Jumada al-thani 1447 | 2025/11/28
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

Marekani Yaanzisha Mashambulizi ya Kikatili kwa Yemen Huku Majeshi Yetu Yakitulia tuli, Yakishindwa Kuinusuru Yemen na Gaza!

Kwa siku nyingi sasa, Amerika imekuwa ikianzisha mashambulizi ya kikatili kwa watu wetu nchini Yemen, kwa kutumia kile Rais wa Marekani Trump alichoeleza kuwa "nguvu kuu mbaya." Alikuwa amewatisha hapo awali, akichapisha, “JAHANAM ITANYESHA JUU YENU KWA NAMNA AMBAYO KWAME HAMJAWAHI KUONA KABLA!!”

Soma zaidi...

Wakati wa Ziara yake nchini India, Tulsi Gabbard katika Taarifa yake Alieleza Kujitolea kwa Ushirikiano wa Marekani na India na Mapambano dhidi ya Uislamu na Waislamu

Ingawa maoni ya chuki yaliyotolewa na Mkuu wa Ujasusi wa Kitaifa wa Kruseda Amerika, Tulsi Gabbard wakati wa ziara yake nchini India juu ya mateso ya watu walio wachache nchini Bangladesh na 'Khilafah ya Kiislamu' hayakuwashtua watu wanaozingatia siasa na wapenda Uislamu wa nchi hii, yaliondoa aibu ya mwisho ya vibaraka wa Amerika nchini Bangladesh. Kwa sababu vibaraka hawa walikuuza kukubalika kusiko epukika kwa Amerika kama rafiki wa Bangladesh ili kukabiliana na India na kuwahakikishia watu wapenda Uislamu wa nchi hii kwamba Amerika ilikuwa imeacha sera ya "vita dhidi ya Uislamu". Ingawa ukweli ni kwamba, hata kama uongozi wa Amerika utabadilika, 'sera yao ya kigeni' haibadilika. Badala yake, Trump shupavu au utawala wake hupenda kuwatusi vibaraka wake na kufichua nia za ‘sera zao za kigeni’. Kwa hili ametaka uwajibikaji wa dolari milioni 29 ambazo zililipwa kwa vibaraka ili kubadilisha mazingira ya kisiasa ya Bangladesh, huku kutumia pesa kama hizo kudhibiti siasa za nchi huru ni uhalifu mkubwa na ni sawa na kuingilia masuala ya ndani ya nchi nyingine.

Soma zaidi...

Enyi Majeshi: Mna nini mnapo ambiwa: Nendeni katika Njia ya Mwenyezi Mungu, mnajitia uzito katika ardhi? Je, mmeridhia maisha ya dunia kuliko ya Akhera? Lakini starehe za maisha ya dunia kulinganisha na ya Akhera ni chache

Enyi Majeshi katika ardhi za Waislamu, hasa zile zinazoizunguka Palestina: Je, kuna udhuru wowote uliobaki kwa wanaoomba msamaha? Je, kuna hoja yoyote iliyobaki kwa wanaolaani? Vipi mnaweza kuona na kusikia uvamizi na mauaji ya Mayahudi hali mmekaa katika sehemu zenu, bila kutikisika, badala ya kuelekea katika ardhi ya Al-Ribat, Palestine Ardhi Iliyobarikiwa, ili kurudisha uvamizi wa Mayahudi na kuliondoa umbile lao?

Soma zaidi...

Hizb ut Tahrir / Wilayah Pakistan: Mjini Gaza, Mashahidi 400 ndani ya Masaa 5!

Maneno yanashindwa kuelezea uhalifu huu wa kutisha katika mwezi huu mtukufu. Mayahudi wa Netanyahu na Marekani ya Trump wanawaonea watu wasio na hatia huku wakiwa wamelala, wakitumia ndege 100, zikiwemo ndege za kivita za Marekani, kulenga mahema yaliyojaa raia, kwa kisingizio kwamba wapiganaji wachache wa upinzani wapo. Waliwafuatiulia huku kukiwa na udanganyifu waliouita "usitisha mapigano"!

Soma zaidi...

Mafanikio ya Kweli Mpaka Siku ya Mwisho ni kwa Umma wa Kiislamu Pekee

Hata leo, katikati ya misiba isiyohesabika na isiyoweza kuvumilika, Ummah huu umethibitika kuwa thabiti katika kitambulisho chake na hivyo hauwezi kuangamizwa. Imethibitika kuwa unastahiki vyeo ulivyotunukiwa na Mola wa walimwengu, Mwenyezi Mungu Azza wa Jall! Angalia Kashmir, India, Afghanistan... Angalia Waislamu wa Syria, Turkestan Mashariki, Myanmar, katika nchi za Afrika, duniani kote, na mwisho kabisa Waislamu wa Palestina na hasa Gaza! Magaidi hao wa Kizayuni wameshindwa katika kila lengo lao kuhusu Gaza. Ummah huu umethibitisha mara kwa mara, kwamba uwepo wake hauzimiki! Hata adui zake wawe wakatili kiasi gani!

Soma zaidi...

Hizb ut Tahrir / Wilayah Uturuki: Amali za Usiku “Mutachukua Hatua Lini kwa ajili ya Gaza?!”

Kwa kuzingatia mauaji ya kikatili ya halaiki ambayo yamekuwa yakiendelea kwa zaidi ya miezi 17, yanayofanywa na umbile halifu la Kiyahudi dhidi ya Waislamu wasio na ulinzi katika Ukanda wa Gaza, ambayo yamesababisha kuuawa shahidi na kujeruhiwa kwa Waislamu zaidi ya 170,000, wanaume na wanawake hadi sasa, Hizb ut Tahrir / Wilayah ya Uturuki iliandaa amali kubwa za usiku katika idadi kadhaa ya miji Uturuki kufuatia umbile halifu la Kiyahudi kukiuka makubaliano dhaifu ya kusitisha mapigano alfajiri ya Jumanne tarehe 18/03/2025.

Soma zaidi...
Jiunge kwa hii RSS feed

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu