Jumanne, 07 Shawwal 1445 | 2024/04/16
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

Mauaji ya Nablus, na Ushujaa wa watu wake, Yafichua Wazembe, na Kutuma Ujumbe kwa Majeshi ya Kiislamu!

Mujahidina watano waliuawa shahidi, akiwemo mmoja wa viongozi mashuhuri wa kundi la Areen Al-Asoud (Shimo la Simba), Wadih al-Hawah, na wengine zaidi ya 20 walijeruhiwa kwa risasi za jeshi la Mayahudi. Majeraha ya watano kati yao yalielezewa kuwa mabaya, wakati wa shambulizi kwenye Mji wa Kale wa Nablus.

Soma zaidi...

Je, Huduma za Usalama na Huduma ya Kijasusi ya Kijeshi Zinatoa Kinga kwa Wahalifu Miongoni mwa Wanachama wao?!

Katika mfano hatari, na uhalifu kamili wa kulaaniwa, jana, Jumamosi 15/10/2022, kundi la shabiha (wanamgambo) mjini Ramallah wanaohusishwa na vyombo vya usalama; kati ya mfanyikazi, watoto wake na mshirika wake wa karibu, anayejulikana kwa jina na cheo, waliwashambulia idadi ya wafanyikazi wa Hizb ut Tahrir kwa visu na marungu mbele ya Msikiti wa Saad bin Muadh mjini Ramallah

Soma zaidi...

Tangazo la Algiers... Umakinishaji wa Orodha za Mamlaka Zilizoharibika, Kung'ang'ania Udanganyifu, na Jitihada ya Kufufua Shirika Linalopaswa Kuzikwa

Huku mashambulizi ya umbile la Kiyahudi dhidi ya watu wa Ardhi Iliyobarikiwa ya Palestina yakizidi, mauaji, kuzingira na kunyanyasa, na huku makundi ya walowezi yakiharibu na kuwashambulia watu, na uvamizi wao kwa Al-Aqsa umeongezeka kwa kasi na ujeuri, na huku watu wa Palestina na watoto wao wakikabiliana na umbile la Kiyahudi kwa uthabiti, ushujaa, na ujasiri wote, makundi yanakusanyika nchini Algeria chini ya usimamizi wa serikali ya Algeria kutia saini makubaliano mapya ya maridhiano chini ya jina “Tangazo la Algiers!”

Soma zaidi...

Sheria ya Mtoto na Kanuni zake za Utendaji ni Utangulizi wa Kusambaratika kwa Familia, na Kisu chenye Sumu Upande wa Watu wa Palestina!

Sawia na jinai zake dhidi ya watu wa Palestina, Mamlaka ya Palestina (PA) imechapisha kanuni za utendaji kwa ajili ya hatua za kulinda na kumpa haki mtoto za mwaka 2022 katika toleo la hivi karibuni la Gazeti la Palestina, Na. 194, sheria ambayo inatoa njia ya kusambaratisha familia na kushambulia mfumo wa kijamii kwa kuharibu malezi ya baba kwa watoto wake na kuwatoa watoto katika familia zao na hukmu za dini yao!

Soma zaidi...

Mamlaka ya Palestina Inaendelea kutekeleza Dori ya Uvamizi katika Umwagaji damu ya Wapalestina

Kwa kushirikiana na umbile la Kiyahudi na uhali wake, vikosi vya Mamlaka ya kihalifu ya Palestina (PA) huko Nablus, jana usiku, tarehe 9/19/2022, walitekeleza uhalifu wao mbaya wa kumuua kijana Firas Yaish na kuwajeruhi wengine kadhaa, wakati wa uwakandamizaji wao wa waandamanaji wanaopinga kukamatwa kwa Mujahidina Musab Shtayyeh na Brigedia Jenerali Tabila ambao wanatafutwa na umbile la Kiyahudi wakati huo huo vikosi vya uvamizi vilikuwa vikikamata watu katika miji ya Ukingo wa Magharibi, na walowezi walikuwa wakivamia Mji wa Mkongwe wa Hebron wakiwa na ulinzi wa jeshi lao.

Soma zaidi...

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu