Alhamisi, 01 Muharram 1447 | 2025/06/26
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

“Baada ya Kuibuka kwa (Israel) Tulikabiliana na Ulimwengu wa Kiarabu Ulioungana, na Polepole Tukaugawanya”

Kwa maneno haya, Netanyahu anahutubia watu wake na ulimwengu, akijigamba kana kwamba amefanya hivyo. Kama ilivyo desturi ya watu wake, ni wachongezi, waongo na kudai wasichokuwa nacho! Kabla ya kuwepo kwa umbile la wale ambao Mwenyezi Mungu amewalaani na kabla ya kuvunjwa kwa Khilafah, “Ulimwengu wa Kiarabu” haukuunganishwa tu. Badala yake, ulikuwa ni umma mmoja chini ya dola moja. Umma huu haukugawanywa na nyinyi, bali mabwana zenu waliokubuni kwa uovu na hila. Mabwana wenu waliopigana na umma huu kwa karne nyingi, wakionja nguvu zake na kushuhudia kuanguka kwa miji yao mikuu mmoja baada ya mwingine. Konstantinopoli ilitekwa na dada yake (Roma) karibu kuanguka, lakini Mwenyezi Mungu akataka ibaki kuwa hifadhi kwa ushindi mpya ujao, Inshallah.

Soma zaidi...

Mamlaka ya Palestina ilimuua Rami Zahran, Kisha Mzee Mmoja, Ikikamilisha Uhalifu wake Dhidi ya Watu wa Palestina

Mnamo siku ya Jumanne,13/5/2025, vikosi vya usalama vya Mamlaka ya Palestina vilimuua kijana Rami Zahran kutoka kambi ya wakimbizi ya Al-Far'a huko Tubas. Kisha wakafuatilisha hili kwa kumuua mzee mmoja (Abu Khalil al-Saba'neh) kutoka mji wa Jenin. Huu ni mwendelezo wa jinai zake dhidi ya watu wa Palestina, zikiwemo za mauaji, uchomaji moto, ukamataji, uvamizi wa misikiti, na unyang'anyaji mali ya Wapalestina kinyume cha sheria, kula mali zao kwa njia ya dhambi na fujo.

Soma zaidi...

Nani Anasherehekea Maadhimisho ya Isra na Mi’raj?

Tawala za ulimwengu wa Kiislamu zinatoa wito wa kuadhimisha kumbukumbu ya mwaka huu, licha ya kuwa wametambua uwepo wa umbile linaloinajisi ardhi iliyobarikiwa ya Isra na Mi’raj. Wamesimama kando, wakishuhudia mito ya damu ya Wapalestina ikitiririka, mabomu yaliyosababisha nyumba kuwa vifusi, na uharibifu ulioharibu vitongoji, mazao, na vizazi. Wametazama huku hofu ikiwashika wazee na vijana, huku njaa isiyo kifani ikiwasibu, na huku baridi ikigandisha miguu na nyoyo za watu.

Soma zaidi...

Mamlaka ya Palestina Yafuata Mbinu za Mashetani Kuhalalisha Uhalifu wake katika Kambi ya Jenin!

Mamlaka ya Palestina (PA) ilikusanya vyombo vyake vya habari na vipaza sauti vya wasemaji na nzi wa kielektroniki (wanyanyasaji wa mtandaoni wanaounga mkono serikali) ili kuchafulia jina kambi ya Jenin na watu wake na kuhalalisha umwagaji wa damu yao. Kisha, ilikusanya vyombo vyake na majambazi katika mji wa Khalil al-Rahman, na wachache wa wale walioitwa watu mashuhuri waliojiuza kwa PA kwa manufaa maovu, na wale ambao iliwatishia kutoka kwa wafanyikazi na walimu. Ilitumia wizara, shule zilizofungwa, na kukodi mabasi ili Jimbo la Khalil al-Rahman, mji na wilaya, ionekane kuwa pamoja nayo katika kumwaga damu ya watu wa kambi ya Jenin. Hii ijapokuwa inajua na wale walio nyuma ya kwamba Khalil al-Rahman, pamoja na watu wake na koo zake, hawawezi kukubali kwamba itoa nusu ya neno kumwaga tone la damu ya Waislamu. Kwa kitendo hiki kiovu, inataka kuleta mgawanyiko kati ya watu wa Palestina (kaskazini na kusini) chini ya pazia la uongo la uhalifu wake.

Soma zaidi...

Tubas ni Shahidi wa Upendeleo wa Mamlaka ya Ndani ya Palestina dhidi ya Maadui wa Palestina na Watu wake

Ni zaidi ya uhaini, kwamba Mamlaka ya Ndani ya Palestina inatangaza uadui wake kwa watu wa Palestina, kama inavyotokea kwa kuwasaka Mujahidina wa Tubas, kuwakamata na kuwapiga risasi, kuwatawanya watu huko kwa gesi ya machozi, kuwaua Mujahidina na kuwatia nguvuni kama wafanyavyo Mayahudi, sawa kwa sawa, na kutenda kwa niaba yake kwa kujaza pengo wakati inashughulika na uvamizi wake dhidi ya Gaza na Lebanon.

Soma zaidi...

Mamlaka ya Palestina Iliyofungamana na Maadui wa Mwenyezi Mungu Yakamilisha Dori ya Ghadhabu katika Kuwatesa Watu wa Palestina na Kuwakamata Watetezi wa Haki

Siku chache zilizopita, vikosi vya usalama vya Mamlaka ya Ndani ya Palestina (PA) viliwakamata Sheikh Aws Abu Arqoub na Sheikh Muhammad Manasrah, wanachama wa Hizb ut Tahrir. Kwa kuwakamata wale wanaosema ukweli, PA na vikosi vyake vinasisitiza kuwa kiongozi wa Mayahudi, wakidunga visu watu wote wa Palestina.

Soma zaidi...

Umbile la Halifu la Mayahudi Kukiuka Nafasi za Ummah na Kuua Watu wake katika Miji Mikuu ni Uhalifu wa Tawala za Kioga mbele ya Umbile la Kiyahudi

Katika shambulizi la kiuhaini na lisilo na aibu, umbile halifu la Kiyahudi lilimuua mkuu wa afisi ya kisiasa ya Hamas jijiniTehran, ambapo Ndugu Ismail Haniyeh aliuawa shahidi alfajiri ya leo na adui wa Mwenyezi Mungu, Mtume Wake, na Umma. Tunamuomba Mwenyezi Mungu rehema na msamaha wake na amjaalie miongoni mwa mashahidi. Hakika sisi ni wa Mwenyezi Mungu, na hakika kwake Yeye tutaregea.

Soma zaidi...

Mkono wa Umbile Halifu Wavamia nchi Yetu ya Yemen na ash-Sham chini ya Njama za Tawala na Kukosekana kwa Uzuiaji

Ndege za umbile halifu la Kiyahudi zilianzisha msururu wa mashambulizi ya kichokozi dhidi ya Yemen. Wakati wa mkutano wake jana, Baraza la Mawaziri la umbile hilo linalohusika na masuala ya usalama liliidhinisha shambulizi hilo dhidi ya Yemen, kwani uvamizi huo ulilenga vituo vya kuhifadhi mafuta na kituo cha umeme katika bandari ya Hodeidah.

Soma zaidi...

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu