Jumatano, 08 Jumada al-awwal 1447 | 2025/10/29
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

Ujumbe kutoka Hizb ut Tahrir / Wilayah Sudan Wakutana na Mkuu wa Chama cha Adalah nchini Sudan

Ujumbe kutoka Hizb ut Tahrir / Wilayah Sudan, ukiongozwa na Ustadh Al-Nadir Muhammad Hussein, mjumbe wa Baraza la Hizb ut Tahrir katika Wilayah Sudan, akifuatana na Mhandisi Banqa Hamid, na Ustadh Issam al-Din Abdul Qadir, wanachama wa Hizb ut Tahrir, walimtembelea Ustadh Al-Tijani Abdul Wahab, mkuu wa Chama cha Adalah nchini Sudan, nyumbani kwake katika mji wa Al-Obeid, mnamo Ijumaa tarehe 05/09/2025, kama sehemu ya kampeni iliyoandaliwa na Hizb ili kutibua mpango wa kuitenganisha Darfur.

Soma zaidi...

Matendo ya Watawala wa Sudan na Misri Kuhusu Bwawa la An-Nahdha Upotevu wa Usalama wa Maji kwa Watu wa Bonde la Nile

Utaratibu wa mashauriano baina ya nchi mbili unaojulikana kama 2+2, unaojumuisha mawaziri wa mambo ya nje na unyunyiziaji maji wa Misri na Sudan, walifanya mkutano katika Wizara ya Mambo ya Nje ya Misri mnamo Jumatano, 3/9/2025, kujadili maendeleo katika faili la Bwawa la Grand Ethiopian Renaissance (GERD). Mkutano huo ulisababisha taarifa ya pamoja ambapo pande hizo mbili zilieleza makubaliano yao kamili kuhusu hatari ya hatua za upande mmoja zinazochukuliwa na Ethiopia kuhusu ujazaji na uendeshaji wa bwawa la GERD. Taarifa hiyo iliashiria hatari kadhaa zinazohusishwa na bwawa hilo, ikiwa ni pamoja na dhamana dhaifu ya usalama, mtiririko wa maji usio wa kawaida, na athari zinazoweza kutokea wakati wa ukame.

Soma zaidi...

Maslahi ya Nani Yanatumikiwa kwa Uamuzi wa Serikali wa Kufungua Tena Kivuko cha Mpakani cha Adre huku Watu wa Fashir Wakifa kwa Njaa?!

Serikali ya Sudan ilitangaza mnamo Jumanne kwamba itaongeza muda wa ufunguzi wa kivuko cha mpakani na Chad cha Adre kwa mashirika ya misaada ya kibinadamu hadi mwisho wa mwaka huu. Wizara ya Mambo ya Nje ilitoa taarifa ikisema kwamba hatua hii inathibitisha dhamira ya serikali ya kuhakikisha kwamba misaada ya kibinadamu inawafikia wale wanaohitaji nchini kote, na kuonyesha nia yake njema katika kuwezesha shughuli za kibinadamu.

Soma zaidi...

Enyi Watu wa Sudan, Mnaweza Kutibua Mpango wa Kuitenga Darfur, Basi Inukeni Kumtii Mwenyezi Mungu!

Katika hatua inayotarajiwa, kamanda wa Vikosi vya Msaada wa Haraka, Mohamed Hamdan Dagalo, alikula kiapo cha kikatiba kama mkuu wa Baraza la Rais la kile kinachoitwa serikali sambamba huko Nyala, mji mkuu wa Darfur Kusini, mnamo Jumamosi, 30/8/2025. Makamu wa Rais, wajumbe wa Baraza la Rais, na Waziri Mkuu pia walikula kiapo.

Soma zaidi...

Watu wa Al-Fashir Baina ya Nyundo ya Vita na Kinoo cha Njaa, na Hawana Wokovu isipokuwa kwa Dola ya Khilafah

Mji wa Al-Fashir, mji mkuu wa Jimbo la Darfur Kaskazini, unashuhudia janga halisi la kibinadamu, huku kukiwa na vita kati ya pande zinazopigana, ambapo makumi ya raia waliuawa katika siku chache zilizopita, huku wakaazi wakiteseka kutokana na kuzingirwa kwa zaidi ya mwaka mmoja, na njaa ya makusudi, katika kivuli cha kimya cha kituliwa shaka cha kimataifa, huku Umoja wa Mataifa ukithibitisha mauaji ya angalau watu 89 katika mapigano ya siku zilizopita.

Soma zaidi...

Wanachama wa Hizb ut Tahrir huko Abbasiya Taqli Watoa Wito Mkali kwa Waislamu Kutibua Mpango wa Marekani wa Kutenganisha Darfur

Kama sehemu ya kampeni iliyoandaliwa na Hizb ut Tahrir/ Wilayah Sudan ya kukwamisha mpango wa kuisambaratisha Sudan kwa kutenganisha eneo la Darfur, na kuzingatia umoja wa Ummah kama suala nyeti, suala la uhai na kifo, wanachama wa Hizb ut Tahrir huko Abbasiya walifanya mkutano mnamo Ijumaa, 6 Rabi' al-Awwal 1447 H sawia na 29 Agosti 2025 M, baada ya swala ya Ijumaa katika Msikiti wa Sheikh Yahya kituo cha kuhifadhi Quran. Walitoa wito wa dhati kwa Waislamu wa matabaka yote, wakiwemo wanasiasa, wanahabari, wanazuoni, maafisa na askari na wengineo, wakiwahimiza kutimiza wajibu wao wa kidini ili kuzuia kujitenga kwa Darfur.

Soma zaidi...

Mvua ni Baraka na Rehema, lakini bila Uchungaji imekuwa ni Laana!

Ni huzuni na pia inasikitisha kwamba msimu wa mvua hauji kwa ghafla, bali ni kipindi cha taarifa ambacho hurudiwa kila mwaka. Kinachoshangaza zaidi ni kwamba vituo vingi vya uchunguzi wa hali ya hewa vilionya kuhusu mvua kubwa, lakini asasi za serikali hazikuchukua hatua yoyote kuzuia madhara yake, ambayo yalikuwa mabaya zaidi kwa vijiji vya Jimbo la Mto Nile, mashariki mwa Sudan na hata Kordofan, miongoni mwa kwengine.

Soma zaidi...

Ujumbe kutoka Hizb ut Tahrir / Wilayah Sudan Wanamtembelea Mkuu wa Chama cha Democratic Unionist mjini Al-Obeid

Ujumbe kutoka Hizb ut Tahrir / Wilayah ya Sudan, ukiongozwa na Ustadh Al-Nazir Muhammad Hussein - Mjumbe wa Baraza la Hizb ut Tahrir katika Wilayah ya Sudan - akifuatana na Ustadh Issam al-Din Abdul Qadir, walimtembelea Ustadh Khalid Hussein, Mkuu wa Chama cha Democratic Unionist, katika afisi yake katika mji wa Al-Obeid, mnamo Jumanne 3 Rabi’ al-Awwal sawia na tarehe 26 Agosti 2025 M, kama sehemu ya kampeni iliyoandaliwa na Hizb ili kutibua mpango wa kuitenganisha Darfur.

Soma zaidi...

Ujumbe kutoka Hizb ut Tahrir / Wilayah Sudan Waitembelea Idara ya Muongozo na Ushauri katika Jimbo la White Nile

Ujumbe kutoka Hizb ut Tahrir / Wilayah Sudan – Mji wa Rabak, White Nile, uliitembelea Idara ya Muongozo na Ushauri mnamo Jumapili, 1 Rabi' al-Awwal 1447 H sawia na tarehe 24 Agosti 2025. Ujumbe huo ulikutana na mkuu wa Sekretarieti katika Jimbo la White Nile, Sheikh Abdul Mubara Mahmoud Al-Mahmoud. Ujumbe huo uliongozwa na Dkt. Ahmed Muhammad Fadl Al-Sayyid, mwanachama wa Hizb ut Tahrir, na alifuatana na Ustadh Faisal Madani, mwanachama wa Hizb ut Tahrir.

Soma zaidi...

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu