Jumamosi, 06 Dhu al-Hijjah 1447 | 2026/05/23
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

Hizb ut Tahrir / Wilayah Pakistan: Kampeni “Katika Kumbukumbu ya Miaka 14 ya Kutekwa Nyara Kwake… Mwachilieni Huru Naveed Butt!”

Hizb ut Tahrir / Wilayah Pakistan ilizindua kampeni ya mitandao ya kijamii, haswa kwenye mtandao wa X (zamani ikijulikana kama Twitter), yenye kichwa “Katika Kumbukumbu ya Miaka 14 ya Kutekwa Nyara Kwake... Mwachilieni Huru Naveed Butt!” Kampeni hii inalenga kuishinikiza serikali dhalimu ya Pakistan, ambayo huduma zao za siri zilimteka nyara Mhandisi Naveed Butt, msemaji rasmi wa Hizb ut Tahrir nchini Pakistan, miaka 14 iliyopita mbele ya familia yake na majirani zake.

Soma zaidi...

Hizb ut Tahrir / Wilayah Tunisia: Kongamano la kila Mwaka la Khilafah “Kwa Khilafah Tunakabiliana na Udhibiti wa Marekani”

Mnamo Jumamosi 02 Mei 2026 M, Hizb ut Tahrir / Wilayah Tunisia iliandaa kongamano la kila mwaka la Khilafah katika ukumbi wa mikutano na makongamano ulio katika makutano ya Sakiet Ariana katika mji mkuu wa Tunis, lenye kichwa: “Kufeli kwa Dola ya Kisasa na Kutoepukika kwa Dola ya Khilafah”

Soma zaidi...

Hizb ut Tahrir / Wilayah Tunisia: Matembezi dhidi ya Ujanja wa Kijeshi wa Marekani katika ardhi ya Tunisia!

Mnamo Ijumaa, 17 Aprili 2026, matembezi yaliyoandaliwa na Hizb ut Tahrir / Wilayah ya Tunisia, yalianza kutoka Msikiti wa Al-Fath jijini Tunis, mji mkuu, baada ya swala ya Ijumaa. Matembezi hayo yalikuwa na kichwa: “Ujanja wa Kijeshi wa Marekani kwenye Ardhi ya Tunisia ni Uhalifu.”

Soma zaidi...

Hizb ut Tahrir Wilayah Sudan: Amali na Shughuli Wakati wa Mwezi Mtukufu wa Ramadhan 1447 H

Hizb ut Tahrir/Wilayah Sudan iliongeza shughuli zake za umma wakati wa mwezi mtukufu wa Ramadhan, ikihimiza jamii ya Waislamu kufanya kazi nayo ili kuanzisha jengo kuu la Uislamu: Khilafah Rashida kwa njia ya Utume, ambayo ilivunjwa miaka 105 iliyopita. Iliendesha hotuba za kisiasa, mihadhara, na visimamo katika viwanja vya misikiti, masoko, na maeneo mengine ya umma, pamoja na programu zake za kawaida katika afisi zake katika miji mbalimbali ya Sudan.

Soma zaidi...

Hizb ut Tahrir / Wilayah Sudan: Amali kwa Mnasaba wa Idd ul-Fitr Iliyobarikiwa 1447 H

Katika siku ya tatu ya Idd al-Fitr Iliyobarikiwa, sawia na Jumamosi, 12 Machi 2026 M, mashababu wa Hizb ut Tahrir/Wilayah Sudan walikusanyika katika afisi ya hizb katikati mwa jiji la Khartoum ili kupeana salamu za Idd. Mkutano huo ulijumuisha mashababu kutoka kote Khartoum, Omdurman, Jabal Awliya, Kalakila, Nile Mashariki, na maeneo mengine. Walitoa pongezi zao kwa Idd iliyobarikiwa na kuelezea furaha yao ya kuonana baada ya miaka mingi ya vita.

Soma zaidi...

Hizb ut Tahrir / Wilayah Uturuki: Amali Kubwa “Iokoeni Al-Aqsa! Simameni dhidi ya Amerika!”

Hizb ut Tahrir / Wilayah ya Uturuki, kupitia matembezi mikubwa na taarifa kwa vyombo vya habari zilizoandaliwa kote Uturuki chini ya kauli mbiu “Iokoeni Al-Aqsa! Simameni dhidi ya Amerika!”, ililaani ukandamizaji wa umbile nyakuzi la Kizayuni, kiburi cha mkoloni Amerika, na kimya cha watawala wa nchi za Kiislamu kuhusu udhalilishaji huu.

Soma zaidi...

Hizb ut Tahrir / Wilayah Tunisia: Matembezi “Nusra kwa Al-Aqsa na Wafungwa”

Mnamo siku ya Ijumaa, 3 Aprili 2026, matembezi yaliyoandaliwa na Hizb ut Tahrir katika Wilayah ya Tunisia, mji mkuu wa Tunisia, yalianza kutoka Msikiti wa Al-Fath baada ya swala ya Ijumaa. Matembezi hayo, yaliyofanyika kwa ajili ya kuunusuru Msikiti wa Al-Aqsa na wafungwa wa Palestina, yalikuwa na kichwa: “Kuhamasisha majeshi, kupindua viti vya watawala, na kutangaza jihad ndiyo njia pekee ya kuwaokoa wafungwa na kuikomboa Masra.”

Soma zaidi...

Hizb ut Tahrir / Wilayah Tunisia: Amali ya Jioni ya Ramadhan: “Mikataba ya Kimataifa... Mkataba wa Hudaybiyyah kama Mfano”

Kamati Kuu ya Mawasiliano ya Hizb ut Tahrir katika Wilayah ya Tunisia iliandaa amali ya jioni ya Ramadhan iliyopewa kichwa “Mikataba ya Kimataifa: Mkataba wa Hudaybiyyah kama Mfano” siku ya Jumapili, 8 Machi 2026, saa 4:00 PM kwa saa za Tunisia, katika Kituo cha Makongamano jijini Tunis.

Soma zaidi...

Hizb ut Tahrir / Wilayah Tunisia: Matembezi ya Takbira “Ni Dola ya Khilafah Pekee ndiyo Itakayomaliza Kiburi cha Amerika.”

Baada ya Swala ya Ijumaa ya mwisho ya Ramadhan Tukufu 1447 H, matembezi ya Takbira (Allahu Akbar) yaliyoandaliwa na Hizb ut-Tahrir / Wikayah ya Tunisia yalianza kutoka Msikiti wa Al-Fath katika mji mkuu, Tunis. Umati mkubwa wa Watunisia ulishiriki, wakipiga Takbira na Tahlil, na matembezi hayo yaliendelea kupitia barabara kuu za mji mkuu kuelekea Barabara ya Al-Thawra. Mabango yaliinuliwa, bango kuu likiwa limeandikwa, “Ni Dola ya Khilafah Pekee ndiyo Itakayomaliza Kiburi cha Amerika.”

Soma zaidi...

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu