Tanzania na Janga la Utegemezi
- Imepeperushwa katika Habari na Maoni
- Kuwa wa kwanza kutoa maoni!
- |
Jumapili ya tarehe 02 Juni, Juni 2024, Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na serikali ya Korea Kusini zilitia saini mikataba ya makubaliano ya ushirikiano kati ya nchi hizo mbili jijini Seoul. Mikataba hiyo ilijumuisha mkopo wa dolari bilioni 2.5 (Tsh trilioni 6.5) uliotolewa na Korea Kusini chini ya Mfuko wa Ushirikiano wa Maendeleo ya Kiuchumi wa Korea Kusini (EDCF) kwa ajili ya miradi mbalimbali ya miundombinu.



