Kanuni Sawa za Kiraia na Ukandamizaji wa Wanawake wa Kiislamu nchini India
- Imepeperushwa katika Habari na Maoni
- Kuwa wa kwanza kutoa maoni!
- |
Nchini India, wanawake wa Kiislamu kwa mara nyingine tena wanakuwa walengwa wa ajenda ya kisiasa ya chama tawala cha Bharatiya Janata Party (BJP) chini ya uongozi wa Waziri Mkuu Narendra Modi. Pendekezo la Kanuni Sawa ya Kiraia (UCC) si chochote zaidi ya jaribio jipya la kudhibiti zaidi maisha ya wanawake wa Kiislamu na kuzuia desturi zao za Kiislamu.