Hizb ut Tahrir / Wilayah Tunisia: Matembezi ya Takbira “Ni Dola ya Khilafah Pekee ndiyo Itakayomaliza Kiburi cha Amerika.”
- Imepeperushwa katika Tunisia
- Kuwa wa kwanza kutoa maoni!
Baada ya Swala ya Ijumaa ya mwisho ya Ramadhan Tukufu 1447 H, matembezi ya Takbira (Allahu Akbar) yaliyoandaliwa na Hizb ut-Tahrir / Wikayah ya Tunisia yalianza kutoka Msikiti wa Al-Fath katika mji mkuu, Tunis. Umati mkubwa wa Watunisia ulishiriki, wakipiga Takbira na Tahlil, na matembezi hayo yaliendelea kupitia barabara kuu za mji mkuu kuelekea Barabara ya Al-Thawra. Mabango yaliinuliwa, bango kuu likiwa limeandikwa, “Ni Dola ya Khilafah Pekee ndiyo Itakayomaliza Kiburi cha Amerika.”



