Jumapili, 02 Dhu al-Qi'dah 1447 | 2026/04/19
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu
kesho kutwa

kesho kutwa

Enyi Madhalimu! Fungueni Macho yenu!

Mnamo 19 Mei 2025, kesi ya wanachama 33 wa Hizb ut Tahrir, iliyodumu kwa karibu miezi minane, ilifikia kikomo. Kwa mujibu wa uamuzi wa mahakama, Musayev Shukrullah alihukumiwa kifungo cha miaka 17 katika jela maalum ya utawala; Selimov Dilshod alihukumiwa miaka 16 katika gereza maalum la utawala; Watu 20 walihukumiwa kifungo cha miaka 12 katika gereza maalum la utawala; Watu 8 walihukumiwa kifungo cha kati ya miaka 8 na 10, 4 kati yao katika hali maalum na wengine 4 katika hali kali; na watatu waliosalia walihukumiwa kati ya miaka 4 na 5 chini ya kifungo cha nyumbani.

Hizb ut Tahrir/ Wilayah Pakistan: Ummah na Majeshi Yake Lazima Ukatae Uhalalishaji Mahusiano na Mayahudi na Mabaniani!

Vyanzo vya kimatibabu vimeandika kuuawa shahidi kwa Wapalestina wasiopungua 42 kutokana na ulipuaji mabomu wa umbile la Kiyahudi katika Ukanda wa Gaza tangu alfajiri ya Jumatatu, 12 Mei 2025. Uvamizi huo ulianza tena jioni baada ya kusimama kwa saa kadhaa, ambapo mwanajeshi mmoja aliyekamatwa wa umbile la Kiyahudi aliachiliwa huru.

Mstari Mwekundu wa Unafiki: Jinsi Mauaji ya Halaiki mjini Gaza, Yanavyofichua Nyuso

Mnamo Jumamosi, tarehe 17 Mei 2025, kitovu cha kisiasa cha Uholanzi kiligeuka kuwa chekundu. Maelfu ya watu walijiunga na maandamano jijini The Hague, ambapo mstari mwekundu wa ishara ulichorwa - mstari unaoashiria mpaka wa maadili wa kile ambacho bado kingali kinaweza kutetewa. Kichocheo hakikuwa tu ushiriki wa ‘Israel’ katika Shindano la Nyimbo la Eurovision, bali zaidi ya yote ni kuongezeka kwa hasira juu ya baa la njaa mjini Gaza na kutochukua hatua kwa aibu kwa serikali za Magharibi.

Jibu la Swali: Mashambulizi ya Droni na Yanayojiri katika Vita nchini Sudan

Siku za hivi karibuni zimeshuhudia maendeleo ya ajabu katika vita. Droni zilishambulia Port Sudan, mji mkuu wa utawala, kwa siku sita mfululizo, na kushambulia uwanja wa ndege wa kiraia, kambi ya anga, na maghala ya mafuta, na kusababisha mgogoro wa mafuta kote nchini. Droni pia zilishambulia mji wa Kassala kwenye mpaka wa Eritrea upande wa mashariki, pamoja na miji mingine. Haya yote yalisababisha vikosi vya jeshi kuondoka kuelekea upande wa El Fasher na kuzingatia kulinda Sudan mashariki, kama BBC ilivyoripoti mnamo tarehe 10/5/2025. Je, hii ina maana kwamba shambulizi la mashariki mwa Sudan linalenga kuliondoa jeshi kutoka Darfur, na kuiacha ikiwa chini ya udhibiti wa Vikosi vya Msaada wa Haraka (RSF) pekee? Je, matukio haya ni utangulizi wa Jukwaa la Jeddah (kongamano la mazungumzo)? Au kuna malengo mengine?

Jiunge kwa hii RSS feed

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu