Jumapili, 30 Dhu al-Qi'dah 1447 | 2026/05/17
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu
kesho kutwa

kesho kutwa

Mauaji ya Halaiki mjini Gaza Hayatamalizika hadi sisi kama Waislamu Tumalize Utegemezi wetu kwa Demokrasia

Uchaguzi wa Marekani wa 2024 ulifanyika mnamo tarehe 5 Novemba huku Donald Trump, akipata ushindi mkubwa dhidi ya Kamala Harris. Waislamu wengi nchini Marekani, kwa mara nyengine tena walishiriki katika chaguzi hizi za kidemokrasia kwa matumaini kwamba kura yao ingesaidia kumaliza mauaji ya halaiki huko Gaza. Wengine walimuunga mkono Trump, ima wakiamini katika ahadi yake kwamba angeleta amani katika eneo hilo, au “kumuadhibu” Harris na utawala wa Biden kwa kuendelea kuunga mkono na kufadhili umbile la mauaji ya halaiki la Kizayuni. Wengine walimuidhinisha Harris, wakiamini kwamba yeye ndiye ‘la hafifu ya madhara mawili’ na njia bora kwa wapinzani wa vita vya Gaza kuendeleza ajenda zao. Wengine walipiga kura zao kwa mwakilishi wa Green Party, Jill Stein na mgombea wa People's Party Cornel West, kutokana na msimamo wao thabiti wa kupinga vita na kuahidi kukomesha mauaji ya halaiki.

Sio kila chenye Kumetameta ni Dhahabu

Tawala dhalilifu za vibaraka zimesisitiza kuthibitisha, kwa yakini, kwamba ni tawala ambazo si za Ummah, huku Ummah ukiwa si sehemu yake. Katika kupambana waziwazi na hisia za Waislamu, zilikimbilia kumpongeza Rais Trump wa Marekani baada ya kutangazwa ushindi wake katika uchaguzi huo. Zilikimbilia kumpa majukumu yao ya utiifu na uaminifu, na kusahau kuuawa kwa watoto wa Waislamu huko Gaza, Lebanon na kwengineko katika vita vya wazi vinavyoongozwa na Amerika, kwa kutumia mali zake, huku wakisahau kauli za bwege huyu katika kuunga mkono kwake wazi kusiko na mipaka kwa Mayahudi. Je, inawezekana kutarajia kwamba zabibu zitatoka kwenye miiba?!

Jiunge kwa hii RSS feed

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu