Jumapili, 16 Safar 1447 | 2025/08/10
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

Mwaliko wa Kuhudhuria Kikao cha Kisiasa

Afisi ya Habari ya Hizb ut Tahrir katika Wilayah ya Sudan inafuraha kuwaalika wanahabari, wanasiasa, na wote walio na hamu na masuala ya Umma kuhudhuria na kushiriki katika kikao kipya cha kisiasa, ambacho kitamwalika Ustadh Muhammad Jami' (Abu Ayman), Msaidizi wa Msemaji Rasmi wa Hizb ut Tahrir katika Wilayah ya Sudan.

Soma zaidi...

Kuzingirwa kwa Gaza ni Ushahidi wa Khiyana ya Serikali ya Misri

Gaza imeingia katika awamu ya tano njaa (awamu ya janga la njaa), kulingana na ripoti ya Umoja wa Mataifa. Huku Waislamu kila mahali wakijaribu kuwanusuru ndugu zao kwa michango na kuanzisha misafara ya kuvunja mzingiro dhidi yao, nchi jirani zinatazama bila harakati yoyote—mbele yao zaidi ni Misri, ambayo ina mpaka na Gaza, lakini inadai kuwa haina usemi katika suala hilo na imeridhia kuchukua dori ya mpatanishi. Hivyo, je, kweli Misri haina uwezo wa kuwanusuru watu wa Gaza?!

Soma zaidi...

Enyi Wanazuoni wa Al-Azhar: Ikiwa hamtasema neno la haki leo... lini basi?!

Katika wakati ambapo sura za mauaji yanayofanywa na Mayahudi mjini Gaza zikiongezeka, na chakula, dawa, na maji vikizuiliwa kwa watoto, wanawake na wanaume, Al-Azhar ilitoa tamko la kulaani "jinai ya kuweka njaa" inayofanywa na umbile halifu la Kiyahudi. Taarifa hiyo ilifutwa baadaye! Basi je, inajuzu kilio dhidi ya dhalimu kifutwe?! Na je, sauti ya wanazuoni inaweza kukaa kimya dhidi ya mauaji?! Taarifa hiyo ilikuja ikiwa imejaa misamiati ya kibinadamu, yenye kuwavutia watu wenye dhamiri hai, jumuiya ya kimataifa, na dola zenye ushawishi, na kutoa wito wa kufunguliwa kwa vivuko na utoaji wa misaada. Umbile la Kiyahudi lilielezewa kuwa linafanya uhalifu wa njaa, likituhumiwa kwa mauaji ya halaiki na kuzuia misaada, na ilitoa wito kwa mashirika ya kibinadamu, Umoja wa Mataifa na mashirika ya kimataifa kusonga mbele kufungua vivuko, pamoja na kuwaombea dua watu wa Gaza kwamba Mwenyezi Mungu awanusuru na alipize kisasi kwa ajili yao.

Soma zaidi...

Kuitelekeza Gaza ni Doa katika vipaji vya Nyuso Zenu Enyi Wanajeshi wa Kinana na muhimu zaidi, ni Swali kutoka kwa Mwenyezi Mungu Siku ya Kiyama

Kila siku, mtoto mjini Gaza hufa kwa njaa, au mzee hupumua pumzi yake ya mwisho bila dawa, au mwanamke hufunga macho yake kwa mara ya mwisho kwa maumivu yasiyoweza kuvumilika kutokana na kiu au njaa. Kila saa mbingu hutokwa na machozi, mawe yanapiga kelele, na ardhi inawalaani wale waliowaacha peke yao. Hii ndiyo Gaza... Gaza, ambayo imezingirwa si tu kwa mipaka na vifaru, bali na uzio wa usaliti uliosukwa na viongozi wa majeshi, watawala wa khiyana, na kimya cha Umma wao.

Soma zaidi...

Kuhamishwa kwa Watu wa Arish ni Uhalifu wa Kisiasa Uliojificha kama Maendeleo

Wakati serikali ya Misri ikizungumzia "kuimarisha bandari ya Arish," kuigeuza kuwa bandari ya kimataifa na kuiunganisha na mradi mpya wa ukanda wa kiuchumi, uhalifu wa halisi unafanywa dhidi ya wakaazi wa kitongoji cha Al-Raisa huko Arish. Watu wanalazimishwa kuondoka majumbani mwao chini ya athari ya matingatinga, na nyumba zao zinabomolewa kinyume na matakwa yao kwa kisingizio cha manufaa ya umma. Wanakabiliwa na shinikizo la kisaikolojia na mazungumzo ambayo hayaendani na hadhi ya kibinadamu na yanakiuka kanuni za Kiislamu.

Soma zaidi...

Vyombo vya Ukandamizaji vya Serikali ya Jordan Vyamkamata Sheikh Saeed Radwan kutoka Hizb ut Tahrir

Katika wakati ambapo watu wa Jordan kutoka kaskazini hadi kusini na kutoka matabaka yote ya maisha wanaongeza hasira na uungaji mkono kwa Gaza, ambayo inaangamizwa, watu wake wanakabiliwa na njaa ya kikatili inayolazimishwa na umbile halifu la Kiyahudi kwa njama za fedheha kutoka kwa serikali ya Jordan, na huku vyombo vya ukandamizaji vya serikali hii vikisimama kupinga uasi huu kupitia ukandamizaji na ukamataji wa wana na watu waheshimiwa wa Umma huu.

Soma zaidi...

Hasira ya Watu wa Gaza kutoka Ng'ambo za Bahari Inataka Mzingiro Uvunjwe... Watu wa Misri na Jeshi lake Watakasirika Lini? Lini Hasira yao Itakuwa Moto wenye Kuteketeza Umbile la Kiyahudi na Tawala za Mamluki Zinazolilinda?

Wakati Gaza ikiwa inakufa kwa njaa, ikizingirwa kwa kimya cha aibu cha Waarabu na njama ya wazi ya kimataifa, kijana mmoja wa Kimisri kutoka ng'ambo, Anas Habib, alifunga milango ya ubalozi wa Misri nchini Uholanzi na kumwaga unga kwenye kizingiti chake. Alipiga kelele kwa jina la watu waliozingirwa wa Gaza na kuliita jeshi lake nchini Misri kuvunja mzingiro, kufungua kivuko, na kumaliza njaa ya kupangwa... Kilio kutoka nchi ya mbali kilisikika ndani ya nyoyo huru. Je, kuna yeyote kati ya watu wa Misri atakayejibu? Je, kuna ulinzi wowote katika nyoyo za watu wa jeshi la Kinana? Au kufuli zilizowekwa kwenye ubalozi wa Misri jijini The Hague ni za kikatili kidogo kuliko kufuli zilizowekwa kwenye utashi na silaha zao?!

Soma zaidi...

Mafanikio ya Kiuchumi ya Mahouthi Baada ya Miaka 11: Kutengeneza Sarafu Mbili za Riyal 50 na 100!!

Mnamo Jumatatu, tarehe 14/07/2025, Waziri wa Habari wa Wizara ya Ujenzi na Mabadiliko, Hashem Sharaf al-Din, alitoa taarifa kwa Shirika la Saba, ambapo alisema: “Kila sarafu ya kitaifa inayotolewa kwa wananchi ni daraja la kuelekea katika maamuzi huru, na kila ushindi wa kiuchumi unaopatikana ni ngome isiyotikisika mbele ya dhoruba na kila mafanikio ya kifedha ni ngao ya kinga katika vita vya hadhi, na upanga unaozikata njama za maadui wa Yemen, kwa fadhila ya Mwenyezi Mungu kwanza, kisha kwa azma ya watu wasiojua lisilowezekana.”

Soma zaidi...

Ewe Hamasa ya Uislamu ndani ya Umma wa Muhammad (saw) Mtume wa Mwenyezi Mungu (saw) amesema: “Si Muumini anayelala ameshiba na hali jirani yake ana njaa.”

Miti na mawe yamelia kutokana na hofu iliyotusibu. Vifua vyetu vinatoa damu na maumivu, watoto wetu wanasisimka kutokana na njaa na kiu, wanawake wetu wanalia ili kuchochea wivu wa ulinzi wa waumini. Asiyeuawa kwa kupigwa mabomu hufa kwa njaa na kiu. Lakini maumivu ya usaliti ni mazito juu yetu kuliko milipuko ya mabomu, njaa, na kiu. Kaka na dada zenu mjini Gaza wanatangatanga bila malengo, bila makaazi, sauti zao zimenyamazishwa na udhaifu ulioletwa na njaa na kiu, baada ya kutoweka matumaini yote kwamba yeyote isipokuwa Mwenyezi Mungu atakuja kuwasaidia. Wanapiga kelele: Uko wapi Umma wa Uislamu? Iko wapi hamasa ya Dini? Uko wapi msaada wa Waumini?

Soma zaidi...

Taasisi zote za Kikoloni, ikiwemo Tume Kuu ya Umoja wa Mataifa ya Haki za Kibinadamu, ni Ala za kufikia Maslahi ya Marekani; Khilafah pekee kupitia kung'oa Misingi ya Taasisi zote hizi ndio itakayolinda Uislamu, Maslahi ya Watu na Ubwana wa Nchi hii

Licha ya maandamano na wasi wasi wa ngazi zote za wananchi na vyama vya kisiasa, hatimaye serikali ya mpito ya Bangladesh imetia saini makubaliano ya kuanzisha afisi ya taasisi ya Kikoloni yenye ushawishi wa Marekani, Tume Kuu ya Haki za Binadamu ya Umoja wa Mataifa. Uamuzi huu wa serikali umekaribishwa na mashirika ya wanawake yenye chuki dhidi ya Uislamu, ambayo yanashiriki kikamilifu katika usawa wa kijinsia wa Magharibi, utambuzi wa kijamii wa "taaluma" ya kuchukiza ya ukahaba, na kile kinachoitwa haki za binadamu za LGBTQ ikiwa ni pamoja na ushoga unaoangamiza jamii; ilhali wana utata na kukosolewa na ngazi zote za watu kwa sababu hawana sauti katika kuweka haki adilifu na utu wa wanawake, uhuru kutokana na kazi za kikatili, na uboreshaji wa hali ya maisha.

Soma zaidi...
Jiunge kwa hii RSS feed

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu