Jumapili, 16 Safar 1447 | 2025/08/10
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

Kitengo cha Wanawake katika Afisi Kuu ya Habari ya Hizb ut Tahrir Chazindua Kampeni ya Kimataifa “Vita vya Sudan: Hadithi ya Ukoloni, Usaliti na Udanganyifu”

Mgogoro wa kikatili nchini Sudan kati ya Wanajeshi wa Sudan (SAF) wanaoongozwa na mtawala mkuu wa Sudan, Jenerali Abdel Fattah al-Burhan, na Kikosi cha Msaada wa Haraka (RSF) kinachoongozwa na Mohamed Hamdan Dagalo (Hemedti), ambaye hapo awali alikuwa naibu wa al-Burhan katika Baraza Kuu, sasa umeingia mwaka wake wa tatu, na kusababisha vifo vya maelfu ya raia. Baadhi ya makadirio yanaweka idadi ya waliofariki katika vita hivi vya kipumbavu kufikia 150,000, huku kukiwa na ukatili wa kutisha uliofanywa na pande zote mbili, ikiwa ni pamoja na mauaji ya kinyama, mateso, ubakaji mkubwa na uhalifu mwingine wa kingono dhidi ya wanawake na wasichana. Mauaji ya kikabila pia yameripotiwa, huku jamii nzima zikiteketezwa kwa moto na kuangamizwa, na mauaji ya halaiki katika miji mbalimbali, vijiji na kambi za watu waliokimbia makaazi yao.

Soma zaidi...

Hizb ut Tahrir / Wilayah Uturuki: Matembezi ya Halaiki ya Kuinusuru Gaza “Kuwahutubia wale Wanaohusika!”

Kwa kuzingatia mauaji ya kikatili (mauaji ya halaiki) ambayo yamekuwa yakiendelea kwa muda wa miezi 21, yanayofanywa na umbile halifu la Kiyahudi dhidi ya Waislamu wasio na ulinzi katika Ukanda wa Gaza, ambayo yamesababisha kuuawa shahidi, kujeruhiwa na kupotezwa kwa zaidi ya wanaume na wanawake 200,000 Waislamu hadi sasa. Hizb ut Tahrir / Wilayah ya Uturuki iliandaa matembezi makubwa ya halaiki kote nchini Uturuki licha ya serikali ya Uturuki kuyapiga marufuku.

Soma zaidi...

Mkataba wa Biashara na Unyenyekeaji wa Indonesia kwa Maslahi ya Marekani

Rais wa Marekani Donald Trump alitangaza makubaliano ya kibiashara na Indonesia, kupunguza ushuru unaotishiwa wa 32% kwa bidhaa za Indonesia hadi 19%. Kwa upande wake, Indonesia ilijitolea kununua nishati ya Marekani kwa dolari bilioni 15, bidhaa za kilimo kwa dolari bilioni 4.5, na ndege 50 za Boeing, ikiwa ni pamoja na aina ya 777. Trump alidai Marekani itapata ufikiaji kamili wa soko la Indonesia bila kulipa ushuru. Makubaliano hayo yalifuatia vitisho vya ushuru wa juu na yalikamilishwa baada ya mazungumzo na Rais wa Indonesia Prabowo Subianto. Bado haijulikani ni lini upunguzaji wa ushuru na ununuzi utaanza kutekelezeka. Biashara ya Indonesia na Marekani ilifikia karibu dolari bilioni 40 mwaka 2024, na nakisi ya biashara ya bidhaa za Marekani ya takriban dolari bilioni 18.

Soma zaidi...

Idhini ya Marekani sio Kipimo cha Uamuzi wa Kisiasa kwa Umma wa Kiislamu

Mnamo tarehe 17 Julai 2025, Dawn News ilinukuu kutoka Reuters, "Ikulu ya White House mnamo Alhamisi ilisema kwamba hakuna ziara ya Rais wa Marekani Donald Trump iliyopangwa Pakistan "kwa wakati huu" baada ya kuenea kwa taarifa za safari hiyo. Mapema siku hiyo, baadhi ya vituo vya habari vya televisheni vya ndani viliripoti, vikinukuu vyanzo, kwamba Trump alitarajiwa kuzuru Pakistan mwezi Septemba. Chaneli za habari zilisema kwamba Trump pia angetembelea India baada ya kuwasili jijini Islamabad mwezi Septemba. Chaneli hizo baadaye ziliondoa ripoti zao.” [Dawn]

Soma zaidi...

Taarifa ya Msemaji Rasmi wa Hizb ut Tahrir katika Wilaya ya Sudan katika Mkutano na Waandishi wa Habari Uliofanyika Jumamosi, 19/07/2025, jijini Port Sudan “Hakuna Serikali Inayoleta Matumaini Isipokuwa chini ya Uislamu na Dola yake ya Khilafah”

Mnamo Jumatatu, 19/05/2025, Mwenyekiti wa Baraza la Utawala, Abdel Fattah Al-Burhan, alitoa uamuzi wa kumteua afisa wa zamani wa Umoja wa Mataifa Kamal Idris kuwa Waziri Mkuu kuunda serikali ya kitaalamu. Siku hiyo hiyo, Al-Burhan pia alitoa uamuzi wa kufutilia mbali agizo la hapo awali lililowapa wanachama wa Baraza Kuu usimamizi wa wizara na vitengo vya serikali ya kifederali.

Soma zaidi...

Uislamu uko Mbali na Mazungumzo ya Dini Mseto

Mnamo tarehe 5 Julai 2025, jumba jipya la ibada katika Kanisa la Arise and Shine Tanzania lililopo Kawe, viungani mwa jiji la Dar es Salaam lilizinduliwa. Kanisa hilo linaongozwa na Mwinjilisti na anayejiita ‘mtume’ Boniface Mwamposa ambaye mahubiri yake mwaka 2020 yalileta msiba wa vifo vya waumini zaidi ya 20 kutokana na mkanyagano waliokuwa wakikimbia kupakwa mafuta yenye baraka.

Soma zaidi...

Mwaliko wa Kuhudhuria Mkutano na Waandishi Habari

Kwa ndugu na dada zetu waheshimiwa katika vyombo vya habari, ikiwa ni pamoja na magazeti, redio, na runinga, sisi, katika Hizb ut Tahrir / Wilayah Sudan, tuna furaha kukualikeni kuhudhuria mkutano na waandishi wa habari wenye kichwa: Hakuna Serikali inayoweza Kutoa Matumaini Isipokuwa chini ya Uislamu na Dola yake ya Khilafah.

Soma zaidi...

Ziara ya Azerbaijan: Hatua kuelekea Kusukuma Uhalalishaji Mahusiano na Umbile la Kiyahudi Ambayo Itakuwa ni Mchomo wa Kisu ndani ya Moyo wa Ummah

Chanzo cha kidiplomasia jijini Damascus kilisema mnamo Jumamosi kwamba mkutano wa moja kwa moja utafanyika kati ya afisa mmoja wa Syria na afisa mwengine wa 'Israel' huko Baku kando ya ziara ya Rais wa Syria Ahmad Al-Shara nchini Azerbaijan, kulingana na shirika la habari la Agence France-Presse (AFP).

Soma zaidi...
Jiunge kwa hii RSS feed

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu