Gazeti la Al-Raya: Vichwa Vikuu vya Toleo 550
- Imepeperushwa katika Al-Rayah
- Kuwa wa kwanza kutoa maoni!
- |
Hizb ut Tahrir/Wilayah Lebanon iliandaa maandamano ya Takbir, Tahlil, na Tahmid katika mji wa Tripoli, Syria, chini ya kauli mbiu "Tuko Pamoja nawe, ewe Gaza, tukipiga Takbir na Tahmid," kwa mnasaba wa ujio wa siku kumi za kwanza za Dhul-Hijjah 1446 H – 2025 M Idd al-Adha iliyobarikiwa. Matembezi hayo yalihitimishwa kwa dua ya kugusa moyo ya Sheikh Ahmed Al-Shamali.
Hizb ut Tahrir Wilayah ya Kenya imechapisha toleo jipya la Jarida la UQAB kwa ajili ya mwezi wa Juni 2025 M.
Shirika la Afya Duniani (WHO) limefichua kuwa takriban wagonjwa 60,000 wa kipindupindu wamerekodiwa nchini Sudan, na kusababisha vifo vya zaidi ya 1640, likionya madhara ya kuporomoka kwa mfumo wa afya nchini humu. Ufichuzi huu unakuja wakati kipindupindu kikienea kwa kasi katika Jimbo la Khartoum, ambapo maambukizi mapya yanazidi 90% ya jumla ya nchi, haswa huko Karari, Omdurman, na Ombada. Mnamo Jumanne, 27/5/2025, Wizara ya Afya ya Sudan ilitangaza kurekodi kesi 2729, pamoja na vifo 172, katika wiki moja. Waziri wa Afya wa Sudan Dkt. Haitham Mohamed Ibrahim alisema kuwa kuenea kwa kipindupindu jijini Khartoum kunatokana na kuzorota kwa hali ya mazingira na matatizo ya vyanzo vya maji ya kunywa. Wakati huo huo, Waziri Mkuu mpya Kamil Idriss anatoa wito kwa WHO, huku ripoti za vyombo vya habari zikisema kuwa anawasiliana na Mkurugenzi Mkuu wa WHO Tedros Adhanom ili kujadili kusaidia juhudi za kudhibiti kipindupindu nchini humu.
Hizb ut Tahrir / Wilayah Sudan, inamuomboleza kwa macho yenye machozi na nyoyo ziliyoridhika na mapenzi ya Mwenyezi Mungu marehemu: Al-Kamel Mohammad Khair
Islamabad, Pakistan – Baraza la mawaziri la Pakistan mnamo Jumanne lilimpandisha cheo Jenerali Syed Asim Munir, mkuu wa jeshi la nchi hiyo, hadi cheo cha field marshal, kufuatia mzozo wa hivi majuzi wa kijeshi kati ya nchi hiyo na India.
Mnamo Aprili 2025, wakati wa Mkutano wa Mawaziri wa Mambo ya Nje wa BRICS nchini Brazil, Waziri wa Mambo ya Nje wa Malaysia Datuk Seri Mohamad Hasan alitoa ujumbe ulio wazi: ulimwengu hauwezi tena kutegemea utawala wa dola moja ili kuhakikisha utulivu wa kimataifa. Alihimiza mataifa ya Kusini mwa Ulimwengu – inayojumuisha nchi zinazoendelea kote Asia, Afrika, Amerika ya Kusini, na Oceania – kuinuka kwa pamoja na kuongoza uundaji wa mfumo mpya wa kilimwengu. Matamshi yake yanaangazia sauti za vibwagizo vinazokua zisizoridhika na utawala wa muda mrefu na kuanguka kwa uaminifu wa utawala wa kimataifa unaoongozwa na Marekani.
Taarifa ya mwisho ya Mkutano wa Waarabu, ulioandaliwa na mji mkuu wa Iraq, Baghdad mnamo tarehe 17 Mei 2025, ilisisitiza haja ya kuleta misaada ya kibinadamu mjini Gaza. Watawala wa Waislamu, Waarabu na wasiokuwa Waarabu, wamezuia majeshi ya Waislamu kupigana na Mayahudi, kwa zaidi ya mwaka mmoja na nusu. Mtume ﷺ ametuambia kuwa kupigana na Mayahudi na kuwashinda kunaleta malipo makubwa.
Baada ya wasagaji wawili wanachama wa chama chenye uhusiano na Chuo Kikuu cha Marekani cha Beirut (AUBMC), chini ya kivuli na jina "Programu Oanishi ya Afya ya Jimai ya Wanawake (WISH) katika AUBMC," kutembelea shule ya upili ya wasichana jijini Tripoli, kwa uratibu wa Wizara ya Elimu; kisha kwa mbwembwe na bila aibu kuendekeza mambo machafu na kuonyesha picha na maudhui machafu kwa wanafunzi, wazazi wakasukumwa kuripoti tukio hilo kwa uongozi wa shule, ambao nao ulieleza kuwa wawili hao walikuja shuleni kwa amri ya Wizara ya Elimu na Elimu ya Juu!
Je, watu wa Jordan wanasherehekea uhuru unaodaiwa wakati jana, daktari Muislamu mwenye msimamo thabiti huko Gaza alipoteza watoto wake tisa wote kwa wakati mmoja, kutokana na kombora lililorushwa na ndege ya jeshi la mauaji ya halaiki nyumbani kwao, katika mandhari ya kinyama isiyo na kifani katika historia ya mwanadamu?