Mwenye Hekima si Yule Anayesitasita Kati ya Mema na Maovu, Bali Yule Anayechagua Mema
- Imepeperushwa katika Khilafah
- Kuwa wa kwanza kutoa maoni!
- |
Ni sababu gani za udhaifu wa Waislamu leo? Kwa nini heshima yao inavunjwa, ardhi yao inanyakuliwa, na wanamefukarishwa na kutiwa njaa, lakini hawajitetei dhidi ya dhulma, udhalilifu, na kudunishwa? Kwa nini wanatazamana wakifa kwa njaa, mauaji, na mateso mikononi mwa makafiri wahalifu bila kuinua kidole? Kwa nini wanahisi hawana msaada, dhaifu, na watiifu kwa Magharibi mbele ya majanga na vitisho vyote vinavyowapata?



