Alhamisi, 05 Rajab 1447 | 2025/12/25
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

Kuwakataa Wanariadha wa ‘Israel’: Kipimo Halisi cha Msimamo Madhubuti wa Indonesia?

Indonesia: Mahakama ya Usuluhishi wa Michezo (CAS) ilikataa rufaa ya Shirikisho la Michezo ya Viungo (Gymnastics) la ‘Israel’ (IGF) kuruhusu wanariadha wake kushiriki Mashindano ya Dunia ya Sanaa za Gymnastiki jijini Jakarta, Indonesia, kuanzia Oktoba 19–25, 2025. Serikali ya Indonesia iliwanyima viza wachezaji sita wa mazoezi ya viungo wa ‘Israel’, ikionyesha uungaji mkono kwa Wapalestina na shinikizo la ndani. IGF ilkata rufaa kwa CAS na Shirikisho la Kimataifa la Gymnastiki (FIG), ikiomba hatua za kuhakikisha ushiriki au kubatilisha michezo hiyo. CAS ilitupilia mbali rufaa zote mbili, na FIG ilisema haina mamlaka juu ya maamuzi ya visa. Indonesia ilithibitisha tena msimamo wake, ikiegemea katika sera yake ya kigeni na hisia za umma.

Soma zaidi...

Kimbunga cha Al-Aqsa kiko Hai na Kinaendelea

Operesheni ya Kimbunga cha Al-Aqsa haikuwa tukio la muda mfupi ambalo lilimalizika kwa makubaliano ya mhalifu Trump na dola ya kikafiri nyuma yake, Marekani, muungaji mkono rasmi wa umbile la Kiyahudi. Badala yake, Kimbunga cha Al-Aqsa kilikuwa ni cheche iliyowasha moto ndani ya nyoyo za Waislamu, na kuzifungua akili na nyoyo zao. Waliona unyonge na uovu wa watawala wao wasaliti, na wakatambua unafiki wa wale wanaodai kuwa ni na ubinadamu, na wanaotetea haki za wanawake na watoto. Wakawa na hakika kwamba sheria za kimataifa, na mikataba si chochote ila ni silaha inayotumiwa na makafiri, dhidi ya Uislamu na Waislamu.

Soma zaidi...

Utumiaji kama Silaha wa “Chuki dhidi ya Mayahudi” kunyamazisha Nusra ya Ukombozi wa Palestina

Katika siku za hivi karibuni, kumekuwa na mijadala mingi nchini Uingereza ikiashiria kuwepo mafungano kati ya maandamano ya Palestina na kuongezeka kwa chuki dhidi ya Mayahudi na mashambulizi dhidi ya Mayahudi nchini humo. Kabla ya kumbukumbu ya mwaka wa 2 wa shambulizi la Octoba 7 la Hamas dhidi ya umbile la Kizayuni, Waziri Mkuu wa Uingereza Keir Starmer, aliwataka wanafunzi wasijiunge na maandamano yanayoiunga mkono Palestina siku hiyo, akionya juu ya “kuongezeka chuki dhidi ya Mayahudi katika barabara zetu”, na kwamba “sio tamaduni ya Uingereza kuwa na heshima ndogo kwa wengine” kwa kufanya maandamano juu ya kumbukumbu hiyo, na kuongeza kuwa maandamano yametumiwa  na baadhi kama “udhuru wa kuchukiza kuwashambulia Mayahudi wa Kiingereza”.

Soma zaidi...

Ulaya Inaendelea Kuunga Mkono Mauaji ya Halaiki mjini Gaza

Licha ya kauli mbiu tupu kuhusu kuitambua dola ya Palestina, Ulaya inaendelea kusafirisha silaha kwa umbile hilo la Kizayuni. Habari zilizovuja zilizopatikana na gazeti la Denmark zinafichua kuwa hivi majuzi mwezi wa Agosti, serikali ya Denmark ilituma vifaa vya silaha kwa ndege zilizotumiwa kuua watoto mjini Gaza.

Soma zaidi...

Mpango wa Trump wa Gaza ni Mpango Muovu wa Usaliti Unaolenga Kuangamiza Kadhia ya Palestina

Rais wa Marekani Donald Trump alitangaza kuwa Waziri Mkuu wa “Israel” Benjamin Netanyahu amekubali mpango wenye vipengee 20 ambao ungemaliza vita katika Ukanda wa Gaza. Trump na Netanyahu walifanya mkutano wa pamoja na waandishi wa habari baada ya mkutano wao jijini Washington. Trump alisema kuwa amani ya Gaza ilikuwa karibu sana kupatikana na kumshukuru Netanyahu kwa kuidhinisha mpango huo (DW Turkish 29.09.2025).

Soma zaidi...

Hotuba ya Rais Erdoğan ya Umoja wa Mataifa: Maneno Yaso Vitendo

Rais Recep Tayyip Erdoğan, katika hotuba yake kwa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa, alielezea kile kinachotokea Gaza kama “mauaji ya halaiki,” alisisitiza kuwa Israel inaua watoto kila siku, na kutoa wito kwa jumuiya ya kimataifa kuchukua hatua. Akisambaza picha kutoka Gaza, Rais Erdoğan alisema: “Hakuna vita mjini Gaza ... Huu ni uvamizi, uhamishaji, ufukuzaji, mauaji ya halaiki na uharibifu wa maisha.”

Soma zaidi...

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu