Alhamisi, 03 Dhu al-Qi'dah 1446 | 2025/05/01
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

Amani ya Kudumu Inaweza Tu Kupatikana huko Balochistan kupitia Kuung'oa Mfumo wa Wakoloni na Kusimamisha Khilafah Rashida

Machafuko katika jimbo la Balochistan si jambo geni. Yamedumu tangu uhuru wa Pakistan kutoka kwa Raj wa Uingereza. Watu wa Balochistan wana malalamiko ya kina, yaliyoachwa bila kutatuliwa na utawala wa kikoloni wa Uingereza na watawala ambao ni vibaraka wa wakoloni wa Magharibi. Mfumo wa wakoloni ulipangwa kuwatiisha Waislamu, badala ya kuangalia mambo yao. Unawanyima haki na unadumisha udhibiti kupitia nguvu za kijeshi.

Soma zaidi...

Msimamo Unaokinzana wa Indonesia juu ya umbile la Kiyahudi: Maneno Makali Lakini Ingali Inadumisha Mahusiano Mazuri

Indonesia imeyataka mataifa ya Kiislamu na Kiarabu kukata uhusiano wa kibiashara na kiuchumi na ‘Israel’ ili kukomesha ghasia mjini Gaza. Katika kikao cha Riyadh cha Jumuiya ya Nchi za Kiarabu na OIC, Makamu wa Waziri wa Mambo ya Nje Anis Matta alisisitiza ulazima wa kukata vitega uchumi vinavyohusiana na taasisi za Kizayuni na kuimarisha biashara ndani ya uchumi wa nchi za Kiislamu. Licha ya wito huu, biashara ya Indonesia na ‘Israel’ ilifikia dolari milioni 173 kuanzia Januari hadi Septemba 2024, ongezeko la 24.6% kutoka mwaka uliopita.

Soma zaidi...

Mtazamo kwa Ghasia za Baada ya Uchaguzi wa Msumbiji

Kwa mujibu wa Kituo cha Demokrasia na Haki za Binadamu cha Msumbiji na shirika la Reuters, kufikia tarehe 8/11/2024, jumla ya vifo 34 viliripotiwa huku vyanzo vyengine vikisema kuwa waliouawa ni zaidi ya 50, kutokana na ghasia za baada ya uchaguzi. kutangazwa kwa mgombea wa chama tawala cha Front for Liberation of Msumbiji (Frelimo), Daniel Chapo kuwa mshindi wa uchaguzi wa rais uliofanyika mnamo Oktoba 24 mwaka huu ambapo wapinzani walidai kuwa matokeo ya kura yaliibwa.

Soma zaidi...

Mauaji ya Halaiki mjini Gaza Hayatamalizika hadi sisi kama Waislamu Tumalize Utegemezi wetu kwa Demokrasia

Uchaguzi wa Marekani wa 2024 ulifanyika mnamo tarehe 5 Novemba huku Donald Trump, akipata ushindi mkubwa dhidi ya Kamala Harris. Waislamu wengi nchini Marekani, kwa mara nyengine tena walishiriki katika chaguzi hizi za kidemokrasia kwa matumaini kwamba kura yao ingesaidia kumaliza mauaji ya halaiki huko Gaza. Wengine walimuunga mkono Trump, ima wakiamini katika ahadi yake kwamba angeleta amani katika eneo hilo, au “kumuadhibu” Harris na utawala wa Biden kwa kuendelea kuunga mkono na kufadhili umbile la mauaji ya halaiki la Kizayuni. Wengine walimuidhinisha Harris, wakiamini kwamba yeye ndiye ‘la hafifu ya madhara mawili’ na njia bora kwa wapinzani wa vita vya Gaza kuendeleza ajenda zao. Wengine walipiga kura zao kwa mwakilishi wa Green Party, Jill Stein na mgombea wa People's Party Cornel West, kutokana na msimamo wao thabiti wa kupinga vita na kuahidi kukomesha mauaji ya halaiki.

Soma zaidi...

Mvunjifu na Mdhamini Pamoja: Serikali Yalenga Nini?

Iwe ni serikali au upinzani, miundo kama hii ya kisiasa haiwezi kukwepa kuwa wafungwa wa ukoloni, kama vile mtazamo wao wakati wa Mapinduzi ya Kiarabu na Kimbunga cha Al-Aqsa kinachoendelea, wanatumikia maslahi ya makafiri wakoloni ili tu kudumisha viti vyao. Madhumuni yao pekee ni kuzuia ummah wa Kiislamu kuelekea katika Khilafah na kujaribu kuzalisha miungano bandia, dhidi ya umoja halisi wa Khilafah.

Soma zaidi...

Sio kila chenye Kumetameta ni Dhahabu

Tawala dhalilifu za vibaraka zimesisitiza kuthibitisha, kwa yakini, kwamba ni tawala ambazo si za Ummah, huku Ummah ukiwa si sehemu yake. Katika kupambana waziwazi na hisia za Waislamu, zilikimbilia kumpongeza Rais Trump wa Marekani baada ya kutangazwa ushindi wake katika uchaguzi huo. Zilikimbilia kumpa majukumu yao ya utiifu na uaminifu, na kusahau kuuawa kwa watoto wa Waislamu huko Gaza, Lebanon na kwengineko katika vita vya wazi vinavyoongozwa na Amerika, kwa kutumia mali zake, huku wakisahau kauli za bwege huyu katika kuunga mkono kwake wazi kusiko na mipaka kwa Mayahudi. Je, inawezekana kutarajia kwamba zabibu zitatoka kwenye miiba?!

Soma zaidi...

Mirziyoyev Afufua “orodha nyeusi” za Waislamu

Mwanablogu mashuhuri wa Uzbekistan, Mirrahmat Muminov, alitangaza kwamba ana habari kuhusu kuanzishwa kwa udhibiti kamili na ufuatiliaji wa waumini sugu wa misikiti nchini. Aliripoti haya kwenye ukurasa wake wa Facebook: Kamati ya Masuala ya Kidini na Bodi ya Waislamu ya Uzbekistan, pamoja na Wizara ya Mambo ya Ndani, waliagizwa kuandaa orodha za waumini sugu wa kudumu wa misikiti. Uamuzi huu unahusiana na kukua kwa itikadi kali za kidini na umaarufu wa fikra za kidini miongoni mwa vijana.

Soma zaidi...

Kuchaguliwa tena kwa Trump: Mporomoko wa Demokrasia uso Kifani

Mnamo Novemba 6, 2024, ilithibitishwa kuwa Donald Trump, mhalifu aliyepatikana na hatia, alishinda tena uchaguzi wa rais nchini Marekani. Tukio hili sio tu suala la mtu wa kuchukiza, bali ni dalili ya uozo wa kina katika mfumo wa kidemokrasia wa Magharibi. Huku ulimwengu ukitazama, kuchaguliwa tena kwa Trump kunafichua udanganyifu mwingi ambao demokrasia ya Magharibi imeunadi kwa ulimwengu kwa miaka mingi.

Soma zaidi...

Kupigana kwa Heshima, au Kutotenda kwa Udhalilifu?!

Mnamo tarehe 30 Oktoba 2024, Naim Qassem alisema katika hotuba yake ya kwanza ya video baada ya kuapishwa kama Katibu Mkuu wa kundi linaloungwa mkono na Iran, “Tofauti kati yetu na ‘Israel’ ni kwamba tunapigana kwa heshima, tukilenga kambi, jeshi, vifaru na askari, huku wao wanaua raia na watu wasio na silaha, na kuangamiza watu na majengo ya miundombinu.”

Soma zaidi...

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu