Jumatano, 19 Safar 1447 | 2025/08/13
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

Sio kila chenye Kumetameta ni Dhahabu

Tawala dhalilifu za vibaraka zimesisitiza kuthibitisha, kwa yakini, kwamba ni tawala ambazo si za Ummah, huku Ummah ukiwa si sehemu yake. Katika kupambana waziwazi na hisia za Waislamu, zilikimbilia kumpongeza Rais Trump wa Marekani baada ya kutangazwa ushindi wake katika uchaguzi huo. Zilikimbilia kumpa majukumu yao ya utiifu na uaminifu, na kusahau kuuawa kwa watoto wa Waislamu huko Gaza, Lebanon na kwengineko katika vita vya wazi vinavyoongozwa na Amerika, kwa kutumia mali zake, huku wakisahau kauli za bwege huyu katika kuunga mkono kwake wazi kusiko na mipaka kwa Mayahudi. Je, inawezekana kutarajia kwamba zabibu zitatoka kwenye miiba?!

Soma zaidi...

Mirziyoyev Afufua “orodha nyeusi” za Waislamu

Mwanablogu mashuhuri wa Uzbekistan, Mirrahmat Muminov, alitangaza kwamba ana habari kuhusu kuanzishwa kwa udhibiti kamili na ufuatiliaji wa waumini sugu wa misikiti nchini. Aliripoti haya kwenye ukurasa wake wa Facebook: Kamati ya Masuala ya Kidini na Bodi ya Waislamu ya Uzbekistan, pamoja na Wizara ya Mambo ya Ndani, waliagizwa kuandaa orodha za waumini sugu wa kudumu wa misikiti. Uamuzi huu unahusiana na kukua kwa itikadi kali za kidini na umaarufu wa fikra za kidini miongoni mwa vijana.

Soma zaidi...

Kuchaguliwa tena kwa Trump: Mporomoko wa Demokrasia uso Kifani

Mnamo Novemba 6, 2024, ilithibitishwa kuwa Donald Trump, mhalifu aliyepatikana na hatia, alishinda tena uchaguzi wa rais nchini Marekani. Tukio hili sio tu suala la mtu wa kuchukiza, bali ni dalili ya uozo wa kina katika mfumo wa kidemokrasia wa Magharibi. Huku ulimwengu ukitazama, kuchaguliwa tena kwa Trump kunafichua udanganyifu mwingi ambao demokrasia ya Magharibi imeunadi kwa ulimwengu kwa miaka mingi.

Soma zaidi...

Kupigana kwa Heshima, au Kutotenda kwa Udhalilifu?!

Mnamo tarehe 30 Oktoba 2024, Naim Qassem alisema katika hotuba yake ya kwanza ya video baada ya kuapishwa kama Katibu Mkuu wa kundi linaloungwa mkono na Iran, “Tofauti kati yetu na ‘Israel’ ni kwamba tunapigana kwa heshima, tukilenga kambi, jeshi, vifaru na askari, huku wao wanaua raia na watu wasio na silaha, na kuangamiza watu na majengo ya miundombinu.”

Soma zaidi...

Maldives Yatumbukia Zaidi ndani ya Mgogoro wa Kifedha, huku Ikiyumba Kati ya China na India

Suluhisho la migogoro ya kiuchumi ya Maldives haliko katika kuyumba kati ya dola mbili zinazopiga vita Waislamu na Uislamu. Mfumo wa sasa wa ulimwengu unaleta madhara kwa Waislamu, kiuchumi na kijeshi. Unafanya dola za Waislamu kuwa uwanja wa kunyonywa na wakoloni, na washirika wao, India na umbile ya Kiyahudi. Suluhisho kwa Maldives ni kuwa sehemu ya Khilafah tukufu, kama ilivyokuwa huko nyuma.

Soma zaidi...

Wale Waliotazama Moto wa Gaza Wamehukumiwa Udhalilifu!

Ikiwa Bw. Erdogan angekuwa mkweli, angejibu uwepo huu wa kigaidi kwa nguvu za kijeshi, mateso haya yasingetokea Gaza. Ikiwa kweli wewe ni mkweli, hutanyamaza tena kuhusu mauaji yanayofanywa na magenge ya Kiyahudi huko Gaza na Lebanon, bali utahamasisha jeshi. Kwa hivyo, kanda na jiografia iliyo chini ya moto itakomesha ukatili huu, na utafanya kile kinachohitajika hata ikiwa kimechelewa.

Soma zaidi...

Chini ya Udhamini na Usimamizi wa Marekani: Iran na Umbile la Kiyahudi Zimeungana katika Kuangamiza Ulimwengu wa Kiislamu

Usimamizi na uratibu wa Marekani wa dhana inayoendelea kati ya Iran na umbile la Kiyahudi kuhusu mashambulizi ya kiusanii, ambayo haidhuru pande zote mbili, inakusudiwa kutoa muda zaidi kwa umbile la Kiyahudi kuua vikosi vya upinzani vilivyobaki mjini Gaza na Lebanon. Hii ni pamoja na kuiingiza Iran katika hali ya kisiasa katika Mashariki ya Kati, na kuitumia, pamoja na umbile la Kiyahudi kusimamia eneo hilo kwa njia inayohudumia maslahi ya Amerika pekee.

Soma zaidi...

Sakata ya Genge la Watoto Wachanga nchini Uturuki

Maelezo ya kutisha ya sakata ya “genge la watoto wachanga” nchini Uturuki yametikisa taifa. Watu, wakiwemo madaktari, wauguzi na wafanyikazi wa hospitali, walifanya njama ya uhamishaji watoto wachanga wagonjwa hadi hospitali za kibinafsi kwa pato la kifedha. Angalau watoto 12 walipoteza maisha kutokana na vitendo vya genge hilo, kwani utunzaji muhimu ulipuuzwa kwa ajili ya faida. Kutokana na uhalifu huu wa kutisha uliopangwa, washukiwa 22 kati ya 47 walikamatwa, hospitali 10 za kibinafsi jijini Istanbul zilifungwa, na katika siku zilizofuata, ilifichuliwa kuwa uhalifu huu ulifanyika katika majimbo mengine manne.

Soma zaidi...

Firauni Rahmon Awawinda Vijana wa Kiislamu nchini Tajikistan

Majaribio ya dhalimu Rahmon ya kusitisha mwamko wa Uislamu miongoni mwa watu yanafanana na wazimu wa Firauni wa Misri. Baada ya kujua juu ya utabiri kwamba maangamivu yake yangetoka kwa mwanamume aliyezaliwa kati ya wana wa Israeli, Firauni, akiwa ameshikwa na hofu, aliamuru wavulana wote wanaozaliwa wauawe. Askari wake waliwaua kikatili watoto wachanga wa kiume, bila kumsaza yeyote.

Soma zaidi...

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu