Sio kila chenye Kumetameta ni Dhahabu
- Imepeperushwa katika Habari na Maoni
- Kuwa wa kwanza kutoa maoni!
- |
Tawala dhalilifu za vibaraka zimesisitiza kuthibitisha, kwa yakini, kwamba ni tawala ambazo si za Ummah, huku Ummah ukiwa si sehemu yake. Katika kupambana waziwazi na hisia za Waislamu, zilikimbilia kumpongeza Rais Trump wa Marekani baada ya kutangazwa ushindi wake katika uchaguzi huo. Zilikimbilia kumpa majukumu yao ya utiifu na uaminifu, na kusahau kuuawa kwa watoto wa Waislamu huko Gaza, Lebanon na kwengineko katika vita vya wazi vinavyoongozwa na Amerika, kwa kutumia mali zake, huku wakisahau kauli za bwege huyu katika kuunga mkono kwake wazi kusiko na mipaka kwa Mayahudi. Je, inawezekana kutarajia kwamba zabibu zitatoka kwenye miiba?!