Amerika ya Trump Itashindwa Kufanya Kile ambacho Kikongwe Biden Hakuweza Kukifanya
- Imepeperushwa katika Habari na Maoni
- Kuwa wa kwanza kutoa maoni!
- |
“Rais mteule wa Marekani Donald Trump ametoa kauli kadhaa zenye utata ambazo zinaakisi waziwazi ukubwa wa tofauti katika sera za ndani na nje za Marekani na za Rais anayeondoka wa chama cha Democrat Joe Biden. Kwa upande wa sera ya mambo ya nje, Trump alisema atakomesha kile alichokitaja kuwa machafuko katika Mashariki ya Kati, kusitisha vita nchini Ukraine, na kuzuia kuzuka kwa Vita vya Tatu vya Dunia, bila kueleza jinsi atakavyofanya haya yote...



