Wanajificha Chini ya Jiwe Gani na Katika Sayari Gani Wanajeshi na Majenerali wa Majeshi ya Waislamu Wakati Hata Askari wa Jeshi la Adui Yetu Hawawezi Kukaa Kimya?!
- Imepeperushwa katika Habari na Maoni
- Kuwa wa kwanza kutoa maoni!
- |
Katika kupinga mauaji ya halaiki yanayoendelea kufanywa juu ya watu wa Gaza, mwanajeshi wa Marekani anayeitwa Aaron Bushnell alijitolea maisha yake mbele ya ubalozi wa ‘Israel’ kwa kujichoma moto. Alisema alipokuwa akielekea kifo chake kwamba hawezi kushiriki tena katika mauaji ya watu wasio na hatia huko Gaza, na maneno yake ya mwisho yalikuwa ‘Iacheni Huru Palestina’.