Mtazamo kwa Ghasia za Baada ya Uchaguzi wa Msumbiji
- Imepeperushwa katika Habari na Maoni
- Kuwa wa kwanza kutoa maoni!
- |
Kwa mujibu wa Kituo cha Demokrasia na Haki za Binadamu cha Msumbiji na shirika la Reuters, kufikia tarehe 8/11/2024, jumla ya vifo 34 viliripotiwa huku vyanzo vyengine vikisema kuwa waliouawa ni zaidi ya 50, kutokana na ghasia za baada ya uchaguzi. kutangazwa kwa mgombea wa chama tawala cha Front for Liberation of Msumbiji (Frelimo), Daniel Chapo kuwa mshindi wa uchaguzi wa rais uliofanyika mnamo Oktoba 24 mwaka huu ambapo wapinzani walidai kuwa matokeo ya kura yaliibwa.



