Jumanne, 28 Dhu al-Hijjah 1446 | 2025/06/24
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

Afisi ya NATO nchini Jordan: Kujisalimisha kwa Nchi na Kuahidi Kutumikia Maslahi ya Kikoloni ya Maadui wa Ummah

Mnamo siku ya Alhamisi, 12 Juni 2025, Jordan na Shirika la Mkataba wa Atlantiki ya Kaskazini (NATO) walitia saini makubaliano jijini Brussels ili kuwa mwenyeji wa afisi ya mawasiliano ya kidiplomasia ya muungano huo katika mji mkuu, Amman. Makubaliano hayo yalitiwa saini kwa niaba ya Jordan na Balozi Yusuf Bataineh, balozi aliyeidhinishwa katika NATO, na kwa niaba ya muungano huo na Javier Colomina, Mwakilishi Maalum wa NATO kwa jirani wa Kusini, ambaye alisifu uhusiano uliotukuka na Jordan na kuthamini ukaribishaji wa afisi ya Jordan na dori yake kuu katika kanda, akiizingatia kuwa mshirika wa kutegemewa kwa muungano huo katika nyanja tofauti tofauti.

Soma zaidi...

Kongamano la Amani ya Kiraia jijini Damascus Utangulizi wa Kuwaondoa Watiifu wa Serikali na Kuhalalisha Nembo za Ukandamizaji na Uhalifu

Mkutano na waandishi wa habari uliofanywa na Kamati ya Amani ya Kiraia katika jengo la Wizara ya Habari jijini Damascus mnamo Jumanne, Juni 10, 2025, chini ya uenyekiti wa mwanakamati Hassan Soufan, ulizua wimbi kubwa la hasira na chuki kubwa miongoni mwa Wasyria, hasa miongoni mwa familia za mashahidi na waliopotea, na watoto wa mapinduzi. Wengi waliona kauli za mkutano huo kama uchochezi kwa familia za wahasiriwa, kupuuza mihanga ya wanamapinduzi, kudharau damu ya mahsahidi, kukana ukweli usiopingika, na uhalalishaji wa wazi wa wahalifu wa kivita. Hafla hiyo ilionekana kama jaribio la kulalalisha mahusiano kwa nembo za utawala ulio ng’atuliwa chini ya mabango ya "amani ya raia," "kujenga taifa," na "kuzuia umwagaji damu."

Soma zaidi...

Pongeza kutoka kwa Hizb ut Tahrir / Wilayah Iraq kwa Sikukuu ya Idd al-Adha 1446 H

Afisi ya Habari ya Hizb ut Tahrir / Wilayah Iraq inatoa pongezi na baraka zake nyingi kwa Umma wa Kiislamu kwa mnasaba wa Idd al-Adha iliyobarikiwa. Hasa tunatoa salamu hizi kwa wabebaji da’wah, na kwa mwanachuoni mkubwa, Amiri wa Hizb utTahrir, Ata Bin Khalil Abu Al-Rashtah Mwenyezi Mungu amlinde na amhifadhi na ampe ushindi na tamkini kupitia mikono yake.

Soma zaidi...

Hizb ut Tahrir / Wilayah Yemen Inawapongeza Watu wa Imani na Hekima na Umma wa Kiislamu kwa Sikukuu ya Idd al-Adha iliyobarikiwa

Hizb ut Tahrir / Wilayah Yemen inatoa pongezi zake za dhati na baraka zenye thamani kubwa zaidi kwa watu wa imani na hekima, na kwa Amiri wa Hizb, mwanachuoni mkubwa Ata Bin Khalil Abu Al-Rashtah, na kwa wanachama wote wa Hizb, na kwa Ummah mzima wa Kiislamu kwa sikukuu ya Idd al-Adha iliyobarikiwa mwaka huu wa 1446 H. Mwenyezi Mungu airudishe kwao, juu yetu, na juu ya ulimwengu wote kwa kheri, baraka, na furaha.

Soma zaidi...

Pongezi kwa Idd Al-Adha Iliyobarikiwa 1446 H

Hizb ut Tahrir inatoa pongezi na baraka nyingi zaidi kwa Umma wetu mpendwa wa Kiislamu, wenye subira na wenye kukubali malipo licha ya maafa na majanga yote unaopitia, maafa na majanga ambayo ni mzigo mzito hata kwa kundi lililo imara zaidi la wanadamu, hususan watu wetu wenye subira mjini Gaza na katika Ardhi Iliyobarikiwa ya Palestina, katika Sikukuu ya Idd ul-Adha. Tunamuomba Mwenyezi Mungu azijaalie siku za Idd hii kuwa ni utulivu katika nyoyo zao na wanyanyuliwe daraja mbele ya Mola wa walimwengu wote.

Soma zaidi...

Hizb ut Tahrir Ndio Inayofanya Kazi Ipasavyo Kusimamisha Khilafah Basi Acheni Kuvuruga Ulinganizi Wake na Kuwakamata Wanachama Wake

Tangu kuanzishwa kwake kama chama cha kisiasa chenye msingi wa Uislamu mwaka 1953, Hizb ut Tahrir imefanya kazi ya kurudisha mfumo kamili wa Kiislamu wa maisha ya Kiislamu kupitia kusimamisha dola ya Kiislamu, ambayo dola yake ya kwanza ilianzishwa na Mtume Muhammad (saw) mjini Madina. Ingawa inafuata njia ya Mtume (saw) ya kusimamisha dola hii, haijishughulishi na kitendo chochote cha kinguvu au kile kinachoitwa vurugu katika kufanya hivyo.

Soma zaidi...

Kutafakari juu ya Gaza, Mfano wa Ibrahim (as) na Wito wa Haraka wa Nusrah Leo

Umma unapoingia katika siku tukufu za Tashriq, katikati ya ibada za Hijja, tunakumbushwa kwamba nguzo hii adhimu ya Uislamu ni safari ya kiroho, faradhi wa kiwahyi inayoonyesha kujitolea kipekee kwa ajili ya Mwenyezi Mungu (swt). Ibada za Hijja zinajumuisha mila ya Nabii mtukufu Ibrahim (as), mke wake mtukufu Hajar (as), na mwanawe Ismail (as), familia ambayo mitihani yao iliufundisha Ummah asili ya tawakkul, imani isiyoyumba kwa Mwenyezi Mungu (swt), na kujisalimisha kikamilifu kwa amri Yake tukufu, hata pale amri hiyo inapopingana na mantiki ya kidunia.

Soma zaidi...

Pongezi kutoka Hizb ut Tahrir/ Wilayah ya Sudan Kwa Mnasaba wa Idd Al-Adha 1446 H

Sisi, katika Hizb ut Tahrir / Wilayah ya Sudan, tunafuraha kuwapongeza watu wetu nchini Sudan na Umma wote wa Kiislamu kwa mnasaba wa Idd Al-Adha. Mwenyezi Mungu airudishe kwetu, tukiwa Ummah ulioungana chini ya bendera ya Al-Uqab, bendera ya Mtume wa Mwenyezi Mungu (saw), chini ya kivuli cha Khilafah Rashida kwa njia ya Utume.

Soma zaidi...

Kuna Uungwana kutoka Ng'ambo ya Bahari... Uko wapi Uungwana wa Jeshi la Misri?!

Katika wakati ambapo mauaji dhidi ya watu wa Gaza yamezidi, na ardhi kuungua chini ya miguu ya wanyonge, vyombo vya habari vya Marekani vimeandika kichwa cha kikuu habari kuhusu kijana Muislamu kutoka Misri aitwaye Mohammed Sabry Soliman, ambaye alituhumiwa kwa kurusha vinywaji vya Molotov kwenye maandamano ya kuunga mkono umbile la Kiyahudi nchini Amerika, akiimba "Uhuru kwa Palestina." Wakati vyombo vya habari vinajadili tukio hili, kiini cha tukio hili hakiwezi kupuuzwa: kijana Muislamu, aliyehama kutoka ng'ambo ya bahari, akisukumwa na maumivu ya moyo wake na maumivu ya Ummah wake, kueleza kukataa kwake kimya cha kimataifa na kufeli kwa Waarabu kushughulikia hali inayoendelea mjini Gaza.

Soma zaidi...

Hizb ut Tahrir / Wilayah Sudan Yahuisha Ibada ya Takbira Katika Mwezi wa Dhul-Hijjah kwa Matembezi ya Kishindo katika Soko Kuu la Port Sudan

Baada ya swala ya Alasiri mnamo siku ya Jumatatu, tarehe 6 Dhul-Hijjah 1446 H, sawia na tarehe 2 Juni 2025 M, Mashababu wa Hizb ut Tahrir / Wilayah Sudan walihuisha ibada ya takbira katika mwezi wa Dhul-Hijjah. Ustadh Muhammad Jami’ (Abu Ayman), Msaidizi wa Msemaji wa Hizb ut Tahrir katika Wilayah ya Sudan, alihutubia waumini katika Msikiti wa Ibn Mas’ud katika soko kuu la Port Sudan baada ya Swalah ya Alasiri, akiwakumbusha juu ya ubora wa siku hizi zilizobarikiwa za Dhul-Hijjah, na jinsi Maswahaba – Mwenyezi Mungu awe radhi nao – walivyozitukuza siku hizi kwa takbira na tahleel. Kisha akaanza kupiga takbira, ikifuatiwa na dua. Baadaye wote wakatoka kwa matembezi ya kishindo wakiwa wamebeba Rayah (bendera) ya Mtume wa Mwenyezi Mungu (saw), na alama kubwa isemayo: "Kuhuisha Ibada ya Takbira katika Mwezi wa Dhul-Hijjah."

Soma zaidi...

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu