Afisi ya NATO nchini Jordan: Kujisalimisha kwa Nchi na Kuahidi Kutumikia Maslahi ya Kikoloni ya Maadui wa Ummah
- Imepeperushwa katika Jordan
- Kuwa wa kwanza kutoa maoni!
- |
Mnamo siku ya Alhamisi, 12 Juni 2025, Jordan na Shirika la Mkataba wa Atlantiki ya Kaskazini (NATO) walitia saini makubaliano jijini Brussels ili kuwa mwenyeji wa afisi ya mawasiliano ya kidiplomasia ya muungano huo katika mji mkuu, Amman. Makubaliano hayo yalitiwa saini kwa niaba ya Jordan na Balozi Yusuf Bataineh, balozi aliyeidhinishwa katika NATO, na kwa niaba ya muungano huo na Javier Colomina, Mwakilishi Maalum wa NATO kwa jirani wa Kusini, ambaye alisifu uhusiano uliotukuka na Jordan na kuthamini ukaribishaji wa afisi ya Jordan na dori yake kuu katika kanda, akiizingatia kuwa mshirika wa kutegemewa kwa muungano huo katika nyanja tofauti tofauti.