Alhamisi, 05 Rajab 1447 | 2025/12/25
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

Moyo wa Hebron na Msikiti wa Ibrahimi Wafanywa Kuwa wa Kiyahudi kwa Kufuata Hatua Zile Zile kama Ulivyofanywa kuwa wa Kiyahudi Msikiti wa Al-Aqsa

Baada ya umbile la Kiyahudi kuamua kuhamisha mamlaka ya kiidara ya Msikiti wa Ibrahimi kutoka Manispaa ya Hebron hadi “Baraza la Kidini la Kiyahudi huko Kiryat Arba,” na baada ya umbile hilo kukataa pingamizi iliyowasilishwa na Manispaa ya Hebron kuhusu uamuzi huu, pamoja na uamuzi uliofuata wa kugeuza ua wa ndani wa Msikiti wa Ibrahimi kuwa uwanja wa umma, na pamoja na vyama vya Kiyahudi vinavyofanya kazi ya kununua nyumba katika mji wa Hebron (al-Khalil) - moyo wa Mji wa Hebron, huku Msikiti wa Ibrahimi ukiwa kiini chake, unafanywa kuwa wa Kiyahudi waziwazi mbele ya ulimwengu na mbele ya Umma wa Kiislamu, kama vile eneo la Safari ya Usiku ya Mtume wake (saw) na viunga vyake linavyofanywa kuwa la Kiyahudi.

Soma zaidi...

Kukamatwa Kupya kwa Wanachama wa Hizb ut Tahrir nchini Yemen na Mahouthi Je, kauli mbiu “Kifo kwa Amerika” inawezaje kuishi sambamba na Kutetea Mpango wa Trump kuhusu Gaza?!

Mnamo Alhamisi, 27/11/2025, vikosi vya usalama vya Mahouthi vilimkamata Saddam Ali Qa’id al-Mukirdi, mwenye umri wa miaka 28, kutoka wilaya ya Ṣabr al-Mawadim katika Mkoa wa Taiz ulio chini ya udhibiti wa Mahouthi katikati mwa Yemen. Kukamatwa huku ni kwa pili, kufuatia kukamatwa kwa ndugu Osama na Mohammad Mas’ad Al-Wurafi katika Mkoa wa Ibb mnamo 21/11/2025, baada ya kugawanya toleo lenye kichwa: “Trump Awaongoza Wafuasi Wake Miongoni mwa Watawala katika Ardhi za Waislamu kwenye Mpango wa Fedheha na Aibu, Wanaosujudu Vichwa Vyao Nyuma Yake kwa Kuiweka Gaza ya Hashim Chini ya Udhamini na Ukoloni.”

Soma zaidi...

Udhalimu wa Watawala Wakandamizaji Unaweza Kukomeshwa Tu Kupitia Mabadiliko Msingi

Tangu Jumamosi iliyopita, mkoa wa Erbil umekuwa ukishuhudia mvutano wa kiusalama kufuatia maandamano ya makabila ya Herki katika wilaya ya Khabat, yakikituhumu Chama cha Kidemokrasia kwa kukaidi ahadi zake za kuwapa viti vitatu bungeni kwa badali ya kabila hilo kuwapa kura zao katika uchaguzi. Maandamano hayo kisha yakageuka kuwa mapigano kati ya makabila ya Herki na vikosi vya usalama, na kusababisha vifo na majeraha. Katika tukio muhimu, kabila hilo lilitangaza uhamasishaji wa jumla huko Erbil, na waandamanaji wakachoma makao makuu ya Chama cha Kidemokrasia cha Kurdistan katika wilaya hiyo leo, Jumatatu.

Soma zaidi...

Vikosi vya Pakistan Lazima Vitumwe Kuikomboa Ardhi Iliyobarikiwa ya Palestina, Sio Kutimiza Ndoto za Adui wa Mwenyezi Mungu (swt), Trump, na Mayahudi!

Kutumwa kwa vikosi vya jeshi la Pakistani Gaza kuwanusuru watu wake na kupigana na Mayahudi ambao wameendelea na operesheni ya mauaji ya halaiki huko, tangu tarehe 7 Oktoba 2023 hakukujadiliwa kamwe, kwa kisingizio kwamba Gaza iko mbali, na kwamba wajibu wa Sharia wa kuinusuru unawaangukia wale walio karibu zaidi. Lakini mara tu bwana wa serikali ya Pakistan na adui wa Mwenyezi Mungu (swt), Trump, alipoamuru serikali hii kutuma vikosi ili kufikia ndoto zake mjini Gaza, ghafla Pakistan ikawa nchi jirani na Gaza, na vikosi vya jeshi la Pakistan vimewekwa tayari kufanya operesheni za kijeshi nje ya mipaka ya kitaifa ya Pakistan. Hivyo uongo wa serikali hii ulifichuliwa kuhusu kutoweza kwake kutuma vikosi vya jeshi kuwanusuru watu wetu mjini Gaza.

Soma zaidi...

Ujumbe kutoka Hizb ut Tahrir / Wilayah Sudan Wakutana na Mkuu wa Chama cha Wanasheria katika Jimbo la Bahari Nyekundu

Mnamo Jumatatu, 1 Disemba 2025, ujumbe kutoka Hizb ut Tahrir / Wilayah Sudan, ukiongozwa na Ustadh Nasser Ridha, Mwenyekiti wa Kamati Kuu ya Mawasiliano ya Hizb ut Tahrir katika Wilayah Sudan, akifuatana na Ustadh Abdullah Ismail, Mjumbe wa Kamati Kuu ya Mawasiliano ya Hizb ut Tahrir katika Wilayah Sudan, walimtembelea Dkt. Imad al-Din Muhammad Hamdallah, mkuu wa Chama cha Wanasheria katika Jimbo la Bahari Nyekundu, afisini kwake Port Sudan.

Soma zaidi...

Kauli za Patriarch Bechara Al-Rahi Kuhusu Wakristo katika Eneo Hili Mshikamano wa Kudumu kwa Fahamu ya Marekani na Kimagharibi ya “Walio wachache”, iliyo ngeni kwa Watu wa Eneo Hili na Historia Yao!

Katika mahojiano yake na chaneli ya Lebanon Al-Jadeed katika kipindi cha “Huyu ni Mimi” na mwandishi wa habari Samar Abu Khaleel, kauli za Patriarch Bechara Al-Rahi zinaambatana na ziara ya Papa Leo XIV katika eneo hili, ikiwa ni pamoja na Lebanon, hasa kuhusu suala la kubadilisha utawala wa Syria na kauli yake: “Wakristo wanaondoka Syria leo kwa sababu dola iliyopo ni dola ya Kiislamu! Ingawa haikuwa hivyo wakati wa utawala uliopita...” Na msimamo huu ni uthibitisho wa msimamo uliopita wa Patriarch mwenyewe; ambapo alisema mwaka wa 2011 wakati wa ziara yake nchini Ufaransa chini ya Sarkozy: “Kukiri kwamba makosa na ukiukwaji wa sheria uliotokea nchini Syria hakubatilishi ukweli kwamba Rais Bashar Al-Assad alikuwa ameanza mageuzi, na angepaswa kupewa nafasi”!

Soma zaidi...

Kampeni ya Umbile la Kizayuni katika Ukingo wa Kaskazini Magharibi ni Sehemu ya Mpango wake wa Kuimarisha Makaazi na Kuimarisha Udhibiti wake katika Eneo Hilo. Je, Hakuna Kiongozi Anayeongozwa na Mungu wa Kuikomboa Ardhi Iliyobarikiwa?!

Hawa hapa Mayahudi wakizidi kuwa wakali zaidi katika Ukingo wa Magharibi, wakitangaza “operesheni ya kijeshi” kaskazini mwake, wakibomoa nyumba na kuzigeuza zengine kuwa kambi za kijeshi, wakinyang'anya ardhi, wakikamata kundi la Wapalestina na kuua kundi jengine, wakiharibu mifereji ya maji na kung'oa miti, na operesheni yao ya kijeshi inaenea hadi sehemu iliyobaki ya Ukingo wa Magharibi, katikati yake na kusini yake, na hii inaendana na kile walowezi hao wanachofanya, kwa kuzingatia kutolewa kwa sheria inayowaruhusu kupata mali katika Ukingo wa Magharibi, ambayo ilitanguliwa na kufutiliwa mbali kwa sheria ya kutengwa kaskazini yake.

Soma zaidi...

Mwaliko wa Kuhudhuria Muhadhara wa Kisiasa

Afisi ya Habari ya Hizb ut Tahrir katika Wilayah Sudan inafuraha kuwaalika wataalamu wa vyombo vya habari, wanasiasa, na wale wote wanaopenda masuala ya umma kuhudhuria na kushiriki katika muhadhara mpya ya Kikao cha Kisiasa, ambao utawasilishwa na Ustadh Ibrahim Mushrif, mwanachama wa Afisi ya Habari ya Hizb ut Tahrir katika Wilayah Sudan, wenye kichwa: Mzozo wa Kikoloni barani Afrika - Sudan kama Mfano

Soma zaidi...

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu