Jumanne, 28 Dhu al-Hijjah 1446 | 2025/06/24
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

Sheria ya Kimataifa ni Sheria ya Pori - Hairuhusiwi Kuiendea

Chini ya ufadhili wa Daniel Capoli, Mratibu wa Masuala ya Kibinadamu katika misheni ya Kamati ya Kimataifa ya Msalaba Mwekundu (ICRC) nchini Yemen, ICRC huko Sana'a ilipanga, mnamo Jumanne na Jumatano, 20-21/05/2025, kwa ushirikiano na Wizara ya Habari na Wizara ya Mambo ya Nje, kozi ya mafunzo katika Wizara ya Mambo ya Nje kwa wafanyikazi wa vyombo vya habari na taasisi ya waandishi wa habari. Kozi hiyo ilishughulikia sheria za kimataifa, misingi na malengo yake, na istilahi zinazohusiana na sheria za kimataifa za kibinadamu, haswa katika suala la haki za binadamu katika ulinzi na maisha yenye staha, kuzuia ghasia, na kukidhi mahitaji ya vikundi vilivyo hatarini zaidi vinavyofinikwa na ulinzi wake, na vile vile kulinda raia dhidi ya athari za uhasama na kuharamisha mateso yasiyo na haja au madhara kupita kiasi.

Soma zaidi...

Ni Nani atakayewatetea Wanawake wa Sudan na Darfur?

Shirika la Madaktari Wasio na Mipaka (Médecins Sans Frontières) limeonya kuwa wanawake na wasichana katika jimbo la Darfur nchini Sudan wako katika hatari ya karibu kila mara ya unyanyasaji wa kijinsia. Mizani halisi ya mgogoro huu inasalia kuwa vigumu kubainisha, kwani huduma bado ni chache na watu wanakabiliwa na vikwazo katika kutafuta matibabu au kuzungumza kuhusu masaibu yao. Hata hivyo, manusura wote waliozungumza na timu za MSF huko Darfur na kuvuka mpaka nchini Chad walisimulia hadithi za kutisha za ghasia za kikatili na ubakaji. Huku wanaume na wavulana pia wakiwa hatarini, kiwango cha mateso kinapita maelezo.

Soma zaidi...

Ugonjwa wa Kipindupindu Waangamiza Sudan, na Serikali, kwa Uzembe wake, Inaomba Msaada kwa Mashirika ya Kimataifa!

Shirika la Afya Duniani (WHO) limefichua kuwa takriban wagonjwa 60,000 wa kipindupindu wamerekodiwa nchini Sudan, na kusababisha vifo vya zaidi ya 1640, likionya madhara ya kuporomoka kwa mfumo wa afya nchini humu. Ufichuzi huu unakuja wakati kipindupindu kikienea kwa kasi katika Jimbo la Khartoum, ambapo maambukizi mapya yanazidi 90% ya jumla ya nchi, haswa huko Karari, Omdurman, na Ombada. Mnamo Jumanne, 27/5/2025, Wizara ya Afya ya Sudan ilitangaza kurekodi kesi 2729, pamoja na vifo 172, katika wiki moja. Waziri wa Afya wa Sudan Dkt. Haitham Mohamed Ibrahim alisema kuwa kuenea kwa kipindupindu jijini Khartoum kunatokana na kuzorota kwa hali ya mazingira na matatizo ya vyanzo vya maji ya kunywa. Wakati huo huo, Waziri Mkuu mpya Kamil Idriss anatoa wito kwa WHO, huku ripoti za vyombo vya habari zikisema kuwa anawasiliana na Mkurugenzi Mkuu wa WHO Tedros Adhanom ili kujadili kusaidia juhudi za kudhibiti kipindupindu nchini humu.

Soma zaidi...

Katikati ya Tabasamu za Idd na Machozi ya Gaza: Wito kwa Maafisa na Wanajeshi

Huku Waislamu wakijiandaa kukaribisha Idd al-Adha na kusherehekea pamoja na watoto wao na wenza wao katika siku hizi za sherehe, tunaelekeza ujumbe huu makhsusi kwa wanajeshi na maafisa wanyoofu wa jeshi la nyuklia la Pakistan, na majeshi mengine ya Ummah kwa jumla. Tunawakumbusha katika siku hizi kwamba wamewatelekeza watu wao wenyewe, wanawake, watoto, wazee, na wanaume katika Ardhi Iliyobarikiwa ya Palestina na Gaza, na hawakujitokeza kuwanusuru licha ya kuwa na uwezo wa kufanya hivyo.

Soma zaidi...

Kudumu kwa Mashirika ya Kifeministi na Mashoga hadi kufikia Hatua ya Kueneza Uchafu miongoni mwa Waumini ni Shambulizi la Dhahiri kwa Heshima ya Waislamu

Baada ya wasagaji wawili wanachama wa chama chenye uhusiano na Chuo Kikuu cha Marekani cha Beirut (AUBMC), chini ya kivuli na jina "Programu Oanishi ya Afya ya Jimai ya Wanawake (WISH) katika AUBMC," kutembelea shule ya upili ya wasichana jijini Tripoli, kwa uratibu wa Wizara ya Elimu; kisha kwa mbwembwe na bila aibu kuendekeza mambo machafu na kuonyesha picha na maudhui machafu kwa wanafunzi, wazazi wakasukumwa kuripoti tukio hilo kwa uongozi wa shule, ambao nao ulieleza kuwa wawili hao walikuja shuleni kwa amri ya Wizara ya Elimu na Elimu ya Juu!

Soma zaidi...

Serikali Yalazimisha Watu Kusherehekea Uhuru Unaodaiwa Sambamba na Mauaji ya Kikatili ya Halaiki!

Je, watu wa Jordan wanasherehekea uhuru unaodaiwa wakati jana, daktari Muislamu mwenye msimamo thabiti huko Gaza alipoteza watoto wake tisa wote kwa wakati mmoja, kutokana na kombora lililorushwa na ndege ya jeshi la mauaji ya halaiki nyumbani kwao, katika mandhari ya kinyama isiyo na kifani katika historia ya mwanadamu?

Soma zaidi...

Enyi Madhalimu! Fungueni Macho yenu!

Mnamo 19 Mei 2025, kesi ya wanachama 33 wa Hizb ut Tahrir, iliyodumu kwa karibu miezi minane, ilifikia kikomo. Kwa mujibu wa uamuzi wa mahakama, Musayev Shukrullah alihukumiwa kifungo cha miaka 17 katika jela maalum ya utawala; Selimov Dilshod alihukumiwa miaka 16 katika gereza maalum la utawala; Watu 20 walihukumiwa kifungo cha miaka 12 katika gereza maalum la utawala; Watu 8 walihukumiwa kifungo cha kati ya miaka 8 na 10, 4 kati yao katika hali maalum na wengine 4 katika hali kali; na watatu waliosalia walihukumiwa kati ya miaka 4 na 5 chini ya kifungo cha nyumbani.

Soma zaidi...

Serikali ya Muda Inatengwa na Wananchi kwa sababu ya Utiifu wao kwa Amerika; kwa upande mwingine, Msimamo wa Jeshi letu katika Kupendelea Ubwana wa Nchi kwenye Masuala ya 'Mkondo' na 'Bandari' ni Dhihirisho la Matarajio ya Watu

Huku serikali ya mpito, ikiwapuuza Waislamu wa Rohingya na ubwana wa nchi hiyo, inatamani sana kupeana 'mkondo' kwa maslahi ya kisiasa ya kijiografia ya Amerika na kukabidhi shughuli za 'New Mooring Container Terminal' kwa kampuni yenye ushawishi wa Marekani "DP World", msimamo mkali wa jeshi letu kuunga mkono ubwana wa nchi umesifiwa na watu wengi.

Soma zaidi...

Wananchi Wanataka Kupinduliwa kwa Serikali na Kusimamishwa kwa Utawala wa Kiislamu

Aden, mji mkuu wa muda wa serikali ya Yemen, umeshuhudia maandamano matatu ya wanawake na wanaume katika wiki mbili zilizopita. Kutokana na mateso yanayoendelea kwa wananchi, maandamano ya hasira yamefanyika mjini Aden, wakidai huduma za msingi na kukemea hali ngumu ya maisha na huduma duni. Maandamano haya yalijumuisha kauli mbiu dhidi ya muungano wa Waarabu, serikali ya Yemeni, na Baraza la Mpito, ambalo linadhibiti mji mkuu wa muda, Aden. Maandamano haya pia yalishuhudia milio ya risasi na kukamatwa kwa baadhi ya waandamanaji. Maandamano haya yalifanywa na wanawake na wanaume kwa siku tofauti. Kilichotia fora ni kuregea kauli mbiu isemayo “Wananchi wanataka kupinduliwa kwa serikali,” ambayo inatukumbusha Mapinduzi ya Kiarabu dhidi ya ukandamizaji na udhalimu.

Soma zaidi...

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu