Alhamisi, 08 Muharram 1447 | 2025/07/03
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

Hizb ut Tahrir / Kenya Iliandaa Msururu wa Amali katika Kumbukumbu ya Miaka 104 ya Kuvunjwa kwa Dola ya Khilafah

Kama sehemu ya kumbukumbu ya miaka 104 ya kuondolewa kwa Khilafah, Hizb ut Tahrir/Kenya ilifanya kampeni nchi nzima katika mwezi mtukufu wa Rajab 1446 H. Kampeni hii iliyoanza mwanzoni mwa mwezi mtukufu wa Rajab ilihusisha shughuli mbali mbali; Darsa, Semina na Visimamo. Hii ilikuwa ni kuukumbusha Ummah kuhusu hali yake ya kusikitisha ambayo umekuwa ukikabiliana nayo tangu kuondolewa kwa Khilafah mnamo tarehe 28 Rajab 1342 H sawia na tarehe 3 Machi 1924 M.

Soma zaidi...

Kuondolewa kwa Umbile la Kiyahudi ndio Suluhisho Pekee, Sio Suluhisho la Dola Mbili, Safadi

Waziri wa Mambo ya Nje wa Jordan Ayman Safadi, wakati wa kushiriki kwake katika Kongamano la Kiuchumi la Dunia huko Davos mnamo Jumatano, 22/01/2025, alisema kuwa mbinu yoyote ya baadaye ya Gaza lazima iegemee juu ya umoja wa Ukanda wa Gaza na Ukingo wa Magharibi na lengo la kufikia amani tu kwa msingi wa suluhisho la dola mbili. Alisema: “Katika muktadha wa suluhisho la kisiasa, serikali ya Palestina ndiyo pekee inayoshikilia uamuzi wa amani na vita, na hakupaswi kuwe na makundi ya kisilaha nje yake.”

Soma zaidi...

Pesa Zilizotumika Kutuua, Tunawezaje Kujitolea Kuzilipa?!

Katika mahojiano na gazeti la ‘Financial Times’, waziri wa mambo ya nje wa Syria alifichua ruwaza ya serikali mpya ya Syria baada ya Assad, akisisitiza kwamba nchi hiyo “haitaki kuishi kwa msaada,” na kwamba suluhisho liko katika kupunguza vikwazo vya Amerika na Ulaya. Aliongeza kuwa serikali haina mpango wa kusafirisha mapinduzi hayo ng’ambo au kuingilia masuala ya nchi nyingine. Hivyo, ikionyesha mabadiliko makubwa katika sera ya kigeni. Pia alionyesha katika mahojiano yayo hayo nia ya kubinafsisha bandari na viwanda vinavyomilikiwa na serikali na kuvutia uwekezaji wa kigeni, licha ya changamoto kubwa zinazoikabili Syria, ikiwemo madeni ya dolari bilioni 30 kwa washirika wa zamani wa Assad; Iran na Urusi.

Soma zaidi...

Machafuko na Ghasia nchini Sudan Kusini Zinasisitiza Haja ya Umma kuwa na Kiongozi mwenye Kuwalinda

Ulimwengu umefuatilia machafuko ya Juba, mji mkuu wa Sudan Kusini, ambayo yalilenga watu waliokimbia makaazi yao na wakaazi kutoka Sudan Kaskazini. Matukio haya yalichochewa na ripoti zinazowatuhumu wanajeshi wa Sudan kwa kuwaua watu kutoka Sudan Kusini huko Wad Madani baada ya jeshi kuutwaa tena mji huo. Kulingana na gazeti la ‘Sudan Tribune’, Wasudan watatu waliuawa mjini Juba, na wengine saba kujeruhiwa.

Soma zaidi...

Baada ya Kutazama Tu Mauaji ya Kinyama kwa Siku 467, Watawala wa Pakistan Sasa Wanasherehekea Usitishaji Vita

“Watu wa Pakistan wanaungana nami katika kukaribisha tangazo la usitishaji mapigano uliosubiriwa kwa muda mrefu nchini Palestina,” Waziri Mkuu wa Pakistan, Shehbaz Sharif, aliandika kwenye ukurasa wa Twitter mnamo tarehe 16 Januari 2025. Hata hivyo, ukweli ni kwamba, kwa zaidi ya mwaka mmoja, utawala wa Munir-Sharif umekuwa ukitizama tu vifo na uharibifu huko Gaza, ambako mauaji ya halaiki ambayo hayajawahi kuonekana yalitokea, na walionusurika sasa kuganda kwa baridi hadi kufa. Walikuwa wakiyatazama haya yote, kana kwamba Pakistan haina jeshi kubwa zaidi katika Ulimwengu wa Kiislamu, na kana kwamba jeshi hilo nimeundwa kwa watu wasio na uwezo, dhaifu, waoga na vilema, kwa hivyo watawala hawawezi kufanya chochote kujibu ukatili huu isipokuwa kulaani, kushutumu na kupinga.

Soma zaidi...

Watawala Vibaraka Wana Hofu juu ya Tishio kwa Viti vyao vya Utawala lakini Hawana Wasiwasi juu ya Vita vya Mauaji ya Halaiki!

Mnamo Jumanne na Jumatano, wizara za mambo ya nje za Jordan, Saudia, Imarati, Mamlaka ya Palestina na Jumuiya ya Nchi za Kiarabu zililaani uchapishaji wa akaunti rasmi unaohusiana na umbile la Kiyahudi wa ramani za kanda hiyo ambazo ni pamoja na maeneo ya ardhi za Palestina zinazokaliwa kwa mabavu, Jordan, Lebanon na Syria, wakidai kwamba hayo ni ramani ya kihistoria ya umbile la Kiyahudi. Walionyesha wasiwasi wao kuhusu masuala mawili.

Soma zaidi...

Unafiki wa Kisiasa katika Demokrasia Kamwe Hautaisha Mpaka Tuubadilishe kwa Siasa za Kiislamu

Mnamo tarehe 06/01/2025, rufaa ya aliyekuwa Waziri Mkuu wa Malaysia, Datuk Seri Najib Tun Razak kuhusu kuwepo kwa amri ya nyongeza ya Mfalme, inayomruhusu kutumikia kifungo chake kilichosalia chini ya kifungo cha nyumbani, imekubaliwa na mahakama kwa wingi wa 2-1. Majaji wa Mahakama ya Rufaa kisha wakaamuru kesi hiyo irudishwe katika Mahakama Kuu ili ombi la Najib la uhakiki wa mahakama lisikizwe na jaji mpya. Amri hii ya nyongeza, ambayo ni sehemu ya mchakato wa msamaha wa kifalme, imekuwa jambo la kawaida, ambalo halijawahi kutokea katika asili yake. Sambamba na hilo, kulikuwa na jambo jengine - mkusanyiko mkubwa wa kuonyesha mshikamano uliokusanyika nje ya mahakama, ulioandaliwa na vyama ambavyo hapo awali vilikuwa wapinzani wa kisiasa wa Waziri Mkuu huyo wa zamani.

Soma zaidi...

Kuganda Baridini hadi Kufa kwa Watoto Wachanga, na Njaa na Uuaji wa Watoto Hayatoshi Kukomesha Mauaji ya Halaiki huko Gaza!

Mnamo tarehe 30 Disemba, iliripotiwa kuwa mtoto wa 6 waliganda hadi kufa mjini Gaza ndani ya wiki mbili kutokana na hali ya baridi inayovumiliwa na wakimbizi wa Kipalestina katika mahema ya muda, waliohamishwa kutoka kwa nyumba zao kutokana na mashambulizi ya mara kwa mara ya Ukanda huo na uvamizi wa Kiyahudi. Ali al-Batran mwenye umri wa mwezi mmoja alifariki siku moja baada ya kaka yake pacha, Jumaa al-Batran, huko Deir el-Balah. Baba yao, Yahya Muhammad al-Batran, alisema kuwa Jumaa alipatikana kichwa chake kikiwa kama “donge la barafu”. Nariman, mama wa Sila Mahmoud al-Fassih mwenye umri wa siku 20, ambaye pia alifariki kutokana na kupungua kwa joto la mwili, alielezea kumkuta mtoto wake akiwa rangi ya bluu na kuuma ulimi wake huku damu ikimtoka mdomoni. Zaidi ya watu milioni 1.6 wa Gaza wamelazimishwa kuingia kwenye makaazi ya muda, wakiishi katika mahema hafifu ambayo hayatoi ulinzi kutokana na hali ya hewa ya baridi kali.

Soma zaidi...

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu