Jumatatu, 14 Dhu al-Qi'dah 1446 | 2025/05/12
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

Ikiwa Sera ya Mambo ya Nje ni Kufanya Urafiki na Adui, Basi Ziara ya Adui Hakika Itakaribishwa!

Inasikitisha kwamba Malaysia inaendelea kudumisha uhusiano wa kidiplomasia na China (na pia Urusi), licha ya ukatili uliothibitishwa na ukandamizaji unaofanywa na nchi hiyo ya kikomunisti dhidi ya Waislamu wa Uighur kwa miongo kadhaa. Mbali na uhusiano wa kidiplomasia, Malaysia pia imeanzisha uhusiano mkubwa wa kibiashara na China, na kuifanya kuwa mshirika mkubwa zaidi wa kibiashara wa nchi hiyo.

Soma zaidi...

Heshima ya Wanawake wa Kiislamu ni ya Khiyari katika Demokrasia za Kiliberali

Mnamo tarehe 3 Oktoba, CBS News iliripoti kwamba mwanamke mmoja Muislamu alizuiliwa na polisi wa Philadelphia ambao walimvua hijabu yake. Wakati wa saa 20 ya kukamatwa kwake, aliachwa wazi na hakupewa njia ya kubadilisha nguo zake. Kwa sasa ameajiri mshauri wa kisheria kutoka Baraza la Mahusiano ya Kiislamu la Marekani (CAIR) na anataka haki kwa unyanyasaji wake.

Soma zaidi...

Hizb ut Tahrir ni Chama cha Kisiasa Ambacho Mfumo Wake ni Uislamu. Kamwe Hakina Uhusiano wowote na Uanamgambo

Hizb ut Tahrir haina uhusiano wowote na uanamgambo. Hata hivyo, watawala wa Waislamu wanaogopa kazi ya Hizb ut Tahrir kwa sababu mradi wa Khilafah ni badali ya kimfumo na ya kisiasa kwa mfumo wa sasa wa dunia. Watawala wa Waislamu hawawezi kupambana kifikra na misimamo ya kifikra ya Hizb ut Tahrir. Wao, kwa hivyo hukimbilia uongo ili kuichafua kazi ya kisiasa na kifikra ya Hizb. Wanaunda uhalali wa kuwanyima wanachama wa Hizb haki zao za kisiasa.

Soma zaidi...

Mauaji Mapya na Msimamo wa Majeshi yetu ni Ule Ule! Je, hakuna Mwenye Hekima Miongoni mwenu Awezaye Kurudisha Izza Tena?!

Mwenyezi Mungu Mtukufu alitufahamisha kuwa sisi ni Umma wa kheri na jihad, na Mtume wa Mwenyezi Mungu (saw) alitupa bishara njema ya kwamba tutaifungua Roma, kwa hivyo Al-Quds iko karibu na ukombozi, Mwenyezi Mungu akipenda, kuwa mji mkuu wa dola inayokuja ya Khilafah, na historia kwa mapana yake yote inathibitisha kwamba sisi ni Ummah ambao hata tukilala kwa muda gani, tutaamka na kuwaondoa maadui zetu kwa pigo kubwa ambalo baada ya hapo hawana pa kukimbilia.

Soma zaidi...

Kuhusu Kesi ya Mahakama ya Rufaa ya Wafungwa wa Zamani wa Kisiasa

Kama tulivyotaja awali, mahakama ya rufaa inaendesha kesi ya wafungwa 15 wa zamani wa kisiasa huko Tashkent. Wanaume kumi na watano kati ya 23 (Mashababu), ambao awali walifungwa miaka 20 kwa fikra na imani zao, walihukumiwa mnamo Julai mwaka huu kifungo cha kuanzia miaka 7 hadi 14, wengi wao walihukumiwa kifungo katika kituo maalum cha uzuizi cha serikali.

Soma zaidi...

Mwaka Umepita, na Mauaji ya Kikatili ya Halaiki mjini Gaza Yanazidi na Kuenea. Je, Sio Wakati sasa kwa Ummah Kuwaondoa Watawala wake Waoga Ambao Wameshindwa Kuinusuru?!

Umbile hili ovu sio tu ni kadhia ya kiusalama, kijeshi, au ya kisiasa. Inawezekana kulitokomeza na kuliondoa kwenye uso wa ardhi milele, kwa nguvu ya jeshi la Jordan pekee. Hii si ndoto au nadharia; wale wanaotilia shaka wanahitaji tu kuitazama Gaza, fahari, ambayo kwayo ilisimama kidete dhidi ya Mayahudi, ambao sura yao ilichanwa chanwa mbele ya ulimwengu, ikidhihirisha umbile lao halisi.

Soma zaidi...

Viumbe Vidhalilifu Zaidi Vyatishia na Kuahidi! Je, Mtajibu Vipi?

Ulimwengu mzima umeshuhudia athari kubwa ya Operesheni ya Kimbunga cha Al-Aqsa kwa jeshi la umbile la Kiyahudi, ambalo lilijivunia nguvu, uwezo, ufikiaji, na uwezo wake wa kijasusi, hadi wakawadanganya walimwengu kwamba wao ndio jeshi lisiloshindwa na kwamba wao ndio wenye nguvu kuu katika Mashariki ya Kati, mlinzi wa maslahi ya Magharibi katika kanda hiyo, na kiongozi wa Amerika na Uingereza.

Soma zaidi...

Haishangazi hata kidogo kwamba Serikali ya Modi, kwa kuhofia kutokea kulikokaribia kwa Khilafah ingepiga marufuku Hizb ut Tahrir - Chama cha Kweli cha Kisiasa na Kisicho na Vurugu

Kwa kuhofia kuibuka Khilafah inayoongozwa na Hizb ut Tahrir, Wizara ya Mambo ya Ndani ya India (MHA) mnamo Alhamisi iliyopita (Oktoba 10, 2024) ilipiga marufuku Hizb ut Tahrir, ikieleza kwamba “inataka kusimamisha dola ya Kiislamu ya kimataifa na Khilafah, ikiwemo India, kupitia jihad na shughuli za kigaidi”.

Soma zaidi...

Tubas ni Shahidi wa Upendeleo wa Mamlaka ya Ndani ya Palestina dhidi ya Maadui wa Palestina na Watu wake

Ni zaidi ya uhaini, kwamba Mamlaka ya Ndani ya Palestina inatangaza uadui wake kwa watu wa Palestina, kama inavyotokea kwa kuwasaka Mujahidina wa Tubas, kuwakamata na kuwapiga risasi, kuwatawanya watu huko kwa gesi ya machozi, kuwaua Mujahidina na kuwatia nguvuni kama wafanyavyo Mayahudi, sawa kwa sawa, na kutenda kwa niaba yake kwa kujaza pengo wakati inashughulika na uvamizi wake dhidi ya Gaza na Lebanon.

Soma zaidi...

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu