Alhamisi, 17 Dhu al-Qi'dah 1446 | 2025/05/15
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

Kama Matokeo ya Kutekeleza Kanuni ya Kisekula ya Kibepari, Makampuni ya Hisa Yanaiba Pesa za Wanachi wa Kawaida wa Yemen

Mnamo siku ya Jumatano, tarehe 18 Dhu al-Qa`adah 1444 H sawia na 07 Juni 2023, Mahakama ya Fedha za Umma katika Manispaa ya Mji mkuu ilitoa uamuzi wake katika kesi ya kile kinachojulikana kama Kampuni ya Sultana Palace, ambapo iliwatuhumu watu 82 kwa kuwalaghai watu 110,000 katika kipindi cha kati ya Januari 2016 na Julai 15, 2020 na tarehe ya baadaye, kupitia hilo, walipata makadirio ya riyal 66,314,405,000.

Soma zaidi...

Khilafah Pekee ndiyo Inayoweza Kutatua Mgogoro Unaoendelea wa Uhaba wa Fedha katika Uchumi wa Pakistan

Serikali za Pakistan mtawalia zimekabiliwa na changamoto ya upungufu wa fedha. Inamaanisha kuwa serikali ina uhaba wa rasilimali za kutumia kwa ajili ya watu. Uhaba huu wa rasilimali unaoikabili serikali ni matokeo ya moja kwa moja ya miundo ya utawala wa kiuchumi inayotekelezwa nchini. Kipote cha watawala wa Pakistan kinatabikisha mtindo wa uchumi wa kirasilimali nchini.

Soma zaidi...

Amerika Inarefusha Mzozo nchini Sudan ili Kuwalazimisha Raia Kukubali Utawala wa Kijeshi

Marekani ilizindua kile ilichokiita jukwaa la Kuchunguza Mzozo wa Sudan. Mnamo tarehe 9 Juni 2023, afisi ya msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Marekani ilitoa taarifa kuhusu suala hili, “Jukwaa la Kuchunguza Mzozo wa Sudan linathibitisha dhamira ya Marekani ya uwazi tunapofanya kazi na washirika ili kukomesha mzozo wa kijeshi nchini Sudan

Soma zaidi...

Bajeti ya Kibepari ni Njia ya Uporaji wa Kinidhamu wa Pesa za Umma Kufadhili Uporaji na Ufujaji wa Kupangiliwa

Mnamo Juni 1, 2023, serikali ya Hasina ilizindua bajeti ya kitaifa inayoitwa "Kuelekea Bangladesh ya kijanja inayofuata maendeleo" kwa mwaka wa fedha wa 2023-24. Waziri wa Fedha AHM Mustafa Kamal aliweka bajeti ya Taka trilioni 7.6 ambayo ni asilimia 13.5 kubwa kuliko FY 23 yenye mwelekeo 'unaotarajiwa' wa kukabiliana na mfumko wa bei

Soma zaidi...

Hao ndio Wanajeshi wa Misri, wa Kweli, na hivi ndivyo inavyopaswa kuwa Hasira yao kwa ajili ya Mwenyezi Mungu

Ummah unaendelea kuweka mifano bora kabisa ya kujitolea muhanga, ikithibitisha kwamba ni Ummah ulio hai ambao unaweza kuugua lakini kamwe haufi na hauagi. Kila moto wa hasira unapopungua katika nyoyo za watu wake, wanyoofu huwasha cheche zake na kuwaangazia njia za Mto Nile dhidi ya wale walioasi dhidi ya Ummah wao, wakakiuka matukufu yake, wakanajisi sehemu zake takatifu, na kumwaga damu yake.

Soma zaidi...

Hizb ut Tahrir / Wilayah Tunisia Yawasilisha Barua ya Wazi kwa Waziri wa Sheria

Asubuhi ya Alhamisi, tarehe 01/06/2023, ujumbe kutoka Hizb ut Tahrir/Wilayah Tunisia, akiwemo Mkuu wa Afisi ya Kisiasa Ustadh Abdul Raouf Al-Amiri na Mkuu wa Kamati Kuu ya Mawasiliano Ustadh Yassin bin Yahya, na mjumbe wa Kamati Kuu ya Mawasiliano Ustadh Mwanasheria Fathi Al-Khamiri, na mjumbe wa Afisi ya Habari Ustadh Ahmed Al-Tatar, walimkabidhi Waziri wa Sheria, Bi Leila Jaffal, barua ya wazi kuhusu kukithiri kwa kukamatwa mara kwa mara kwa wanachama wa Hizb ut Tahrir nchini Tunisia.

Soma zaidi...

Uhalifu wa Kivita wa Mkongwe wa Vita Aliyepambwa Zaidi wa Australia ni Akisi ya Sera ya Vita ya Serikali

Madai ya uhalifu wa kivita dhidi ya mkongwe wa vita aliye hai nchini Australia, Ben Roberts-Smith, yalipatikana kuwa "kweli kabisa" na jaji wa Mahakama ya Shirikisho. Jaji huyo alihitimisha kuwa madai ya kuwashambulia na kuwaua Waafghani wasio na hatia na wasio na silaha yalithibitishwa, na kwamba alileta fedheha kwa nchi yake na jeshi la Australia kwa kuvunja 'kanuni za maadili na kisheria' za ushiriki wa kijeshi.

Soma zaidi...

Ujasusi wa Ufaransa Waikanyaga Sheria na Kufichua Ukweli kuhusu Nchi ya Maarifa na Uhuru kwa Kuomba Kufanyika Sensa ya Watoro Shuleni siku ya Idd al-Fitr!!

Gazeti la kila siku la Ufaransa la La Dépêche lilichapisha mnamo Ijumaa, Mei 19, 2023, habari iliyosema kwamba takriban shule mia moja huko Toulouse na vitongoji vyake zilipokea barua pepe kutoka kwa polisi wa Ufaransa wakiomba kiwango cha utoro wa wanafunzi mnamo Aprili 21, 2023, ambayo ilisadifu kuwa ni sikukuu ya Idd al-Fitr.

Soma zaidi...

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu