Jumamosi, 11 Shawwal 1445 | 2024/04/20
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

Uchaguzi Sio Suluhisho na Hautaleta Jambo Lolote Jipya, Hata kama Watu Wanaotekeleza Utawala Watabadilika na Wanajeshi Kuondolewa kwenye Orodha

Siku hizi, sauti zinamtaka Sisi ang’atuke na aondoke kwa salama kutoka kwa mandhari. Wakosoaji wa sera na maamuzi yake wameibuka kutoka kwa wale waliolelewa katika kukumbatia serikali hiyo na walikuwa miongoni mwa nguzo zake enzi ya Mubarak.

Soma zaidi...

Hao ndio Wanajeshi wa Misri, wa Kweli, na hivi ndivyo inavyopaswa kuwa Hasira yao kwa ajili ya Mwenyezi Mungu

Ummah unaendelea kuweka mifano bora kabisa ya kujitolea muhanga, ikithibitisha kwamba ni Ummah ulio hai ambao unaweza kuugua lakini kamwe haufi na hauagi. Kila moto wa hasira unapopungua katika nyoyo za watu wake, wanyoofu huwasha cheche zake na kuwaangazia njia za Mto Nile dhidi ya wale walioasi dhidi ya Ummah wao, wakakiuka matukufu yake, wakanajisi sehemu zake takatifu, na kumwaga damu yake.

Soma zaidi...

Jeshi la Al-Kinana ni Ngao ya Uislamu na Msaidizi wa Ummah Hivyo ndivyo lilivyokuwa na hivyo ni lazima Lirudi Kuwa

Hayat Washington ilisema kwenye tovuti yake, Jumatatu, 22/5/2023, kwamba vyombo vya habari vya Nigeria viliripoti kwamba Shirika la Miradi ya Huduma ya Kitaifa ya Wizara ya Ulinzi ya Misri inakusudia kuwekeza katika sekta ya kilimo katika jimbo la Ogun (magharibi).

Soma zaidi...

Utiifu kati ya Uislamu na Ubepari

Aliyekuwa Mufti Mkuu wa Misri, Mkuu wa Kamati ya Masuala ya Kidini na Kamati ya Awqaf (Wakfu) Bungeni, Ali Gomaa alisema kuwa fahamu ya uraia katika zama za kisasa ni mkataba wa kijamii kati ya mtu binafsi na dola na fahamu hiyo ndiyo iliegemezwa fahamu ya Utaifa juu yake, ambayo inahusisha haki na wajibu wa mtu binafsi katika jamii.

Soma zaidi...

Utawala wa Misri Hauna Uhalali na Mazungumzo yake ni Ujanja wa Kuwahadaa Watu Waliodhulumiwa

Mazungumzo ya kitaifa ambayo utawala wa Misri unadai si chochote bali ni ujanja ambao ulilazimishwa na hali mbaya ya kiuchumi, na yote ambayo inaota ni kwamba mgogoro huu upite, ili kuregelea sera zake za zamani, na pengine kuwafuta washirika wao wenyewe ambao walitoa shinikizo la aina yoyote juu yake, au wapinzani wake, ambao wanaweza kuwa wamekataa kuwa kama wale ambao Sisi aliwaleta kwenye kile alichokiita mazungumzo ya kisiasa ya kitaifa.

Soma zaidi...

Palestina Inakombolewa kwa Majeshi, Sio kwa Makongamano na Sheria ya Kimataifa

“Wakati umewadia wa amani...” Risala za Al-Sisi kutoka kwa Kongamano wa Kuinusuru Al-Quds, chini ya kichwa hiki Gazeti la Al-Dustour liliandika mnamo Jumapili 12/2/2023, kuwasilisha kile lilichokiita risala za rais wa Misri, ambaye alisema: Kadhia ya Palestina bado ni kipaumbele kwa Misri na Waarabu.

Soma zaidi...

Ushujaa wa Watu wa Ardhi Iliyobarikiwa ya Palestina Hauwezi Kushutumiwa!

France 24 iliripoti kwenye tovuti yake, Jumamosi, Januari 28, 2023, kwamba baadhi ya nchi za Kiarabu, ikiwemo Misri, Jordan na Imarati, zililaani shambulizi lililoua angalau 'Waisraeli' saba katika ufyatuliaji risadi uliowalenga waumini karibu na sinagogi la Kiyahudi katika mtaa wa makaazi katika Jerusalem Mashariki inayokaliwa kimabavu.

Soma zaidi...

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu