Jumapili, 16 Safar 1447 | 2025/08/10
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

Mauaji ya Kikatili ya Sohag katika eneo la Midford la Mji Mkuu Dhaka, ni Matokeo Yasiyoepukika ya Siasa za Kisekula na za Kiwendawazimu zisizomtambua Mungu

Katika eneo la Mitford la mji mkongwe wa Dhaka, baadhi ya viongozi wa eneo la Jubo Dal, wakiongozwa na chama kikuu cha kisekula cha kisiasa nchini humu BNP, walimuua kikatili mfanyibiashara wa vyuma vichakavu aitwaye Sohag (39) kwa kumdunga kisu na kumpiga na jiwe kubwa mfululizo kwa kukataa kulipa pesa za ulaghai. Walioshuhudia walisema kwamba wahalifu hao hawakuishia kumuua tu, bali waliendelea kuonyesha unyama kwenye mwili mfu wa Sohag hata baada ya kifo chake kuthibitishwa. Mwili uliojaa damu, ulioganda uliachwa katikati ya barabara na wauaji wakasimama juu ya mwili huo huku wakisherehekea kiwendawazimu.

Soma zaidi...

Jibu la Swali: Kuamiliana na Dola zilizo za Kivita Kivitendo

Ndugu mmoja aliniuliza kuhusu kufanya kazi katika kiwanda cha kutengeneza makontena katika makaazi ya Barkan. Hivi majuzi, sehemu ya kiwanda hiki iligeuzwa kwa manufaa ya jeshi la ‘Israel’, na kinatengeneza matrela ya kusafirisha majenereta ya umeme na vitu vyengine vinavyohusiana na jeshi. Je, inajuzu kufanya kazi katika sehemu hii inayotengeneza matrela kwa ajili ya jeshi?

Soma zaidi...

Kwa Maongezi Matamu, Yenye Sumu kuhusu Mustakabali wa Lebanon na Kanda! Mjumbe wa Marekani Tom Barrack yuko nchini Lebanon Kuimarisha Kukamilishwa kwa Makubaliano ya Amani na Uhalalishaji Mahusiano na Umbile la Kiyahudi!

Mnamo Julai 7, 2025, katika mkutano na waandishi wa habari katika Kasri la Rais, Mjumbe wa Marekani Tom Barrack alitoa taarifa akisema kwamba "Lebanon na kanda hii wana fursa nzuri ambayo lazima ichukuliwe," kwamba "wakati umefika wa kubadilisha kanda hii," na kwamba "kila mtu amechoshwa na kile kilichotokea," kama alivyoweka. Pia alisema kwamba "usalama utavutia uwekezaji kwa Lebanon," kwamba "Rais wa Marekani alithibitisha dhamira yake ya kuchangia kujenga amani na ustawi nchini Lebanon," na kwamba "fursa inapatikana kwa Walebanoni kuifanya nchi yao kuwa Lulu ya Mashariki kwa mara nyingine tena."

Soma zaidi...

Enyi Waislamu: Yaelekezeni macho yenu kwenye makasri ya watawala wenu, sio Ikulu ya White House!

Macho ya Waislamu kwa jumla, na waandishi wa habari, wachambuzi, waangalizi, na wale wanaohusika hasa, yanaelekea Ikulu ya White House, na kwenye matokeo ya mikutano ya Rais wa Marekani Donald Trump na Waziri Mkuu wa umbile la Kiyahudi, Benjamin Netanyahu. Je, Trump atamshinikiza Netanyahu kukubali kwa upole kusitisha vita vyake dhidi ya Gaza?

Soma zaidi...

Njama Endelevu, Iliyoimarishwa ya Kimataifa ya Kuzuia Mapinduzi ya ash-Sham yasifikie Malengo na Misingi yake

Mwenyezi Mungu (swt) alipowapa watu wa ash-Sham baraka za kumwangusha dhalimu mhalifu wa Syria, asubuhi ya tarehe 8 Disemba 2024, licha ya mipango na njama kubwa zilizopangwa na ulimwengu wote wa Magharibi, ukiongozwa na Marekani, ili kuyabatilisha mapinduzi na kuyazuia yasifikie lengo lake, ulikuwa ni utashi, azma, na Iman ya watu ash-Sham, kwa zana zao hafifu na za kawaida, ambapo hatimaye walishinda dhidi ya jumuiya ya kimataifa.

Soma zaidi...

Je! Uongozi wa Pakistan Ulipotezaje Hadhi Yake Mbele ya India na Trump?!

Uongozi wa kisiasa na kijeshi wa Pakistan ulipoteza ushindi uliopatikana na mwewe wa Jeshi lake la Anga, na simba wa jeshi lake la nchi kavu, juu ya India mnamo Mei, ikitoa funzo ambalo India haitalisahau kamwe, kwa kukubali kusitishwa kwa mapigano kati ya nchi hizo mbili. Hii ni licha ya msisitizo wa India kusitisha Mkataba wa Maji wa Indus, na kuinyima Pakistan karibu 80% ya maji ambayo hutiririka kutoka kwa Mto Indus, ambao unatoka China, unapitia India, na kisha kuingia Pakistan. Hii pia ni licha ya kwamba India bado inaendelea kuikalia kimabavu Kashmir... Kisha, baada ya upatanishi wa Rais wa Marekani, Donald Trump kuweka usitishaji vita kati ya pande hizo mbili, na kuiokoa India kutokana na mtego iliyokuwa imejiwekea, kutokana na hesabu potofu ya mienendo ya madaraka, serikali ya Pakistan ilitangaza, mnamo tarehe 21 Juni 2025, uteuzi wake wa Rais wa Marekani Donald Trump kwa ajili ya Tuzo ya Amani ya 2026, ikidai ni kutokana na “kuhusika kwake pamoja na Islamabad na New Delhi ambako kulipunguza hali iliyokuwa ikizorota kwa kasi” kati ya Pakistan na India mwezi Mei.

Soma zaidi...

Usaliti wa Watawala wa Pakistan na Kukumbatia Kwao Uhalalishaji wa Mahusiano: Utangulizi wa Kujiunga na Mkataba wa Khiyana wa Abraham na Kutumikia Maslahi ya Amerika ya Trump na Umbile la Kiyahudi

Marekani ya Trump sasa inajitahidi kuunda "Mashariki ya Kati Mpya," ambayo inatumikia maslahi ya Marekani katika kanda hiyo, shauku kuu ikiwa ni kuhakikisha amani, usalama, na upanuzi wa kambi ya kijeshi ya Amerika katika Ulimwengu wa Kiislamu, inayojumuishwa ndani umbile la Kiyahudi. Inatafuta kuliweka umbile la Kiyahudi kama mamlaka kuu katika eneo hilo kisiasa, kiuchumi, na kimfumo. Licha ya haya yote, vibaraka wa Amerika ya Trump wamekimbilia kutekeleza mradi huu, na kutumikia maslahi ya bwana wao.

Soma zaidi...
Jiunge kwa hii RSS feed

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu