Jumamosi, 11 Dhu al-Hijjah 1446 | 2025/06/07
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

Pesa Zilizotumika Kutuua, Tunawezaje Kujitolea Kuzilipa?!

Katika mahojiano na gazeti la ‘Financial Times’, waziri wa mambo ya nje wa Syria alifichua ruwaza ya serikali mpya ya Syria baada ya Assad, akisisitiza kwamba nchi hiyo “haitaki kuishi kwa msaada,” na kwamba suluhisho liko katika kupunguza vikwazo vya Amerika na Ulaya. Aliongeza kuwa serikali haina mpango wa kusafirisha mapinduzi hayo ng’ambo au kuingilia masuala ya nchi nyingine. Hivyo, ikionyesha mabadiliko makubwa katika sera ya kigeni. Pia alionyesha katika mahojiano yayo hayo nia ya kubinafsisha bandari na viwanda vinavyomilikiwa na serikali na kuvutia uwekezaji wa kigeni, licha ya changamoto kubwa zinazoikabili Syria, ikiwemo madeni ya dolari bilioni 30 kwa washirika wa zamani wa Assad; Iran na Urusi.

Soma zaidi...

Katika Kumbukumbu ya Kila Mwaka ya Kuvunjwa Khilafah na ukingoni mwa kuregea kwake, Tunaulingania Umma wa Kiislamu Uharakishe Kuisimamisha

Tangu Khilafah ilipovunjwa mnamo tarehe 28 Rajab 1342 H, sawia na 3 Machi 1924 M, Ummah umekuwa ukipitia majanga na kushindwa mfululizo; kuanzia mgawanyiko wa ardhi yake, mpaka kunyang'anywa mali yake, na kuwaua wanawe, na kudhihakiwa matukufu yake na mashambulizi dhidi ya Sharia yake. Hata hivyo, leo Khilafah iko karibu zaidi kuliko wakati mwingine wowote kurudi, Rayah (bendera) yake iko tayari kupeperushwa kwa mara nyengine tena juu ya ardhi za Waislamu. Kwa hakika, tunaishi katika wakati unaokumbusha usiku ule watu wa Madina walipokuwa wakishauriana, wakikubaliana kwamba wakati umefika wa kumpa Bay'ah bwana wetu Muhammad (saw) kama kiongozi wao wa kisiasa na mkuu wa dola.

Soma zaidi...

Watawala Vibaraka Wana Hofu juu ya Tishio kwa Viti vyao vya Utawala lakini Hawana Wasiwasi juu ya Vita vya Mauaji ya Halaiki!

Mnamo Jumanne na Jumatano, wizara za mambo ya nje za Jordan, Saudia, Imarati, Mamlaka ya Palestina na Jumuiya ya Nchi za Kiarabu zililaani uchapishaji wa akaunti rasmi unaohusiana na umbile la Kiyahudi wa ramani za kanda hiyo ambazo ni pamoja na maeneo ya ardhi za Palestina zinazokaliwa kwa mabavu, Jordan, Lebanon na Syria, wakidai kwamba hayo ni ramani ya kihistoria ya umbile la Kiyahudi. Walionyesha wasiwasi wao kuhusu masuala mawili.

Soma zaidi...

Unafiki wa Kisiasa katika Demokrasia Kamwe Hautaisha Mpaka Tuubadilishe kwa Siasa za Kiislamu

Mnamo tarehe 06/01/2025, rufaa ya aliyekuwa Waziri Mkuu wa Malaysia, Datuk Seri Najib Tun Razak kuhusu kuwepo kwa amri ya nyongeza ya Mfalme, inayomruhusu kutumikia kifungo chake kilichosalia chini ya kifungo cha nyumbani, imekubaliwa na mahakama kwa wingi wa 2-1. Majaji wa Mahakama ya Rufaa kisha wakaamuru kesi hiyo irudishwe katika Mahakama Kuu ili ombi la Najib la uhakiki wa mahakama lisikizwe na jaji mpya. Amri hii ya nyongeza, ambayo ni sehemu ya mchakato wa msamaha wa kifalme, imekuwa jambo la kawaida, ambalo halijawahi kutokea katika asili yake. Sambamba na hilo, kulikuwa na jambo jengine - mkusanyiko mkubwa wa kuonyesha mshikamano uliokusanyika nje ya mahakama, ulioandaliwa na vyama ambavyo hapo awali vilikuwa wapinzani wa kisiasa wa Waziri Mkuu huyo wa zamani.

Soma zaidi...

Hizb ut Tahrir / Wilayah ya Pakistan: Utekaji nyara wa Naveed Butt Unathibitisha kwamba Watawala wa Waislamu Wanazuia Kuhisabiwa Kwao!

Kesi 379 za upotezwaji wa lazima ziliwasilishwa kwa Tume ya Uchunguzi juu ya Kupotezwa kwa Kulazimishwa (COIOED) mnamo 2024. Watawala wa Waislamu huwateka nyara wale wanaowawajibisha, ni wakali kwa Waislamu na wana huruma na maadui. Hawakumnyonga jasusi na muuaji wa Kihindi Kulbhushan Yadav. Walimwachilia huru jasusi na muuaji wa Kimarekani Raymond Davis. Hata hivyo, walimteka nyara Naveed Butt, msemaji rasmi wa Hizb ut Tahrir katika Wilayah ya Pakistan, mnamo Mei 11, 2012. Naveed Butt alitoa wito wa ukombozi kutokana na ukoloni wa Marekani na kusimamishwa kwa Khilafah Rashida. Baada ya zaidi ya miaka kumi na mbili, watawala wangali hawajamwachilia huru. Ni lazima kwa umma na majeshi yake kuwang’oa madhalimu miongoni mwa watawala na kusimamisha Khilafah Rashida.

Soma zaidi...

Hizb ut Tahrir / Wilayah Tunisia: Matembezi ya Ukombozi: “Mapinduzi Yanaendelea Kujikomboa kutokana na Ukoloni na Kusimamisha Khilafah kwa Njia ya Utume.”

Matembezi ya 66 yalianzia mbele ya Msikiti wa Al-Fath katika mji mkuu wa Tunis, baada ya swala ya Ijumaa, mnamo tarehe 10 Januari 2025 yalioandaliwa na Hizb ut Tahrir / Wilayah ya Tunisia kuwanusurur watu wa Palestina na Al-Aqsa iliyo mateka, na kichwa chake kilikuwa “Mapinduzi Yanaendelea Kujikomboa kutokana na Ukoloni na Kusimamisha Khilafah kwa Njia ya Utume”

Soma zaidi...
Jiunge kwa hii RSS feed

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu