Maafa Mawili Yanaukumba Ummah wa Kiislamu – Watawala Wafisadi na Mfumo Fisadi – Yote Lazima Yabadilishwe kwa Wakati Mmoja
- Imepeperushwa katika Malaysia
- Kuwa wa kwanza kutoa maoni!
- |
Mnamo 26 Julai 2025, jiji la Kuala Lumpur lilishuhudia maandamano ya ajabu ya umma — maandamano makubwa ya kudai kujiuzulu kwa Waziri Mkuu wa Malaysia, Datuk Seri Anwar Ibrahim. Mkutano huu ulionyesha hasira kubwa na kuchanganyikiwa kwa watu kuelekea uongozi ambao haujashindwa tu kutekeleza ahadi zake za mageuzi, lakini pia umezidisha ugumu wa watu kupitia nyongeza za kodi, ongezeko la ushuru wa umeme, na kupanda kwa bei za bidhaa muhimu.



