Ijumaa, 10 Dhu al-Hijjah 1446 | 2025/06/06
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

Machafuko na Ghasia nchini Sudan Kusini Zinasisitiza Haja ya Umma kuwa na Kiongozi mwenye Kuwalinda

Ulimwengu umefuatilia machafuko ya Juba, mji mkuu wa Sudan Kusini, ambayo yalilenga watu waliokimbia makaazi yao na wakaazi kutoka Sudan Kaskazini. Matukio haya yalichochewa na ripoti zinazowatuhumu wanajeshi wa Sudan kwa kuwaua watu kutoka Sudan Kusini huko Wad Madani baada ya jeshi kuutwaa tena mji huo. Kulingana na gazeti la ‘Sudan Tribune’, Wasudan watatu waliuawa mjini Juba, na wengine saba kujeruhiwa.

Soma zaidi...

Nani Anasherehekea Maadhimisho ya Isra na Mi’raj?

Tawala za ulimwengu wa Kiislamu zinatoa wito wa kuadhimisha kumbukumbu ya mwaka huu, licha ya kuwa wametambua uwepo wa umbile linaloinajisi ardhi iliyobarikiwa ya Isra na Mi’raj. Wamesimama kando, wakishuhudia mito ya damu ya Wapalestina ikitiririka, mabomu yaliyosababisha nyumba kuwa vifusi, na uharibifu ulioharibu vitongoji, mazao, na vizazi. Wametazama huku hofu ikiwashika wazee na vijana, huku njaa isiyo kifani ikiwasibu, na huku baridi ikigandisha miguu na nyoyo za watu.

Soma zaidi...

Baada ya Kutazama Tu Mauaji ya Kinyama kwa Siku 467, Watawala wa Pakistan Sasa Wanasherehekea Usitishaji Vita

“Watu wa Pakistan wanaungana nami katika kukaribisha tangazo la usitishaji mapigano uliosubiriwa kwa muda mrefu nchini Palestina,” Waziri Mkuu wa Pakistan, Shehbaz Sharif, aliandika kwenye ukurasa wa Twitter mnamo tarehe 16 Januari 2025. Hata hivyo, ukweli ni kwamba, kwa zaidi ya mwaka mmoja, utawala wa Munir-Sharif umekuwa ukitizama tu vifo na uharibifu huko Gaza, ambako mauaji ya halaiki ambayo hayajawahi kuonekana yalitokea, na walionusurika sasa kuganda kwa baridi hadi kufa. Walikuwa wakiyatazama haya yote, kana kwamba Pakistan haina jeshi kubwa zaidi katika Ulimwengu wa Kiislamu, na kana kwamba jeshi hilo nimeundwa kwa watu wasio na uwezo, dhaifu, waoga na vilema, kwa hivyo watawala hawawezi kufanya chochote kujibu ukatili huu isipokuwa kulaani, kushutumu na kupinga.

Soma zaidi...

Hizb ut Tahrir / Ardhi Iliyobarikiwa: Kitengo cha Wanawake “Kalima kwa Mnasaba wa Kumbukumbu ya Miaka 104 ya Kuvunjwa Khilafah!”

Kwa mnasaba wa ujio wa kumbukumbu ya miaka 104 ya kuvunjwa kwa dola ya Kiislamu na makhaini wa Kiarabu na Kituruki iliyoasisiwa na Bwana wa Mitume Muhammad (saw) na maswahaba zake watukufu na waliobarikiwa, Mwenyezi Mungu awawie radhi, na kukomeshwa kwa mfumo wa utawala wa Kiislamu (Khilafah) mnamo tarehe 28 Rajab al-Muharram katika mwaka wa 1342 H sawia na 03/03/1924 M, Kitengo cha Wanawake cha Hizb ut Tahrir katika The Ardhi Iliyobarikiwa (Palestina) kinawasilisha mkusanyiko wa kalima hizo.

Soma zaidi...

Hizb ut Tahrir / Kenya Iliandaa Msururu wa Amali katika Kumbukumbu ya Miaka 104 ya Kuvunjwa kwa Dola ya Khilafah

Kama sehemu ya kumbukumbu ya miaka 104 ya kuondolewa kwa Khilafah, Hizb ut Tahrir/Kenya ilifanya kampeni nchi nzima katika mwezi mtukufu wa Rajab 1446 H. Kampeni hii iliyoanza mwanzoni mwa mwezi mtukufu wa Rajab ilihusisha shughuli mbali mbali; Darsa, Semina na Visimamo. Hii ilikuwa ni kuukumbusha Ummah kuhusu hali yake ya kusikitisha ambayo umekuwa ukikabiliana nayo tangu kuondolewa kwa Khilafah mnamo tarehe 28 Rajab 1342 H sawia na tarehe 3 Machi 1924 M.

Soma zaidi...
Jiunge kwa hii RSS feed

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu