Jumapili, 12 Dhu al-Hijjah 1446 | 2025/06/08
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

Uchumi wa Kibepari Unasambaratisha Familia na Misingi yake

Warsha ya karibuni ya kinachoitwa ‘usawa wa kijinsia’ iliyofanyika ndani Ngorongoro, Kaskazini mwa Tanzania iliibua suala la uwepo baadhi ya wanandoa kutoka katika jamii za wafugaji ambao wametelekezwa na waume zao walioondoka vijijini kwenda mijini kutafuta kazi, na wakati mwengine waume hao hawarudi katika familia zao.

Soma zaidi...

Usasa wa Kiislamu (الحداثة الإسلامية): Shambulizi kwa Sunnah ya Mtume

Usasa wa Kiislamu (الحداثة الإسلامية) unakusudia fikra inayotaka kutafsiri upya Uislamu ili kuwiana na maadili na miundo ya mfumo wa kilimwengu wa kiliberali wa Kimagharibi. Ikiibuka katika karne ya 19, wimbi hili la mageuzi lilisukumwa na watu mashuhuri kama vile Jamal ud Din Afghani, Muhammad Abduh, Rashid Rida, na Syed Ahmed Khan. Juhudi zao zililenga kufanya maridhiano ya Uislamu na mifumo ya kisasa ya kisiasa, kijamii na kiuchumi. Ufafanuzi huu upya, hata hivyo, mara nyingi ulihusisha upotoshaji wa kanuni za Kiislamu ili kuendana na desturi zinazobadilika za ulimwengu wa kisasa, ikiwa ni pamoja na fahamu za Kimagharibi kama vile utaifa, urasilimali, sheria za binadamu, haki za binadamu, usawa wa kijinsia, na maelewano ya dini mbalimbali.

Soma zaidi...

Hizb ut Tahrir / Wilayah Pakistan Umma Mmoja... Khilafah Moja

Katika kumbukumbu ya mwaka wa 104 H wa kuanguka kwa Khilafah mnamo tarehe 28 Rajab 1342 H sawia na tarehe 3 Machi 1924 M, Afisi Kuu ya Habari ya Hizb ut Tahrir inafuraha kuwasilisha kwa wafuasi na wageni wa tovuti za Afisi Kuu ya Habari, silsila mpya inayoitwa: “Ummah Mmoja... Khilafah Moja” iliyotolewa na Afisi ya Habari wa Hizb ut Tahrir ya Wilayah Pakistan.

Soma zaidi...

Tukio la Jalalabad: Kuilinda Dawah ni Wajibu kwa Kila Mmoja Wetu

Mnamo tarehe 26 Novemba, Mashababu wa Hizb ut Tahrir waliandaa amali dhidi ya rasimu ya sheria ya “Uhuru wa Dini na Mashirika ya Kidini” katika eneo la Jalalabad. Wiki tatu baadaye, kati ya Disemba 10 na 14, Kamati ya Serikali ya Usalama wa Kitaifa ilifanya msako katika nyumba 21 katika eneo hilo na kuwaweka kizuizini kinyume cha sheria wanachama wa Hizb ut Tahrir. Vikosi vya usalama havikuruhusu wanachama waliozuiliwa (Mashababu) kukutana na mawakili wao na badala yake walifanya uchunguzi mbele ya mawakili waliofunzwa mahususi kwa kesi hii. Kutokana na hali hiyo, Mashababu wetu walizuiliwa kwa muda kwa kipindi cha mwezi mmoja kwa kisingizio cha kusambaza vipeperushi misikitini vinavyopinga sheria hiyo. Kesi ya jinai ilifunguliwa dhidi yao chini ya shtaka la “kuandaa na kuendesha shughuli za itikadi kali.”

Soma zaidi...

Hotuba Inayohusu Bendera za Rayah na Liwaa za Mtume (saw) Ilipambwa kwa Takbira na Machozi katika Soko Kuu la Port Sudan

Hizb ut Tahrir / Wilayah Sudan ilitoa hotuba yake ya kisiasa ya kila wiki, iliyokuwa na kichwa: “Je, Mtume (saw) alikuwa na bendera na Rayah?”, mnamo Jumatatu tarehe 28 Jumada al-Akhirah 1446 H sawia na 30/12/2024 M. Ustadh Muhammad Jami’ (Abu Ayman), Msaidizi wa Msemaji Rasmi wa Hizb ut Tahrir katika Wilayah ya Sudan, alizungumza akisisitiza kuwa bendera ya Liwaa na Rayah katika Uislamu ni suala la dini, itikadi, mfumo na nembo ya Uislamu. Mtume (saw), ana benera (Liwaa) nyeupe kama bendera ya amiri jeshi, na bendera (Rayah) nyeusi kwa makamanda wa majeshi na vikosi, na inaitwa Uqab, zimeandikwa juu yazo “La Ilaha illa Allah Muhammad Rasulullah”.

Soma zaidi...

Ujasiri Wenu Kwa Mwenyezi Mungu, Enyi Madhalimu, Unatangaza Kukaribia Mwisho Wenu

Wakati Mayahudi walipokuwa wakiizingira Hospitali ya Kamal Adwan mjini Gaza, kisha kuivamia, kisha kuichoma moto, na kuwapeleka wagonjwa, majeruhi, na wafanyikazi wa matibabu kwenye hatima isiyojulikana hadi wakati wa kuandika taarifa hii, badala ya mamlaka hiyo kulaani uhalifu wao, badala ya kuuchochea ulimwengu dhidi ya vitendo vyao viovu na vya kikatili, badala ya kuuhamasisha Umma wa Kiislamu kuwanusuru watu wa Gaza, badala ya kuona haya kwa heshima ya majeraha ya Gaza na Ukingo wa Magharibi, walikataa kufanya chochote isipokuwa kuwa Jenin, wakifanya matendo ya Mayahudi na kuwanyanyasa watu wa Palestina mithili Mayahudi wanavyowanyanyasa.

Soma zaidi...

Mamlaka ya Palestina Yafuata Mbinu za Mashetani Kuhalalisha Uhalifu wake katika Kambi ya Jenin!

Mamlaka ya Palestina (PA) ilikusanya vyombo vyake vya habari na vipaza sauti vya wasemaji na nzi wa kielektroniki (wanyanyasaji wa mtandaoni wanaounga mkono serikali) ili kuchafulia jina kambi ya Jenin na watu wake na kuhalalisha umwagaji wa damu yao. Kisha, ilikusanya vyombo vyake na majambazi katika mji wa Khalil al-Rahman, na wachache wa wale walioitwa watu mashuhuri waliojiuza kwa PA kwa manufaa maovu, na wale ambao iliwatishia kutoka kwa wafanyikazi na walimu. Ilitumia wizara, shule zilizofungwa, na kukodi mabasi ili Jimbo la Khalil al-Rahman, mji na wilaya, ionekane kuwa pamoja nayo katika kumwaga damu ya watu wa kambi ya Jenin. Hii ijapokuwa inajua na wale walio nyuma ya kwamba Khalil al-Rahman, pamoja na watu wake na koo zake, hawawezi kukubali kwamba itoa nusu ya neno kumwaga tone la damu ya Waislamu. Kwa kitendo hiki kiovu, inataka kuleta mgawanyiko kati ya watu wa Palestina (kaskazini na kusini) chini ya pazia la uongo la uhalifu wake.

Soma zaidi...
Jiunge kwa hii RSS feed

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu