Jumapili, 12 Dhu al-Hijjah 1446 | 2025/06/08
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

Mabadiliko ya Kweli Yanaweza Tu Kuja Kutokana na Mradi Unaotokana na Aqidah ya Ummah. Ni nani Aliye Nao?

Umma wa Kiislamu umeishi kwa karne moja katika unyonge na udhalilishwaji, mfarakano na mgawanyiko, na utegemezi kwa nchi kubwa. Hii inatokana na matendo ya watawala Ruwabidha (wajinga watepetevu) ambao hawaheshimu udugu au ahadi yoyote, wanachojali tu ni kubakia kwenye viti vyao vibovu (vya utawala), kutekeleza mipango ya nchi za Kikafiri katika ardhi zetu ili kukazanisha udhibiti wao juu yetu na kupora mali zetu. Wamesimama dhidi ya kila mtu anayewapinga au kutokubaliana nao, au kujaribu kuwabadilisha, na kuwaweka chini ya kifungo, mateso, mauaji, na ukiukaji wa matukufu. Bashar al-Assad na utawala wake wa kihalifu sio wa mwisho wao, ambaye uhalifu dhidi ya watu wake ulifichuliwa na matukio ya hivi majuzi nchini Syria, uhalifu ambao ni wa aibu na kuwafukuza wale wenye maumbile yaliyo sawa.

Soma zaidi...

Amerika ya Trump Itashindwa Kufanya Kile ambacho Kikongwe Biden Hakuweza Kukifanya

“Rais mteule wa Marekani Donald Trump ametoa kauli kadhaa zenye utata ambazo zinaakisi waziwazi ukubwa wa tofauti katika sera za ndani na nje za Marekani na za Rais anayeondoka wa chama cha Democrat Joe Biden. Kwa upande wa sera ya mambo ya nje, Trump alisema atakomesha kile alichokitaja kuwa machafuko katika Mashariki ya Kati, kusitisha vita nchini Ukraine, na kuzuia kuzuka kwa Vita vya Tatu vya Dunia, bila kueleza jinsi atakavyofanya haya yote...

Soma zaidi...

Kizungumkuti cha Syria: Kati ya Ukosefu wa Utambuzi na Tumaini la Kweli

Baada ya miaka 14 ya vita na ukandamizaji, Syria inaonekana iko tayari kwa mabadiliko huku utawala wa Bashar al-Assad ukianguka na vikosi vya upinzani, vinavyoongozwa na Abu Mohammad al-Julani, vikichukua Damascus. Hata hivyo, matumaini ya mustakabali mzuri zaidi yanavurugwa na ushawishi mkubwa wa dola za nje kama vile Marekani na Uturuki, ambao zinaongoza njia ya Syria chini ya mifumo ya kisekula, inayoungwa mkono na Magharibi kama vile Azimio 2254 la Umoja wa Mataifa. Hili linazua maswali muhimu sana kuhusu iwapo tumaini la kweli linaweza kuwepo bila kukataa utawala wa kigeni na kuzipa kipaumbele kanuni za Kiislamu.

Soma zaidi...

Maingiliano ya Ummah na Hotuba: “Khilafah Ndio Mfumo wa Utawala katika Uislamu”

Hizb ut Tahrir / Wilayah Sudan ilitoa hotuba ya kisiasa katikati mwa soko kuu la Port Sudan mnamo Jumatatu, 23 Disemba 2024, chini ya mada: “Khilafah Ndio Mfumo wa Utawala katika Uislamu.” Hotuba hiyo ilitolewa na Ustadh Yaqub Ibrahim mwanachama wa Hizb ut Tahrir ambaye alisisitiza kuwa Mwenyezi Mungu Mtukufu amewawajibisha Waislamu kutabikisha hukmu za Uislamu na kupangilia nyanja zote za maisha yao kwa mujibu wake. Alieleza kwamba utabikishaji huu hutokea kupitia Bay’a halali kwa Khalifa ambaye anasimamisha Dini na kuifikisha kwa ulimwengu.

Soma zaidi...

Mkutano wa Waandishi Habari juu ya Sarafu na Mshtuko wa Nixon

Kabla ya kuanzishwa kwa sarafu, watu walitumia ubadilishanaji wa bidhaa kwa huduma. Kwa kuwa dhahabu na fedha zimezingatiwa kuwa madini ya thamani yenye kima cha asili kwa binadamu tangu nyakati za zamani, zilitabanniwa kama pesa, huku sarafu zikichongwa kwazo ili kurahisisha ubadilishanaji. Dhahabu, hasa, inajulikana kwa kuhimili kwake kuharibika kwa muda mrefu.

Soma zaidi...

Mapinduzi katika Ulimwengu wa Kiislamu Yatapelekea kwenye Mabadiliko ya Kweli Pale tu Watu wenye Nguvu Watakapotimiza Wajibu wao wa Shariah kwa Kuwaondoa Madhalimu na kuupa Nusra Ummah

Baada ya mabadiliko makubwa katika utawala wa Syria, baada ya mabadiliko ya utawala nchini Bangladesh na Afghanistan, pamoja na mabadiliko ya utawala yaliyokuja kabla ya haya, makundi tawala yanaendeleza simulizi ya zamani kwamba mapambano yaliyopangwa ya watu dhidi ya watawala yanazua “machafuko, ufisadi na ukosefu wa utulivu.” Iwe ni mkuu wa Jeshi la Pakistan, Jenerali Asim Munir, au watawala wengine, wote wanadai kwamba hawataruhusu nchi zao kuwa “Libya, Syria, Iraq au Sudan” nyengine.

Soma zaidi...

Amerika ni Adui Yenu Dhahiri. Majaribio ya Kuidekeza ni Batili. Ni kwa Kusimamisha Khilafah Rashida Pekee, ndio Mnaweza Kuzima Faida ya Kimkakati ya Amerika na Kuipa Jibu Lililofaa!

Mnamo tarehe 21 Disemba, 2024, Afisi ya Mambo ya Nje ya Pakistan “ilipinga vikali ukosoaji wa Marekani wa mpango wa makombora wa masafa marefu wa Pakistan, na kuuita usio na mantiki na usio na muktadha wa kihistoria kwani iliapa kuendelea kukuza uwezo wake wa makombora sambamba na kiwango cha chini uzuiaji wake wa kuaminika wa kimkakati, ikisisitiza hitaji lao la kukabiliana na vitisho vinavyoibuka kutoka India.

Soma zaidi...

Jibu la Swali: Je, Yajuzu Mtu Kumpa Zaka Dadake au Binti Yake?

Uislamu umewajibisha kushibisha mahitaji haya ya kimsingi na kuwapa wale wasioweza kuyapata. Ikiwa mtu binafsi anajipatia wenyewe, ni vizuri; ikiwa hawawezi kujiruzuku kwa sababu ya ukosefu wa pesa za kutosha au kutokuwa na uwezo wa kupata pesa za kutosha, Shariah inawajibisha wengine kuwasaidia hadi mahitaji haya ya kimsingi yatimizwe.

Soma zaidi...

Jibu la Swali: Biashara ya Mtandaoni (E-Commerce)

Je, biashara ya mtandaoni (e-commerce) na kampuni ya DXN ya Malaysia inaruhusiwa? Kampuni hii inategemea uuzaji wa virutubisho vya lishe, shampoo, krimu za ngozi...nk. Unapo  nununua kutoka kwake kiasi fulani, inatoa punguzo (discount). Pindi pointi zako zikifika 100 inakupa punguzo la asilimia sita. Kadiri unavyopata pointi zaidi, ndivyo inavyokupa punguzo kubwa zaidi, na pointi hizi hubadilishwa kuwa kiasi cha pesa ambacho huhamishiwa kwako ama kwa njia ya bahasha au barua ambayo hutolewa kwako kila mwezi, au kuhamishiwa kwenye salio (balance) lako la benki.

Soma zaidi...
Jiunge kwa hii RSS feed

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu