Jumapili, 12 Dhu al-Hijjah 1446 | 2025/06/08
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

Mfano Hatari Ambao Haupaswi Kupuuzwa

Katika mfano hatari katika historia ya mapinduzi, Huduma Kuu ya Usalama mjini Aleppo iliteka nyara wanawake kumi mnamo siku ya Jumamosi, 21 Disemba 2024. Wanawake hao walikuwa wamejitokeza wakiandamana, wakitaka utawala wa Uislamu na kuachiliwa huru waume zao, vijana wao na watoto wao waliotekwa nyara zaidi ya mwaka mmoja na nusu uliopita. Watu hawa wamefungwa jela na Jolani [al-Julani] mjini Idlib tangu Mei 7, 2023!

Soma zaidi...

Mumempindua Dhalimu wa ash-Sham, Basi Msikubali Chochote baada ya Dhalimu huyo Zaidi ya Utawala wa Uislamu na Dola yake, Khilafah

Baada ya miaka kumi na nne ya mihanga mikubwa ya watu wa Syria katika mapinduzi yao yaliyobarikiwa, Damascus ilikuwa kwenye miadi ya ushindi alfajiri ya leo, Jumapili 8 Disemba 2024, kwa Idhini ya Mwenyezi Mungu (swt). Mwenyezi Mungu (swt) alitubariki kwa kupinduliwa kwa dhalimu Assad, baada ya zama za dhulma, uhalifu na udhalimu wa familia ya Assad katika utawala wake wa chuki, wa kimadhehebu kwa muda wa miaka 54. Katika zama zao, walipiga vita Dini, Shariah na waja wa Mwenyezi Mungu (swt). Waliwatia watu kila aina ya mateso. Hakuna ushahidi bora zaidi wa hili kuliko idadi ya kutisha ya wafungwa ambao waliachiliwa huru kutoka kwa magereza yake ya dhulma, maovu.

Soma zaidi...

Uvamizi Mpya wa Hay'at Tahrir al-Sham kwa Wanachama wa Hizb ut Tahrir: Hatua ya Kuelekea Uhalalisha Mahusiano au Kuelekea Kujisalimisha?!

Uvamizi mpya wa Huduma ya Kuu ya Usalama yenye uhusiano na Hay'at Tahrir al-Sham (HTS) kwa wanachama wa Hizb ut Tahrir ulikuja baada ya jina kupendekezwa kwa Ijumaa ya 22/11/2024: “Yeyote Anayelinda Mipaka ya NATO, Kuzuia Ufunguzi wa Vita na Kulinda Mipaka ya Utawala.” Huduma Kuu ya Usalama, baada ya uhamasishaji mkubwa iliyoufanya mnamo Ijumaa usiku, iliteka nyara idadi mpya ya wanachama wa Hizb ut Tahrir, ambao ni wakili Muhammad al-Sharif na Fateh al-Tarmanini kutoka mji wa Tarmanin, pamoja na mwanachama Omar Rahhal kutoka mji wa Kafr Nouran, na ndugu wawili, wanafunzi Bashar Abdul-Hay Samsoum na Ahmad Abdul-Hay Samsoum kutoka mji wa Atarib. Hapo awali, Sheikh Amir Salim, ambaye alihamishwa kutoka Jimbo la Daraa, alitekwa nyara.

Soma zaidi...

Uvamizi wa Umbile la Kiyahudi na Mashambulizi Yake ya Kiadui kwenye Ardhi ya Ash-Sham Jinai zinazoendelea ambazo ni Utawala wa Uislamu na Dola Yake ya Khilafah Pekee ndio Unaoweza Kusitisha na Kuvunja Nguvu yao

Tangu kuanguka kwa dhalimu Assad mnamo tarehe nane mwezi huu, makundi ya umbile la Kiyahudi yamekuwa yakishambulia ardhi ya Ash-Sham, na ndege zake zimekuwa zikivamia anga yake kwa mashambulizi ya angani yenye nia mbaya ambayo yalilenga miji kadhaa, na maeneo ya kijeshi. Mashambulizi haya yamefika katika mji wa Deir ez-Zor mashariki mwa Syria. Mashambulizi hayo ya chuki na kihalifu yamejikita kwenye maghala ya silaha, vikosi vya ulinzi wa anga katika maeneo ya kati na kusini, vituo vya utafiti wa kisayansi wa kijeshi, na viwanja vya ndege vya kijeshi, ikiwa ni pamoja na uwanja wa ndege wa kijeshi wa Al-Mazzeh viungani mwa Damascus.

Soma zaidi...

Ziara ya Biden ya Dakika za Mwisho Afrika: Kuimarisha Ajenda ya Ukoloni na Unyonyaji wa Marekani

Jumatano ya tarehe 04/12/2024 Rais wa Marekani Joe Biden alihitimisha ziara yake ya siku tatu nchini Angola. Katika siku ya mwisho ya ziara yake, Biden alitembelea mradi wa Ukanda wa Lobito, mradi wa reli inayojengwa kwa ufadhili wa Marekani yenye kilomita 1,300 inayoanzia Zambia kwenye utajirim kubwa wa madini ya shaba hadi bandari ya Lobito kusini magharibi mwa taifa la Angola. Pia, Biden alifanya mkutano na maraisi wa Angola, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, Zambia na Makamu wa Rais wa Tanzania (VOA Africa 05/12/2024).

Soma zaidi...
Jiunge kwa hii RSS feed

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu