Historia Inawalingania Wanajeshi wa Pakistan – Wakati Umewadia wa Uongozi wa Kweli wa Kiislamu
- Imepeperushwa katika Habari na Maoni
- Kuwa wa kwanza kutoa maoni!
- |
Shambulizi la Pahalgam mnamo Aprili 2025, ambapo washambuliaji wenye silaha waliua raia 26 na kujeruhi wengine kadhaa, kwa mara nyingine tena limeitupa Kashmir katikati ya hali ngumu ya kisiasa na kiitikadi. Ingawa mamlaka mara moja zilielekeza kidole cha lawama kwa makundi ya wapiganaji yanayoungwa mkono na Pakistan kuwa yanahusika, tukio hilo liliingizwa siasa haraka na kuingizwa katika masimulizi mapana ambayo yameunda utawala wa Narendra Modi kwa zaidi ya muongo mmoja: mapambano kati ya dola ya kitaifa ya Kibaniani na wanaodaiwa kuwa maadui zake—wa ndani pamoja na nje.