Jumapili, 19 Dhu al-Hijjah 1446 | 2025/06/15
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

Historia Inawalingania Wanajeshi wa Pakistan – Wakati Umewadia wa Uongozi wa Kweli wa Kiislamu

Shambulizi la Pahalgam mnamo Aprili 2025, ambapo washambuliaji wenye silaha waliua raia 26 na kujeruhi wengine kadhaa, kwa mara nyingine tena limeitupa Kashmir katikati ya hali ngumu ya kisiasa na kiitikadi. Ingawa mamlaka mara moja zilielekeza kidole cha lawama kwa makundi ya wapiganaji yanayoungwa mkono na Pakistan kuwa yanahusika, tukio hilo liliingizwa siasa haraka na kuingizwa katika masimulizi mapana ambayo yameunda utawala wa Narendra Modi kwa zaidi ya muongo mmoja: mapambano kati ya dola ya kitaifa ya Kibaniani na wanaodaiwa kuwa maadui zake—wa ndani pamoja na nje.

Soma zaidi...

Ukamataji wa Waislamu nchini Urusi

Vikosi vya usalama vilipandikiza kazi za SIM wakati wa upekuzi katika nyumba za Waislamu, kesi za kushiriki katika shirika la kigaidi zilitungwa, jamaa zao walisema katika malalamiko kwa wanaharakati wa haki za binadamu. Kwa jumla, watu 48 walizuiliwa wakati wa operesheni ya vikosi vya usalama huko Nalchik na Nartan, Kavkazsky Uzel (tovuti ya habari) iliripoti mnamo Juni 3, ikinukuu wanaharakati wa haki za binadamu.

Soma zaidi...

Ulimwenguni wa Kusini na Mfumo Mpya wa Ulimwengu – Tumaini au Sarabi?

Mnamo Aprili 2025, wakati wa Mkutano wa Mawaziri wa Mambo ya Nje wa BRICS nchini Brazil, Waziri wa Mambo ya Nje wa Malaysia Datuk Seri Mohamad Hasan alitoa ujumbe ulio wazi: ulimwengu hauwezi tena kutegemea utawala wa dola moja ili kuhakikisha utulivu wa kimataifa. Alihimiza mataifa ya Kusini mwa Ulimwengu – inayojumuisha nchi zinazoendelea kote Asia, Afrika, Amerika ya Kusini, na Oceania – kuinuka kwa pamoja na kuongoza uundaji wa mfumo mpya wa kilimwengu. Matamshi yake yanaangazia sauti za vibwagizo vinazokua zisizoridhika na utawala wa muda mrefu na kuanguka kwa uaminifu wa utawala wa kimataifa unaoongozwa na Marekani.

Soma zaidi...

Ulemavu wa Marekani huku Ikijila Yenyewe ikiwa Hai Sehemu Nyingi Zaidi

Kichwa cha habari cha Fox News mnamo tarehe 22 Mei kilisema kwamba "Utawala wa Trump wasitisha mpango wa visa ya wanafunzi wa Harvard" na makala hayo yalimnukuu Waziri wa Elimu, Kristi Noem, akisema: "Utawala huu unaihisabu Harvard kwa kuendeleza vurugu, chuki dhidi ya Mayahudi, na kuratibiana na Chama cha Kikomunisti cha China kwenye chuo chake ... Ni fursa, sio haki, kwa vyuo vikuu kuchukua wanafunzi wa kigeni na kufaidika na malipo yao ya juu ya masomo ili kusaidia kulipa ruzuku zao za mabilioni ya dolari. Harvard ilikuwa na fursa nyingi za kufanya mambo kwa usahihi. Ilikataa. Wamepoteza cheti chao cha Mpango wa Wanafunzi na Ubadilishanaji wa Wageni (Student and Exchange Visitor Programme) kutokana na kushindwa kwao kuzingatia sheria. Hebu hili na liwe ni onyo kwa vyuo vikuu na taasisi zote za kielimu kote nchini."

Soma zaidi...

Bajeti ya kila Mwaka ya Serikali: Utumwa wa Kudumu wa Kikoloni

Dola za kiliberali za kirasilimali zimeundwa kupitia mpango wa kifedha wa kila mwaka wa uendeshaji wa mapato na matumizi ya serikali. Sera hii ya kifedha ambayo inashirikisha nchi za ulimwengu wa tatu katika shinikizo kubwa la kuweka usawa kati ya usimamizi wa serikali wa mambo ya watu na utawala wa kikoloni. Sera ya fedha ya kimataifa (mfumo wa fedha zisizo na thamani ya dhati (fiat)) ambazo thamani zake zimeegemezwa kwa dolari kwa Petroli lazima zisawazishe biashara (mahuruji na maduhuli) ili kuelea thamani ya sarafu ya ndani kutokana na kuzama kwenye dimbwi la mporomoko wa kiuchumi.

Soma zaidi...

Ukoloni Mamboleo ndio Unaopelekea Ukosefu wa Umeme Nchini Zambia

Tarehe 1 Februari 2025, Bodi ya Udhibiti wa Nishati ya Zambia (ERB) iliongeza muda wa tozo za umeme za dharura za Shirika la Ugavi wa Umeme la Zambia (ZESCO) kwa miezi mitatu ya ziada, ambayo ni kuanzia Februari 1 hadi Aprili 30, 2025, huku nchi ikiendelea kukabiliwa na tatizo kubwa la upungufu wa umeme.

Soma zaidi...

Umbile la Kigaidi la Kizayuni Limeufanya Ukingo wa Magharibi kuwa Makaburi ya Watoto kama vile Gaza, Huku Majeshi ya Nchi za Waislamu Yakitazama

Mnamo tarehe 7 Februari, shirika la ‘Save the Children’ liliripoti kwamba watoto wasiopungua 224 wameuawa katika Ukingo wa Magharibi na wanajeshi au walowezi wa Kizayuni tangu Januari 2023, mdogo zaidi akiwa na umri wa miaka 2 pekee. Kulingana na Umoja wa Mataifa, watoto 171 waliuawa katika Ukingo wa Magharibi tangu tarehe 7 Oktoba 2023 - sawia na karibu 1 kila siku. Hakuna mwanajeshi wa Kizayuni aliyefunguliwa mashtaka au kuwajibika kwa mauaji haya. Afisi ya Umoja wa Mataifa ya Kuratibu Masuala ya Kibinadamu ilisema kuwa kumekuwa na ongezeko la mara 20 la idadi ya watoto wa Kipalestina waliouawa na mashambulizi ya anga ya umbile la Kiyahudi katika Ukingo wa Magharibi katika miaka ya hivi karibuni.

Soma zaidi...

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu