Alhamisi, 07 Jumada al-thani 1447 | 2025/11/27
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

Mwaliko wa Kuhudhuria Kikao cha Kisiasa

Afisi ya Habari ya Hizb ut Tahrir katika Wilayah Sudan inafuraha kuwaalika wanahabari, wanasiasa, na wale wote wanaopenda masuala ya umma, kuhudhuria na kushiriki katika kikao kipya cha Kisiasa, ambapo Ustadh Ya‘qub Ibrahim, mwanachama wa Hizb ut Tahrir/Wilayah Sudan, atakuwa mgeni, chini ya kichwa: Ulaya na Ushawishi Wake kwa Matukio nchini Sudan.

Soma zaidi...

Majibu ya Vyombo vya Habari kwa Yaliyomo kwenye Makala ya Mwandishi Sabah Muhammad Al-Hassan

Hizb ut Tahrir ni chama cha kisiasa ambacho mfumo wake ni Uislamu, kinataka kurudisha mfumo kamili wa maisha ya Kiislamu kwa kusimamisha Khilafah Rashida ya pili kwa njia ya Utume kwa njia ya kisiasa, na hakitekelezi vitendo vyovyote vya kisilaha si kwa kumwogopa mtu yeyote, bali ni kujifunga na njia ya Mtume (saw) katika kusimamisha dola ya kwanza ya Kiislamu.

Soma zaidi...

Kujibu Matamshi ya Mjumbe wa Marekani Tom Barrack

Kwa mara nyingine tena utawala wa Marekani unaonyesha sura yake halisi kupitia taarifa za mjumbe wake Tom Barrack, katika mahojiano yake yaliyotangazwa na Sky News na mtangazaji mkuu wa IMI International Hadley Gamble, ambaye alijiruhusu kuingilia waziwazi katika masuala ya Lebanon na kubainisha sifa za dori za taasisi ya Jeshi.

Soma zaidi...

“Khiyana ya ‘Ruwaibidha’ (watawala wasiostahiki) na kuidhinishwa kwa mpango wa Trump kwa gharama ya damu ya mashahidi wa Palestina”

Baada ya hotuba ya rais wa Marekani kwenye Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa – ambayo asili ilikusudiwa kuhakiki kadhia ya Palestina – na katika wakati ambapo, kwa msimamo mmoja kutoka zaidi ya dola 150 kati ya dola 193 za Umoja wa Mataifa, “dola ya Palestina” tayari imetambuliwa, Rais Trump aliikejeli jumuiya ya kimataifa kwa kuyaita maneno ya “viongozi” kama “domo tupu.” Pia alikejeli makubaliano ya kimazingira, akaiichukulia mikataba ya uhamiaji kuwa ya kudharauliwa, na akakashifu mchakato wa Ulaya wa kuitambua Palestina kwa kuiita udhaifu. Hotuba yake ilionekana kama dua ya mwisho ya mazishi (fatiha) iliyosomwa juu ya makubaliano ya kimataifa, madai ya mtazamo wa upande mmoja wa Amerika katika masuala ya kimataifa, na tangazo la kulazimisha rai yake juu ya Mashariki ya Kati – haswa suala la Palestina.

Soma zaidi...

Kutambuliwa kwa Dola ya Palestina Kutambuliwa kwa Mayahudi Kunyakua 78% ya Palestina!

Uingereza, Canada, Australia na Ureno zililitambua ile inayoitwa “Dola ya Palestina,” na kufuatiwa na nchi kadhaa katika mkutano wa ngazi ya juu wa kimataifa wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa uliofanyika kuanzia Septemba 22-30, 2025, na ulioongozwa na Ufaransa na Saudi Arabia. Utambuzi huu ulikaribishwa na watawala Ruwaibidha (wajinga wasio na maana) wa Waislamu, pamoja na Jumuiya ya Ushirikiano wa Kiislamu na Jumuiya ya Waarabu. Jambo la kushangaza ni kwamba, ilikaribishwa pia na mashirika ya Kipalestina, ambayo yanaona kuwa ni matunda ya uthabiti wao, kana kwamba Palestina imekombolewa na na umbile la Kiyahudi kung'olewa!

Soma zaidi...

Ametokea kwa Mlango, Anaingia kwa Dirisha

Kwa mara nyengine tena, Amerika inafichua kiburi chake mbele ya ulimwengu. Onyo la Donald Trump kwamba “mambo mabaya yatatokea” isipokuwa Afghanistan ikabidhi Kambi ya Anga ya Bagram inaakisi sauti ile ile ya kibeberu ambayo kwa muda mrefu imekuwa ikifafanua sera ya Marekani kwa ardhi za Waislamu. Maneno kama haya sio lugha ya dola huru zinazoamiliana kwa usawa, bali ni maagizo ya mkoloni ambaye anaziona ardhi za Waislamu kama kituo cha kijeshi kwa ajili ya matamanio yake. Hii ndiyo hali halisi ya siasa za Magharibi: ushurutishaji, vitisho, na kudharau ubwana wa nchi zetu.

Soma zaidi...

Si Mtazamaji: Dori ya Marekani katika Shambulizi la ‘Israel’ dhidi ya Doha

Mnamo Septemba 2025, “Israel” ilishambulia Doha, na kuua viongozi wa Hamas na mlinzi wa Qatar. Gazeti la ‘The Independent’ liliripoti kuwa Trump alikasirika kwa sababu Netanyahu alimfahamisha katika dakika za mwisho tu – “He's f***ing me” – huku vyanzo vya “Israel” badala yake vilizungumza kuhusu “idhini” ya Trump.

Soma zaidi...

Sudan: Mfano Mwengine wa Utaifa Uliofeli

Tangu 1945 kumekuwa na angalau nchi mpya 34 ambazo zimetambuliwa na Umoja wa Mataifa. Hili lilitokana na wimbi la utaifa ambalo lilienea kote ulimwenguni kwa miongo kadhaa tangu katikati ya miaka ya 1900. Mipaka ya kindoto ilichorwa ili kutoa uhuru kwa makundi mbalimbali na haki ya kutawala, kwani nchi kama vile Sudan iliyoungana hapo awali zilitumbukia ndani ya mizozo na machafuko.

Soma zaidi...

Kutoka Uingereza hadi Australia: Utambuzi wa Uongo Unafungua Njia ya Uhalalishaji Mpana zaidi wa Mahusiano

Miaka miwili baada ya mauaji ya halaiki yaliyofanywa na umbile la Kizayuni katika Ardhi Iliyobarikiwa ya Palestina, likiungwa mkono kikamilifu na Marekani, NATO, na washirika wao makruseda, Umoja wa Mataifa na dola zenye nguvu duniani wamejibu kwa kulituza umbile hilo. Utambuzi wa “Dola ya Palestina” unakuja huku Gaza ikivuja damu, na baada ya dola 150+ tayari kutoa utambuzi sawia.

Soma zaidi...
Jiunge kwa hii RSS feed

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu