Licha ya Serikali ya Jordan Kuwaangusha Watu wa Gaza na Kujisalimisha Kwake kwa Mpango wa Trump, Vyombo Vyake vya Usalama Vyamkamata Mmoja wa Wanachama wa Hizb ut Tahrir
- Imepeperushwa katika Jordan
- Kuwa wa kwanza kutoa maoni!
- |
Serikali ya Jordan inaendelea kwa kiburi katika dhambi na uvamizi, licha ya kuwaangusha watu wa Gaza, na kwa hakika ushirikiano wake na umbile la Kiyahudi katika vita vya mauaji ya halaiki ambavyo imepigana katika Ukanda wa Gaza, kwa kulipatia njia za uwezeshaji na uhai. Haikusita kumbariki Trump mhalifu katika kuifilisi kadhia ya Palestina kwa kuhudhuria kile kinachoitwa “Baraza la Amani” ili kuwa shahidi wa uongo wa mpango wa Trump wa udhibiti juu ya ardhi za Waislamu na kwa kupotea kwa Ardhi Iliyobarikiwa ya Palestina.



