Gazeti la Al-Raya: Vichwa Vikuu vya Toleo 569
- Imepeperushwa katika Al-Rayah
- Kuwa wa kwanza kutoa maoni!
- |
Mnamo Jumapili, 12 Oktoba 2025, Hizb ut Tahrir/Wilayah ya Tunisia iliandaa kikao cha mazungumzo kwa kichwa “Mradi wa Ukombozi... Katika Mizani ya Hukmu za Sheria ya Kiislamu” katika eneo la Kairouan. Kikao hicho kilihudhuriwa na idadi kubwa ya wakaazi wa eneo hilo.
Mnamo tarehe 9 Oktoba, Gazeti la ‘the Guardian’ liliripoti kwamba mkuu wa shirika la kutoa misaada la Waislamu wa Uingereza Shaista Gohir, alikuwa na 'wasiwasi mkubwa' huku uhalifu wa chuki dhidi ya Uislamu ukiongezeka kwa theluthi moja kulingana na takwimu za hivi punde za serikali. Alisisitiza kuwa hata takwimu hizi zinazosumbua pengine ni ‘sio halisi’ kwani matukio mengi hayaripotiwi.
Uhalisia wa sasa wa Waislamu leo ni sawa na awamu ya Makka ya ujumbe wa Mtume, kwani wanaishi katika “Dar ul-Kufr” (Nyumba ya Ukafiri) kutokana na kutawaliwa na sheria zisizokuwa zile zilizoteremshwa na Mwenyezi Mungu (swt) na neno “Dar” ni istilahi ya kifiqhi iliyofafanuliwa kwa kina katika vitabu vya fiqh (Fiqh ya Shariah). Hili linalazimu kufuata njia ya mabadiliko ya Makka. Mtume (saw) alifuata hatua tatu kuu katika njia yake ya kusimamisha dola ya Kiislamu.
Enyi watu wa Gaza: nyinyi leo mmesimama katika msimamo wa Mitume (as) na watu wema, mkisimama kidete kwa ajili ya haki dhidi ya dhulma. Kila dhiki, kila jeraha, kila Shahidi ni riziki katika mizani yenu ya mema, na kunyanyua daraja yenu. Ukuruba wa Mwenyezi Mungu uko pamoja nanyi, na ushindi wake uko karibu, basi subirini na muwe thabiti, na furahieni kwa yale aliyoyaahidi Mwenyezi Mungu (swt) ya bustani na daraja, na heshima ya dunia ambayo hupatikana kwa uthabiti na kujitolea mhanga.
Maandamano ya watu wa Gabes kusini mwa Tunisia yanaendelea kwa sababu ya sumu inayotolewa kutoka kwa tata ya kemikali, ambayo imegeuza jiji hilo kuwa eneo lililoathirika kimazingira na kiafya, na kuathiri moja kwa moja afya ya wakaazi wa Gabes na mali asili yake. Saratani na magonjwa ya kupumua yameenea, na suala hilo limefikia hata visa vya kukosa hewa miongoni mwa wanafunzi. Miongo kadhaa ya ahadi za uongo na kupuuzwa kwa makusudi kumeifanya Gabes kuwa ishara ya kutengwa na uchafuzi wa mazingira, kwani utajiri wa phosphate umegeuka kutoka kuwa baraka hadi laana kwa sababu ya sera za serikali ya kisasa, ambayo ilichagua faida ya haraka na maslahi ya makampuni makubwa kwa gharama ya afya ya watu na haki yao ya maisha bora.
Mnamo Jumamosi usiku, vikosi vya jeshi la Afghanistan na Pakistan vilishiriki katika mapigano ya mpakani, wakishambuliana nafasi za kila mmoja kwenye Mstari wa Durand; matokeo yake, pande zote mbili za Waislamu zilipata hasara. Siku mbili kabla ya hapo, jeshi la Pakistan lilikuwa limeshambulia kwa mabomu maeneo fulani katika miji ya Kabul na Paktika, na kusababisha hasara zake zenyewe.
Chini ya ufadhili wa shirika la Ufaransa la Promediation, vyama vya kisiasa vya Sudan vilifanya warsha jijini Port Sudan, kama ilivyoripotiwa kwenye tovuti ya Sudan Tribune mnamo tarehe 5 Oktoba 2025: “Warsha inalenga kufafanua vigezo vya mazungumzo ya mustakbali yatakayoongozwa na Sudan, ikiwemo washiriki wake, eneo, na dori ya upatanishi wa kimataifa, kulingana na msemaji wa kambi hiyo Mohammed Zakaria. Viongozi wa muungano huo walisisitiza haja ya muungano wa ndani ulioshikamana. Minni Arko Minnawi, mkuu wa kamati ya kisiasa ya umoja huo, alisema hatua ya pamoja kati ya viongozi wa kiraia na kijeshi ni muhimu kwa ajili ya utulivu.
Katika kipindi cha miaka 2 iliyopita, watu wa Gaza wamekuwa wakikabiliwa na mashambulizi ya mabomu, mzingiro wa kikatili na jinai za kutisha zaidi za umbile la mauaji la Kiyahudi, ambapo wanawake na watoto wamekuwa wahanga wakuu. 65,000 wameuwawa, wakiwemo zaidi ya watoto 20,000 – sawa na watoto 30 wanaouawa kila siku. Watoto wamepigwa risasi kimakusudi na wavamizi wa Kiyahudi au mashambulizi ya droni barabarani, au hata wanapotafuta chakula kwenye vituo vya misaada ambavyo vimekuwa ‘mitego ya kifo’ kwa wanaokabiliwa na njaa. Kulingana na ‘Save the Children’, watoto waliuawa au kujeruhiwa katika zaidi ya nusu ya mashambulizi mabaya katika maeneo ya usambazaji wa chakula mjini Gaza ndani ya wiki nne baada ya Wakfu wa Kibinadamu wa Gaza kuanza shughuli zake.
Mazungumzo ya awamu ya kwanza ya mpango wa Rais wa Marekani Donald Trump kusimamisha vita dhidi ya Gaza yalianza mjini Sharm El-Sheikh nchini Misri, kwa kuhudhuriwa na wajumbe wa Marekani Steve Witkoff na Jared Kushner, Waziri Mkuu wa Qatar, na wakuu wa kijasusi wa Uturuki na Misri.