Jumapili, 16 Safar 1447 | 2025/08/10
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

Watoto Wanakufa kwa Njaa... Huku Watawala Wakiendelea na Uzembe wao!

Mkurugenzi Mkuu wa Wizara ya Afya ya Palestina mjini Gaza, Dkt. Munir Al-Barsh, alifichua kuongezeka kwa idadi ya watoto wanaokufa kwa njaa, na kuthibitisha kwamba uvamizi "unafurahi kuwaua," huku kukiwa na mzingiro unaoendelea, kufungwa kwa vivuko, na kupuuza mfumo wa kimataifa. Katika mahojiano katika Chaneli ya Al Jazeera, Al-Barsh alisema kuwa idadi ya watoto waliouawa shahidi kutokana na utapiamlo uliokithiri imefikia 66 hadi sasa, kati yao wa hivi punde ni mtoto mchanga wa miezi mitatu Jouri Al-Masri, akibainisha kuwa makundi yaliyo hatarini zaidi, hasa miongoni mwao ni watoto, wamekuwa wahanga wakuu.

Soma zaidi...

Marekani Yapanga Mpango Mpya baada ya Mpango wa Awali Kufichuliwa na Kutibuliwa na Umma

Makundi yenye silaha ya Rohingya yameanza kusajili kutoka kambi za wakimbizi za Cox's Bazar kusaidia katika mapigano dhidi ya Jeshi la Arakan huko Rakhine. Taarifa hiyo ilifichuliwa katika ripoti moja ya Shirika la Kimataifa la kutatua Migogoro yenye kichwa "Bangladesh/Myanmar: Hatari za Waasi wa Rohingya". Ripoti hiyo inabainisha kuwa, baada ya Jeshi la Arakan kupata ushindi dhidi ya jeshi la Myanmar huko Rakhine, makundi ya Rohingya yamezidi kuwa changamfu na yamekubali kufanya kazi kwa pamoja dhidi ya Jeshi la Arakan, kundi ambalo lenye Mabudha wengi wa Rakhine kuwa kambi yake. (The Business Standard, 18 Juni 2025)

Soma zaidi...

Mjadala juu ya Upandaji wa Malori ya Kuhitimu Unafichua Chuki iliyokithiri ya Vyombo vya Habari na Wanasiasa wa Denmark dhidi ya Uislamu

Wiki hii iliyopita kumeshuhudiwa vurumai kubwa la vyombo vya habari na kisiasa kutokana na machapisho ya mitandao ya kijamii ambapo Waislamu waliwapongeza wahitimu wa mwaka huu huku pia wakiwasilisha mtazamo wa Kiislamu kuhusu kupanda malori ya kuhitimu yenye sifa ya ulevi na tabia mbaya.

Soma zaidi...

Utambuzi wa Urusi wa Serikali ya Afghanistan: Hatua Zaidi ya Kuzuia Kuibuka kwa Mfumo wa Kiislamu katika Kanda hii

Afisi ya Habari ya Hizb ut Tahrir / Wilayah Afghanistan inauona utambuzi huu kama sehemu ya mchakato mpana ambao kwao utawala wa sasa utayeyushwa hatua kwa hatua ndani ya mfumo wa kimataifa wa kisekula wa dola ya kitaifa. Mfumo huu, baada ya muda, utaiweka mbali serikali hii na lengo kuu la Kiislamu la kusimamisha na kubeba Dini ya Mwenyezi Mungu (swt). Zaidi ya hayo, utambuzi huo unaweza kuigeuza Afghanistan kuwa uwanja wa vita vya kiushindani kati ya dola za kikanda na kimataifa.

Soma zaidi...

Hizb ut Tahrir / Wilayah Bangladesh Iliandaa Maandamano na Matembezi ya kupinga Uhamishaji wa India wa Waislamu hadi Bangladesh kwa Mtutu wa Bunduki

Hizb ut Tahrir / Wilayah Bangladesh, iliandaa maandamano na matembezi leo (Ijumaa, 4 Julai 2025) baada ya swala ya Ijumaa katika misikiti mbalimbali ya Dhaka na Chittagong kupinga uhamishaji unaoendelea wa India wa Waislamu hadi Bangladesh kwa mtutu wa bunduki. Wanachama mbalimbali wa Hizb ut Tahrir walitoa hotuba katika maandamano hayo ambayo yalimalizika sambamba na matembezi.

Soma zaidi...

Uhamishaji wa Dola ya Hindutva ya India wa Waislamu hadi Bangladesh kwa Mtutu wa Bunduki ni Uadui wa Wazi kwa Waislamu kama ule wa Umbile Haramu la Kiyahudi

Serikali ya Hindutva ya Modi inaendelea kuongeza kiwango cha ukandamizaji na mateso, ikiwa ni pamoja na kubomoa nyumba za Waislamu wa India na kuwapeleka uhamisho kwa nguvu usio wa haki. Kupitia hili kimsingi wanafuata nyayo za dola haramu ya Kiyahudi ‘Israel’. Hivi karibuni, hata wanawatendea Waislamu wa India kama wanyama kwa kuwaita wahamiaji haramu na kuwarudisha mamia yao nchini Bangladesh kwa mtutu wa bunduki, wakipuuza kile kinachoitwa michakato yao ya kisheria ya kitaifa na kimataifa. "Walitutendea kama wanyama," alisema mwanamke mmoja anayeitwa Rahima Khatun. "Tulipinga kwamba sisi ni Wahindi, kwa nini tuingie Bangladesh? Lakini walituelekezea bunduki na kutishia, 'Ikiwa hamtakwenda kwa huko, tutakupigeni risasi.' Baada ya kusikia milio minne ya risasi kutoka upande wa India, tuliogopa sana na haraka tukavuka mpaka kwa miguu". [Ripoti ya FP].

Soma zaidi...

Mwaliko wa Kuhudhuria na Kushiriki katika Kikao cha Masuala ya Ummah

Sisi, katika Hizb ut Tahrir / Wilayah Sudan, tunafuraha kuwaalika wanataaluma wa vyombo vya habari, wanasiasa, na wale wanaohusika na masuala ya umma kuhudhuria na kushiriki katika Kikao cha Masuala ya Ummah wa kila mwezi, ambacho mwezi huu kitakuwa na kichwa: “Hatari ya Kuyatazama Mamlaka Kama Keki Inayopaswa Kugawanywa”

Soma zaidi...

Haya ndiyo Matendo ya Umoja wa Mataifa... Mutaendelea Kuwahadaa Wananchi Mpaka Lini? Ni Kipi Kipya? Yako wapi Mabadiliko, Ee Wizara ya Ujenzi na Mabadiliko?

Mnamo Jumapili, tarehe 29/6/2025, jijini Sana'a, Waziri wa Masuala ya Kijamii na Leba, Samir Baja'ala, alifanya mkutano na kamati za maandalizi ya Kongamano la Vyama vya Ushirika la 2025, litakaofanyika mapema Julai 2025. Mkutano huo ulihudhuriwa na Ali Al-Razami, Katibu Mdogo wa Wizara ya Sekta ya Maendeleo na Nasser Al-Kahili, Mkurugenzi wa Afisi ya Masuala ya Kijamii na Afisi ya Leba katika Sekretarieti Kuu.

Soma zaidi...

Trump na Netanyahu Wanajigamba na Kujisifu Huku Watawala Wetu Wakikaa Kimya Mithili ya Wafu Makaburini Mwao!

Vita kati ya Iran na umbile la Kiyahudi vimemalizika, na jinai za Mayahudi mjini Gaza hazikukoma wakati wa vita hivyo, wala hadi wakati huu. Marekani ilifanya ujanja wa kiusanii, ikidai kuwa imeangamiza uwezo wa nyuklia wa Iran. Hatua hii imekuja baada ya Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran kukutana na wale wanaojiita mawaziri wa Troika wa Ulaya, ambao walikuwa sehemu ya mazungumzo ya nyuklia ya Iran kabla ya Marekani kujitoa katika mazungumzo hayo wakati wa muhula wa kwanza wa Trump. Iran pia ilifanya mbwembwe za kiusanii kwa kurusha makombora kadhaa katika Kambi ya Kimarekani ya Al Udeid nchini Qatar, baada ya kuifahamisha Marekani kuhusu hilo, kama Trump mwenyewe alivyosema.

Soma zaidi...
Jiunge kwa hii RSS feed

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu