Vipi Tunaweza Kuwa Miongoni Mwa Wenye Mafanikio hapa Duniani na Akhera?
- Imepeperushwa katika Uchambuzi
- Kuwa wa kwanza kutoa maoni!
- |
Mafanikio yanazunguka ulimwengu huu na Akhera, anayemcha Mwenyezi Mungu (swt) humsahilishia mambo yake, hubariki matendo yake, huitengenezea nafsi yake, mke wake na watoto wake, humpa njia ya kutokea katika matatizo, humruzuku kutoka katika vyanzo asivyotarajia, na humtosheleza. Zaidi ya hayo, Yeye (swt) humlipa sana subira yake wakati wa matatizo. Wengine wamesema: "Mafanikio ni kupata ushindi na kufikia lengo la mtu. Katika dunia hii, maana yake ni kupata furaha inayoleta kutosheka katika maisha. Katika Akhera, ina jumuisha mambo manne: uwepo milele usio na mwisho, heshima bila fedheha, mali bila umasikini, na elimu bila ya ujinga."