Ijumaa, 04 Dhu al-Qi'dah 1446 | 2025/05/02
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

Machafuko na Ghasia nchini Sudan Kusini Zinasisitiza Haja ya Umma kuwa na Kiongozi mwenye Kuwalinda

Ulimwengu umefuatilia machafuko ya Juba, mji mkuu wa Sudan Kusini, ambayo yalilenga watu waliokimbia makaazi yao na wakaazi kutoka Sudan Kaskazini. Matukio haya yalichochewa na ripoti zinazowatuhumu wanajeshi wa Sudan kwa kuwaua watu kutoka Sudan Kusini huko Wad Madani baada ya jeshi kuutwaa tena mji huo. Kulingana na gazeti la ‘Sudan Tribune’, Wasudan watatu waliuawa mjini Juba, na wengine saba kujeruhiwa.

Soma zaidi...

Baada ya Kutazama Tu Mauaji ya Kinyama kwa Siku 467, Watawala wa Pakistan Sasa Wanasherehekea Usitishaji Vita

“Watu wa Pakistan wanaungana nami katika kukaribisha tangazo la usitishaji mapigano uliosubiriwa kwa muda mrefu nchini Palestina,” Waziri Mkuu wa Pakistan, Shehbaz Sharif, aliandika kwenye ukurasa wa Twitter mnamo tarehe 16 Januari 2025. Hata hivyo, ukweli ni kwamba, kwa zaidi ya mwaka mmoja, utawala wa Munir-Sharif umekuwa ukitizama tu vifo na uharibifu huko Gaza, ambako mauaji ya halaiki ambayo hayajawahi kuonekana yalitokea, na walionusurika sasa kuganda kwa baridi hadi kufa. Walikuwa wakiyatazama haya yote, kana kwamba Pakistan haina jeshi kubwa zaidi katika Ulimwengu wa Kiislamu, na kana kwamba jeshi hilo nimeundwa kwa watu wasio na uwezo, dhaifu, waoga na vilema, kwa hivyo watawala hawawezi kufanya chochote kujibu ukatili huu isipokuwa kulaani, kushutumu na kupinga.

Soma zaidi...

Watawala Vibaraka Wana Hofu juu ya Tishio kwa Viti vyao vya Utawala lakini Hawana Wasiwasi juu ya Vita vya Mauaji ya Halaiki!

Mnamo Jumanne na Jumatano, wizara za mambo ya nje za Jordan, Saudia, Imarati, Mamlaka ya Palestina na Jumuiya ya Nchi za Kiarabu zililaani uchapishaji wa akaunti rasmi unaohusiana na umbile la Kiyahudi wa ramani za kanda hiyo ambazo ni pamoja na maeneo ya ardhi za Palestina zinazokaliwa kwa mabavu, Jordan, Lebanon na Syria, wakidai kwamba hayo ni ramani ya kihistoria ya umbile la Kiyahudi. Walionyesha wasiwasi wao kuhusu masuala mawili.

Soma zaidi...

Unafiki wa Kisiasa katika Demokrasia Kamwe Hautaisha Mpaka Tuubadilishe kwa Siasa za Kiislamu

Mnamo tarehe 06/01/2025, rufaa ya aliyekuwa Waziri Mkuu wa Malaysia, Datuk Seri Najib Tun Razak kuhusu kuwepo kwa amri ya nyongeza ya Mfalme, inayomruhusu kutumikia kifungo chake kilichosalia chini ya kifungo cha nyumbani, imekubaliwa na mahakama kwa wingi wa 2-1. Majaji wa Mahakama ya Rufaa kisha wakaamuru kesi hiyo irudishwe katika Mahakama Kuu ili ombi la Najib la uhakiki wa mahakama lisikizwe na jaji mpya. Amri hii ya nyongeza, ambayo ni sehemu ya mchakato wa msamaha wa kifalme, imekuwa jambo la kawaida, ambalo halijawahi kutokea katika asili yake. Sambamba na hilo, kulikuwa na jambo jengine - mkusanyiko mkubwa wa kuonyesha mshikamano uliokusanyika nje ya mahakama, ulioandaliwa na vyama ambavyo hapo awali vilikuwa wapinzani wa kisiasa wa Waziri Mkuu huyo wa zamani.

Soma zaidi...

Kuganda Baridini hadi Kufa kwa Watoto Wachanga, na Njaa na Uuaji wa Watoto Hayatoshi Kukomesha Mauaji ya Halaiki huko Gaza!

Mnamo tarehe 30 Disemba, iliripotiwa kuwa mtoto wa 6 waliganda hadi kufa mjini Gaza ndani ya wiki mbili kutokana na hali ya baridi inayovumiliwa na wakimbizi wa Kipalestina katika mahema ya muda, waliohamishwa kutoka kwa nyumba zao kutokana na mashambulizi ya mara kwa mara ya Ukanda huo na uvamizi wa Kiyahudi. Ali al-Batran mwenye umri wa mwezi mmoja alifariki siku moja baada ya kaka yake pacha, Jumaa al-Batran, huko Deir el-Balah. Baba yao, Yahya Muhammad al-Batran, alisema kuwa Jumaa alipatikana kichwa chake kikiwa kama “donge la barafu”. Nariman, mama wa Sila Mahmoud al-Fassih mwenye umri wa siku 20, ambaye pia alifariki kutokana na kupungua kwa joto la mwili, alielezea kumkuta mtoto wake akiwa rangi ya bluu na kuuma ulimi wake huku damu ikimtoka mdomoni. Zaidi ya watu milioni 1.6 wa Gaza wamelazimishwa kuingia kwenye makaazi ya muda, wakiishi katika mahema hafifu ambayo hayatoi ulinzi kutokana na hali ya hewa ya baridi kali.

Soma zaidi...

Hakuna Tofauti Kati ya Uhalifu wa huko New Orleans na Ukatili Unaofanywa na Umbile la Kizayuni huko Gaza

FBI imefichua utambulisho wa mhusika wa shambulizi la kugonga na gari huko New Orleans, Marekani, ambalo lilisababisha vifo na majeruhi ya makumi ya watu wakati wa sherehe za mwaka mpya. Mshambuliaji huyo alitambuliwa kama askari wa zamani wa Wanamaji. Mamlaka mjini New Orleans ziliripoti vifo vya watu 10 na wengine 30 kujeruhiwa baada ya lori kuingia kwenye umati wa watu. Vyombo vya habari vya Marekani viliripoti kwamba watu kadhaa walipoteza maisha baada ya gari hilo kugonga mkusanyiko wa watu kwenye Barabara ya Bourbon katika Mtaa wa Wafaransa wa New Orleans mnamo siku ya Jumatano. Wakati huo huo, Wizara ya Mambo ya Nje ya “Israel” ilisema kwamba “Waisraeli” wawili walijeruhiwa katika tukio hilo.

Soma zaidi...

Uchumi wa Kibepari Unasambaratisha Familia na Misingi yake

Warsha ya karibuni ya kinachoitwa ‘usawa wa kijinsia’ iliyofanyika ndani Ngorongoro, Kaskazini mwa Tanzania iliibua suala la uwepo baadhi ya wanandoa kutoka katika jamii za wafugaji ambao wametelekezwa na waume zao walioondoka vijijini kwenda mijini kutafuta kazi, na wakati mwengine waume hao hawarudi katika familia zao.

Soma zaidi...

Hotuba Inayohusu Bendera za Rayah na Liwaa za Mtume (saw) Ilipambwa kwa Takbira na Machozi katika Soko Kuu la Port Sudan

Hizb ut Tahrir / Wilayah Sudan ilitoa hotuba yake ya kisiasa ya kila wiki, iliyokuwa na kichwa: “Je, Mtume (saw) alikuwa na bendera na Rayah?”, mnamo Jumatatu tarehe 28 Jumada al-Akhirah 1446 H sawia na 30/12/2024 M. Ustadh Muhammad Jami’ (Abu Ayman), Msaidizi wa Msemaji Rasmi wa Hizb ut Tahrir katika Wilayah ya Sudan, alizungumza akisisitiza kuwa bendera ya Liwaa na Rayah katika Uislamu ni suala la dini, itikadi, mfumo na nembo ya Uislamu. Mtume (saw), ana benera (Liwaa) nyeupe kama bendera ya amiri jeshi, na bendera (Rayah) nyeusi kwa makamanda wa majeshi na vikosi, na inaitwa Uqab, zimeandikwa juu yazo “La Ilaha illa Allah Muhammad Rasulullah”.

Soma zaidi...

“Mayahudi Hawawi Radhi Nawe, Wala Wakristo, Mpaka Ufuate Mila Yao” [Al-Baqarah: 120]

Utawala mpya nchini Syria umetoa taarifa mtawalia kuhusu mfumo wa serikali ambayo wananuia kutekeleza baada ya dhalimu kutoroka. Ni wazi kuwa si mfumo aliouweka Mwenyezi Mungu (swt) bali ni mfumo wa kisekula unaotenganisha dini na maisha kwa kisingizio cha kuwapa watu uhuru wa kuchagua mfumo wa utawala. Wanawaruhusu waandamanaji wa kike wanaodai uhuru na kuvua hijab, huku wakiwateka nyara waandamanaji wasafi wanaodai kuachiliwa kwa jamaa zao wanaotaka kutabikishwa kwa Shariah ya Mwenyezi Mungu (swt)!

Soma zaidi...

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu