Alhamisi, 05 Rajab 1447 | 2025/12/25
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

Mauaji Mapya Yatekelezwa na Umbile Halifu la Kiyahudi katika Kambi ya Ain Al-Hilweh!

Katika muktadha wa kile ambacho Amerika inaendesha katika suala la amani na uhalalishaji mahusiano nchini Lebanon na eneo hili—ambapo kiuhalisia ni kusalim amri na kujisalimisha—umbile halifu nyakuzi la Kiyahudi, pamoja na silaha za Marekani, risasi za Ulaya, mikono ya Kiyahudi, na ushirika rasmi wa Waarabu, lililipua uwanja wa michezo na klabu ya michezo katika kambi ya Ain al-Hilweh katika mji wa Sidon kusini mwa Lebanon mnamo Jumanne, 18/11/2025. Mashahidi kumi na tano waliauwawa katika shambulizi hili la kikatili, na makumi ya watoto na raia walijeruhiwa, katika shambulizi baya linalothibitisha uhalifu wa umbile la Kiyahudi na uadui wake dhidi ya Waislamu.

Soma zaidi...

Hukumu ya Kifo kwa Hasina: Udhalimu wa Kisekula Uliomuunda Hasina Ungalipo

Mahakama ya Kimataifa ya Jinai (ICC) imetoa hukumu ya kifo ya kihistoria dhidi ya mtawala wa Bangladesh aliyeondolewa madarakani Sheikh Hasina. Kwa watu waliokandamizwa wa Bangladesh, uamuzi huu unatoa uthibitisho wa kiishara uliochelewa kwa muda mrefu na unasimama kama shtaka lenye nguvu kwa utawala uliokanyaga ubinadamu wa kimsingi. Lakini uamuzi huu unahitaji tafakari ya kina, sio sherehe tu. Haki ya kweli inahitaji mabadiliko ya kimfumo, sio adhabu ya mtawala dhalimu tu. Chanzo kikuu ni mfumo wa kimataifa unaoongozwa na Marekani, ambao unahubiri demokrasia huku ukitekeleza ‘mantiki ya siasa za kijiografia’.

Soma zaidi...

Ukosefu wa Masuluhisho ya Kudumu kwa Mgogoro wa Rohingya

Gazeti la ‘South China Morning Post’ liliripoti mnamo tarehe 10 Novemba kwamba Umoja wa Mataifa umeonya kwamba Kusini-mashariki mwa Asia kuna hatari ya “janga jengine la kibinadamu” ikiwa uvukaji wa bahari wa wakimbizi waliokata tamaa utaendelea bila kudhibitiwa. Vifo vya watu wasiopungua 21, wakiwemo watoto kadhaa, katika ajali ya boti karibu na pwani ya Malaysia vimeibua hofu ya kuongezeka tena kwa uvukaji hatari wa bahari wa wakimbizi wanaokimbia mzozo nchini Myanmar na hali mbaya katika nchi jirani ya Bangladesh. Kulikuwa na miili 12 iliyopatikana nchini Malaysia na tisa katika nchi jirani ya Thailand – kulingana na mkuu wa eneo wa shirika la bahari la Malaysia, Romli Mustafa.

Soma zaidi...

‘Mkataba wa Mageuzi ya Julai: Udanganyifu Mkubwa’: Hizb ut Tahrir Yalaani Mkataba huo, na Kuhimiza Badali Msingi ya Kisiasa kwa Demokrasia Iliyofeli

Katika kujibu hotuba ya hivi karibuni ya Mshauri Mkuu Profesa Yunus kuhusu utekelezaji wa Mkataba wa Kitaifa wa Julai na kura ya maoni kuhusu mapendekezo ya mageuzi ya katiba katika Mkataba huo, Hizb ut Tahrir / Wilayah Bangladesh inatoa onyo kali kwamba mapendekezo ya mageuzi na mchakato wake wa utekelezaji si kitu zaidi ya hatua ya juu juu ambayo inashindwa kushughulikia sababu za msingi za mgogoro wa kisiasa wa Bangladesh. Inatoa udanganyifu wa mabadiliko ili kuhifadhi dhati ya mfumo wa kidemokrasia uliofeli.

Soma zaidi...

Ni Khilafah Rashida pekee kwa Njia ya Utume ndiyo itakayong'oa Mizizi ya Ukoloni wa Magharibi kutoka Ardhi Zetu

Kwa mwaliko wa Balozi wa Uingereza, Kumar Iyer, pamoja na Ujerumani, Ireland, Uholanzi, na Norway, Baraza la Haki za Binadamu la Umoja wa Mataifa lilifanya kikao mnamo Ijumaa, 14/11/2025, kuhusu ukiukaji katika mji wa El-Fasher. Baraza hilo lilipitisha kwa kauli moja azimio linaloiamuru Misheni Huru ya Kutafuta Ukweli, ambayo Baraza lilikuwa limeianzisha mnamo 11/10/2023, kuchunguza ukiukaji uliofanywa katika mji huo, ambapo Baraza liliamuru kuwatambua wote waliohusika, ili kusaidia kuwafikisha mbele ya sheria. Na kama mwendelezo wa mbinu yake ya kukataa misheni hii tangu kuanzishwa kwake, Waziri wa Sheria, Abdullah Darf, alitangaza katika mahojiano na tovuti ya habari ya uchunguzi jana, Jumapili 16/11/2025, kwamba “Sudan inakataa kupeleka uchunguzi kuhusu uhalifu wa Vikosi vya Msaada wa Haraka huko Al-Fashir kwa Kamati ya Kutafuta Ukweli.”

Soma zaidi...

Pakistan, Nchi Safi, Haiwakaribishi Wala Haiwasalimu Vizazi vya Khiyana vya Wasaliti

Baada ya kimya cha wafu makaburini cha serikali za vibaraka zinazobebesha mzigo ardhi za Waislamu, kuhusu mauaji ya Kiyahudi mjini Gaza kwa zaidi ya miaka miwili, vibaraka wa Amerika na Uingereza, washirika wa Mayahudi, walianza kuchukua hatua na kuwa wachangamfu katika kutekeleza mpango wa Trump wa kufilisi kile kilichobaki cha upinzani huko Palestina, kukandamiza na kuua watu mjini Gaza, na kubomoa kile ambacho Mayahudi hawakubomoa cha mawe. “Jenerali anayependwa zaidi wa Trump” Asim Munir alitembelea Jordan mnamo 26 Oktoba, na kwa badali yake, mnamo 16 Novemba 2025, Mfalme Abdullah II bin Al-Hussein, Mfalme wa Ufalme wa Hashimiya wa Jordan na Kamanda Mkuu wa Vikosi vya Wanajeshi wa Jordan, alitembelea Pakistan, akifuatana na binti yake Salma binti Abdullah II bin Al-Hussein, na ujumbe wa maafisa wa kiraia na kijeshi wa Jordan.

Soma zaidi...

Hotuba ya Msemaji Rasmi wa Hizb ut Tahrir / Wilayah ya Sudan katika Mkutano na Waandishi wa Habari yenye kichwa: Makubaliano ya Nchi Nne (Quartet) ya Kusitisha Mapigano na Hatari ya Mazungumzo kwa Msingi wa Hadhara ya Kimagharibi

Tangu Quartet—ambayo inajumuisha sambamba na Amerika, Saudi Arabia na Misri na Imarati, ilipotangaza taarifa yake mnamo 12/9/2025 kuhusu mgogoro wa Sudan, watu wengi nchini Sudan wamegawanywa katika mikondo miwili: mkondo unaounga mkono taarifa ya Quartet inayotaka mazungumzo na suluhisho la kisiasa, kwa kisingizio kwamba inaleta amani, na mkondo mwengine unaosema unakataa kile kilichokuja katika taarifa ya Quartet, na kutaka kuendelea kwa vita. Na ijapokuwa pande zote mbili ni Waislamu, hawakuufanya Uislamu kuwa ndio msingi wa kutoka kwao katika kubainisha misimamo yao, wakati ilitakiwa hapo awali jambo hili litokee

Soma zaidi...

Masanduku ya Kura katika Mfumo Fisadi Ndio Udanganyifu Mkubwa Zaidi kwa Mabadiliko

Tangu Marekani ilipovamia mwaka wa 2003 hadi sasa, Iraq imekuwa ikizama katika matatizo, na hali yake inazidi kuwa mbaya. Yote hayo ni matokeo ya ramani ya kisiasa ambayo mvamizi Marekani aliiunda na kuilazimisha. Ndiyo iliyoweka misingi ya mfumo huo na kuchora ramani ya kisiasa ya nchi hii, ikiudanganya umma wa Iraq kuamini kwamba suluhisho la matatizo yanayozalishswa na mfumo huu ni masanduku ya kura.

Soma zaidi...

Enyi Waislamu: Maisha Yenu Yanawezaje Kuwa Mazuri Wakati Wanawake Walio Huru Wako Katika Magereza ya Mayahudi, Wakiteswa na Heshima Zao Zikivunjwa?!

Kituo cha Haki za Kibinadamu cha Palestina kilifichua, kulingana na ushuhuda mpya uliokusanywa na mawakili na watafiti wa kituo hicho kutoka kwa wafungwa kadhaa walioachiliwa huru kutoka Ukanda wa Gaza kutoka magereza na vituo vya uzuizi vya umbile la Kiyahudi, utaratibu na mpangilio wa mateso ya kingono, ikiwemo ubakaji, kuvua nguo, kulazimishwa kurekodi filamu, na unyanyasaji wa kingono kwa kutumia zana na mbwa, pamoja na udhalilishaji wa kisaikolojia wa makusudi unaolenga kuponda utu wa binadamu na kufuta kabisa kitambulisho cha mtu binafsi.

Soma zaidi...

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu