Alhamisi, 03 Dhu al-Qi'dah 1446 | 2025/05/01
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

Tukio la Jalalabad: Kuilinda Dawah ni Wajibu kwa Kila Mmoja Wetu

Mnamo tarehe 26 Novemba, Mashababu wa Hizb ut Tahrir waliandaa amali dhidi ya rasimu ya sheria ya “Uhuru wa Dini na Mashirika ya Kidini” katika eneo la Jalalabad. Wiki tatu baadaye, kati ya Disemba 10 na 14, Kamati ya Serikali ya Usalama wa Kitaifa ilifanya msako katika nyumba 21 katika eneo hilo na kuwaweka kizuizini kinyume cha sheria wanachama wa Hizb ut Tahrir. Vikosi vya usalama havikuruhusu wanachama waliozuiliwa (Mashababu) kukutana na mawakili wao na badala yake walifanya uchunguzi mbele ya mawakili waliofunzwa mahususi kwa kesi hii. Kutokana na hali hiyo, Mashababu wetu walizuiliwa kwa muda kwa kipindi cha mwezi mmoja kwa kisingizio cha kusambaza vipeperushi misikitini vinavyopinga sheria hiyo. Kesi ya jinai ilifunguliwa dhidi yao chini ya shtaka la “kuandaa na kuendesha shughuli za itikadi kali.”

Soma zaidi...

Mamlaka ya Palestina Yafuata Mbinu za Mashetani Kuhalalisha Uhalifu wake katika Kambi ya Jenin!

Mamlaka ya Palestina (PA) ilikusanya vyombo vyake vya habari na vipaza sauti vya wasemaji na nzi wa kielektroniki (wanyanyasaji wa mtandaoni wanaounga mkono serikali) ili kuchafulia jina kambi ya Jenin na watu wake na kuhalalisha umwagaji wa damu yao. Kisha, ilikusanya vyombo vyake na majambazi katika mji wa Khalil al-Rahman, na wachache wa wale walioitwa watu mashuhuri waliojiuza kwa PA kwa manufaa maovu, na wale ambao iliwatishia kutoka kwa wafanyikazi na walimu. Ilitumia wizara, shule zilizofungwa, na kukodi mabasi ili Jimbo la Khalil al-Rahman, mji na wilaya, ionekane kuwa pamoja nayo katika kumwaga damu ya watu wa kambi ya Jenin. Hii ijapokuwa inajua na wale walio nyuma ya kwamba Khalil al-Rahman, pamoja na watu wake na koo zake, hawawezi kukubali kwamba itoa nusu ya neno kumwaga tone la damu ya Waislamu. Kwa kitendo hiki kiovu, inataka kuleta mgawanyiko kati ya watu wa Palestina (kaskazini na kusini) chini ya pazia la uongo la uhalifu wake.

Soma zaidi...

Amerika ni Adui Yenu Dhahiri. Majaribio ya Kuidekeza ni Batili. Ni kwa Kusimamisha Khilafah Rashida Pekee, ndio Mnaweza Kuzima Faida ya Kimkakati ya Amerika na Kuipa Jibu Lililofaa!

Mnamo tarehe 21 Disemba, 2024, Afisi ya Mambo ya Nje ya Pakistan “ilipinga vikali ukosoaji wa Marekani wa mpango wa makombora wa masafa marefu wa Pakistan, na kuuita usio na mantiki na usio na muktadha wa kihistoria kwani iliapa kuendelea kukuza uwezo wake wa makombora sambamba na kiwango cha chini uzuiaji wake wa kuaminika wa kimkakati, ikisisitiza hitaji lao la kukabiliana na vitisho vinavyoibuka kutoka India.

Soma zaidi...

Maingiliano ya Ummah na Hotuba: “Khilafah Ndio Mfumo wa Utawala katika Uislamu”

Hizb ut Tahrir / Wilayah Sudan ilitoa hotuba ya kisiasa katikati mwa soko kuu la Port Sudan mnamo Jumatatu, 23 Disemba 2024, chini ya mada: “Khilafah Ndio Mfumo wa Utawala katika Uislamu.” Hotuba hiyo ilitolewa na Ustadh Yaqub Ibrahim mwanachama wa Hizb ut Tahrir ambaye alisisitiza kuwa Mwenyezi Mungu Mtukufu amewawajibisha Waislamu kutabikisha hukmu za Uislamu na kupangilia nyanja zote za maisha yao kwa mujibu wake. Alieleza kwamba utabikishaji huu hutokea kupitia Bay’a halali kwa Khalifa ambaye anasimamisha Dini na kuifikisha kwa ulimwengu.

Soma zaidi...

Mfano Hatari Ambao Haupaswi Kupuuzwa

Katika mfano hatari katika historia ya mapinduzi, Huduma Kuu ya Usalama mjini Aleppo iliteka nyara wanawake kumi mnamo siku ya Jumamosi, 21 Disemba 2024. Wanawake hao walikuwa wamejitokeza wakiandamana, wakitaka utawala wa Uislamu na kuachiliwa huru waume zao, vijana wao na watoto wao waliotekwa nyara zaidi ya mwaka mmoja na nusu uliopita. Watu hawa wamefungwa jela na Jolani [al-Julani] mjini Idlib tangu Mei 7, 2023!

Soma zaidi...

Mkutano wa Waandishi Habari juu ya Sarafu na Mshtuko wa Nixon

Kabla ya kuanzishwa kwa sarafu, watu walitumia ubadilishanaji wa bidhaa kwa huduma. Kwa kuwa dhahabu na fedha zimezingatiwa kuwa madini ya thamani yenye kima cha asili kwa binadamu tangu nyakati za zamani, zilitabanniwa kama pesa, huku sarafu zikichongwa kwazo ili kurahisisha ubadilishanaji. Dhahabu, hasa, inajulikana kwa kuhimili kwake kuharibika kwa muda mrefu.

Soma zaidi...

Mahouthi Wanaendelea na Jinai na Uhalifu wao... Kuwakamata Wanachama wa Hizb ut Tahrir

Kuanzia Alhamisi, tarehe 10 Jumada al-Akhir 1446 H sawia na tarehe 12 Disemba 2024 M, wanamgambo wa Houthi walifanya uvamizi kwenye nyumba za wanachama wa Hizb ut Tahrir bila ya kuzingatia vifungu vya sheria ya Kiislamu au hata kanuni na desturi za kikabila! Walivamia nyumba zao katika kurugenzi tatu za Jimbo la Taiz (Taiziyah, Mawiah, na Khadir); na kuwakamata: Suleiman al-Muhajri, Khaled al-Hami (waliyemwekwa kizuizini miezi sita iliyopita kwa tuhuma za kubeba Dawah pamoja na Hizb ut Tahrir), Mhandisi Taqi al-Din al-Zayla'i, Amir al-Sabry, na Muhammad al-Faqih. Wafuasi watatu wa Hizb ut Tahrir pia walikamatwa: Abdul Malik al-Jundi, Abdul Qader al-Sarari, na Adnan al-Zayla'i, ambao wanasalia chini ya ulinzi wa wahalifu hao mpaka kufikia wakati wa kuandika taarifa hii.

Soma zaidi...

Chini ya Urasilimali Utunzaji wa Afya huwa kama Fadhila tu wala Hauchukuliwi kuwa ni Haki Msingi

Serikali imeanzisha Mamlaka ya Afya ya Kijamii (SHA) ili kusimamia bima ya afya ya jamii nchini. SHA ina hazina tatu za kifedha: Hazina ya Huduma ya Afya ya Msingi, Hazina ya Bima ya Afya ya Jamii na ile ya hali ya Dharura na Ugonjwa hatari. Watoa huduma za afya nchini Kenya wanaweza kuingia katika kandarasi na mamlaka ya SHA ili kutoa huduma za afya kwa walengwa.

Soma zaidi...

Mapinduzi katika Ulimwengu wa Kiislamu Yatapelekea kwenye Mabadiliko ya Kweli Pale tu Watu wenye Nguvu Watakapotimiza Wajibu wao wa Shariah kwa Kuwaondoa Madhalimu na kuupa Nusra Ummah

Baada ya mabadiliko makubwa katika utawala wa Syria, baada ya mabadiliko ya utawala nchini Bangladesh na Afghanistan, pamoja na mabadiliko ya utawala yaliyokuja kabla ya haya, makundi tawala yanaendeleza simulizi ya zamani kwamba mapambano yaliyopangwa ya watu dhidi ya watawala yanazua “machafuko, ufisadi na ukosefu wa utulivu.” Iwe ni mkuu wa Jeshi la Pakistan, Jenerali Asim Munir, au watawala wengine, wote wanadai kwamba hawataruhusu nchi zao kuwa “Libya, Syria, Iraq au Sudan” nyengine.

Soma zaidi...

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu